Main Title
4 Februari 2023
Waislamu waadhimisha kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Imam Ali bin Abi Twalib (AS)
Iran imejiunga na uliwengu wa Kiislamu hii leo katika kuadhimisha siku ya kukumbuka kuzaliwa Amirul Muumin Ali (A.S) Imam wa Kwanza wa Waislamu wa Kishia ulimwenguni.

4 Februari 2023
Amnesty International: Saudia inaitumia vibaya michezo kufunika jinai zake
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa utawala wa Saudi Arabia unaitumia vibaya michezo kuficha rekodi yake chafu, ya maafa na ya kutisha ya haki za binadamu.

4 Februari 2023
Palestina yafichua: Ulaya inatushinikiza tuchukue msimamo wa kuilaani Russia
Waziri wa Mambo ya Nje wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amefichua kuwa Ulaya inaishinikiza Palestina ichukue msimamo wa kuilaani Russia sambamba na kueleza kwamba amepokea mwaliko kutoka kwa mwenzake wa Russia wa kuzuru Moscow.

4 Februari 2023
Malengo ya safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia nchini Iraq
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Saudi Arabia, Faisal bin Farhan Al-Saud, tarehe Pili Februari alitembelea Iraq. Safari hiyo ya Bin Farhan inaweza kutathminiwa katika kalibu ya masuala ya kikanda na kimataifa.

4 Februari 2023
Al-Nahdha: Kususiwa uchaguzi ni risala ya wazi ya wananchi wa Tunisia kwa utawala wa Kais Saied
Harakati ya al-Nahdha ya Tunisia imetangaza kuwa, hatua ya wananchi wengi wa nchi hiyo ya kususia uchaguzi na kutojitokeza katika duru ya pili ya uchaguzi wa Bunge uliofanyika hivi karibuni ni ujumbe wao wa wazi kabisa wa kutaka kuhitimishwa mapinduzi ya Rais Kais Saied.

4 Februari 2023
Iran yajibu uropokaji wa Macron, yamtaka azungumzie silaha za nyuklia za Israel
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa matamshi ghalati ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa aliyedai katika mazungumzo yake na Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel kuwa, eti Paris inatiwa wasiwasi na shughuli za nyuklia za Jamhuri ya Kiislamu.

4 Februari 2023
Iran yatoa mwito wa kupanuliwa uhusiano wake na Venezuela
Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Venezuela wametilia mkazo udharura wa kuzidisha uhusiano na ushirikiano wa pande mbili katika nyuga tofauti bila vizingiti.

4 Februari 2023
Iran: Wakiukaji wa kila siku wa haki za binadamu ni wabeba bendera ya uongo ya haki za binadamu
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, watu ambao ndio wakiukajii wakubwa wa kila siku wa haki za binadamu ulimwenguni, leo ni wabeba bendera ya uongo ya kutetea haki za binadamu.

4 Februari 2023
Onyo la Russia kwa Netanyahu kuhusu msaada wa silaha kwa Ukraine
Russia imeuonya vikali utawala haramu wa Israel baada ya Waziri Mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu kutangaza Jumatano usiku kwamba anachunguza suala la kutuma msaada wa kijeshi wa utawala huo nchini Ukraine.

4 Februari 2023
Mpakistan Majid Khan aachiwa huru na Marekani baada ya mateso na kusota gerezani Guantanamo kwa miaka 20
Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) imetangaza kuwa Majid Khan, mfungwa Mpakistani ambaye alifichua jinsi alivyoteswa na shirika la ujasusi la Marekani CIA baada ya mashambulizi ya Septemba 11, 2001, amehamishwa kutoka gereza la Guantanamo Bay nchini Cuba na kupelekwa Belize, nchi iliyoko Amerika ya Kati.

4 Februari 2023
UN: Watoto milioni 222 katika maeneo yaliyoathirika na migogoro wanahitaji msaada wa haraka wa elimu
Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaohusika na kufikisha elimu kwenye maeneo yenye majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait, ECW au kwa lugha ya Kiswahili, Elimu Haiwezi Kusubiri, pamoja na wadau wamesisitiza kuwa, umuhimu wa kusaidia mamilioni ya watoto walio katika mazingira ya migogoro ili waweze kupata elimu, wakisema elimu ndio ufunguo wa kuwakomboa watoto hao hususan wasichana katika maisha yao ya siku za usoni.

4 Februari 2023
Malaysia: Chuki dhidi ya Uislamu inapaswa kujinaishwa
Afisa mmoja wa ngazi ya juu wa Malaysia ametoa mwito wa kujinaishwa chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu.

3 Februari 2023
Mbunge Muislamu atimuliwa katika kamati ya bunge la Marekani kwa kupinga Israel
Wabunge wa chama cha upinzani cha Republican katika Baraza la Wawakilishi la Marekani (Congress) wamepiga kura ya kumtimua Ilhan Omar katika kamati muhimu ya bunge kutokana na kitendo cha mbunge huyo Muislamu cha kuwakejeli wanasiasa wa Marekani kutokana na uungaji mkono wao usio na msingi kwa utawala wa Israel mkabala wa kupokea malipo ya fedha.

3 Februari 2023
Iran yakosoa mtazamo wa nchi za Magharibi kuhusu haki za binadamu
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa mtazamo wa nchi za Magharibi kuhusu haki za binadamu kwa kuchapisha picha za mashahidi wa Kipalestina waliouawa na jeshi la Israel katika mwezi uliopita.

3 Februari 2023
Rais Ebrahim Raisi: Taifa la Iran muda wote limekuwa likiwakatisha tamaa maadui
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kujitokeza vilivyo na kwa wingi wananchi katika nyuga tofauti kumekuwa muda wote kukiwavunja moyo na kuwakatisha maadui wa Iran ya Kiislamu.

3 Februari 2023
Iran yakosoa ripoti 'isiyo sahihi' ya IAEA kuhusu kituo cha Fordow
Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amelalamikia ripoti ya hivi karibuni ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) kuhusu shughuli za nyuklia za kituo cha nyuklia cha Fordow nchini Iran na kusema tafsiri ya mkaguzi wa IAEA aliyetembelea kituo hicho cha nyuklia haikuwa sahihi.

3 Februari 2023
AI: Lazima utawala wa Israel uvunje mfumo wa ubaguzi wa rangi
Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema utawala wa Israel "lazima uvunje mfumo wa ubaguzi wa rangi au apathaidi ambao unasababisha mateso na umwagaji damu mkubwa" katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.

3 Februari 2023
Sababu za kuongezeka hukumu za kifo nchini Saudi Arabia baada ya Bin Salman kuingia madarakani
Shirika la Haki za Binadamu la Ulaya-Saudia, limetangaza katika ripoti ya karibuni kwamba hukumu za kifo au unyongaji wakati wa utawala wa mrithi wa kiti cha ufalme Mohammed bin Salman nchini Saudi Arabia zinaongezeka karibu mara mbili kila mwaka.

3 Februari 2023
Radiamali ya Iran kwa vitendo vya uhasama vya utawala wa Kizayuni na msimamo wa kichochezi wa Ukraine
Amir Saeed Irwani, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa, siku ya Jumatano, akizungumzia shambulio la kigaidi kwenye kiwanda cha Wizara ya Ulinzi huko Isfahan, amesema katika barua kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na pia kwa mwenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama kwamba uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa utawala wa Kizayuni umehusika na tukio hilo la kigaidi.

3 Februari 2023
OIC yaitisha kikao kulaani kuchomwa moto Qur'ani Tukufu
Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imeitisha imelaani jinai iliyofanywa na baadhi ya watu wenye misimamo mikali barani Ulaya ya kuchoma moto nakala ya Qur'ani Tukufu. hatua hiyo imechukuliwa katika kikao cha OIC ambacho kimejadili hatua zinazoweza kuchukuliwa dhidi ya watenda jinai hao.
