Main Title

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:30:53
1451872

Bunge la Marekani laionya Washington isijiingize kwenye vita vya kijeshi na Iran

Mkuu wa Kamati ya Kijasusi ya Bunge la Marekani amewaonya viongozi wa Washington kuhusu matokeo mabaya ya kujiingiza katika hatua yoyote ya kijeshi inayoweza kuchukuliwa dhidi ya Iran.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:30:27
1451871

Ramaphosa: Kama Israel haitodhibitiwa, vita vya Ghaza vinaweza kuenea ukanda mzima

Rais wa Afrika Kusini kwa mara nyingine ameonya kuhusu hatari ya vita vya Ghaza na kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wasio na hatia akisisitiza kuwa kama Israel haitodhibitiwa, basi vita hivyo vinaweza kuenea katika nchi zote za eneo hili.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:29:45
1451870

Russia yakumbwa na mafuriko; nyumba zaidi ya elfu 15 zazama majini

Maafisa wa Russia wa Idara ya Kukabiliana na Majanga ya Kimaumbile wameeleza kuwa idadi ya nyumba zilizozama kutokana na mafuriko nchini humo imepindukia 15,000.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:29:14
1451869

Mienendo ya chuki dhidi ya Uislamu yaongezeka nchini Ujerumani

Vyombo vya habari vya Ujerumani, vimenukuu ripoti zilizochapishwa na serikali ya nchi hiyo, na kuripoti kuwa uhalifu dhidi ya Waislamu nchini humo uliongezeka mwaka 2023 ikilinganishwa na miaka ya kabla yake.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:28:38
1451868

Trump, rais wa kwanza wa zamani Marekani kuhukumiwa katika kesi ya jinai

Kesi ya Donald Trump katika mashtaka ya jinai ilianza jana, Jumatatu, mjini New York na kumfanya kuwa rais wa kwanza wa zamani wa Marekani kufika mbele ya mahakama ya jinai kujibu mashtaka yanayohusiana na kulipa pesa kwa mwigizaji wa filamu za ngono ili kumnyamazisha na kumtaka afiche uhusiano wake wa kingono na mwanamke huyo.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:28:15
1451867

Kikao cha Baraza la Usalama: Uwanja wa makabiliano kati ya waungaji mkono wa Iran na Wamagharibi wanaounga mkono utawala wa Kizayuni.

Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujadili mashambulizi ya Iran ya kuuadhibu utawala wa Israel kilifanyika Jumapili jioni tarehe 14 Aprili, kikao ambacho kilibadilika na kuwa uwanja wa makabiliano kati ya nchi zinazounga mkono Iran na kambi ya Magharibi waitifaki wa utawala wa Kizayuni.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:27:25
1451866

Tehran yaitaka UN ilaani shambulio la Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina wajibu wa kulaani shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:26:47
1451865

Abdollahian amwambia Guterres: Hatukuwa na njia nyingine isipokuwa kuiadhibu Israel

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, operesheni ya jeshi la Iran dhidi ya maeneo ya kijeshi ya utawala ghasibu wa Israel imefanyika ndani ya fremu ya kujilinda na kwa mujibu wa sheria za kimataifa.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:26:06
1451864

Amir-Abdollahian: Iran haitoruhusu Israel kuhatarisha usalama wa ukanda huu

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaamini kwamba usalama na utulivu wa nchi za eneo hili zima ni muhimu sana kwake, bali ni sawa kabisa na usalama wake yenyewe na haitoruhusu utawala wa Kizayuni kuhatarisha usalama wa eneo hili kwa chokochoko zake.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:25:30
1451863

Ebrahim Raisi: Hatua yoyote dhidi ya Iran itapata majibu makali

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hatua yoyote hata ndogo kiasi gani itakayochukuliwa dhidi ya manufaa ya Iran, bila ya shaka yoyote itapata majibu makali na ya kuumiza kwa wote watakaohusika na hatua hiyo.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:25:08
1451862

Mgogoro ulioanzishwa na utawala wa Kizayuni; matokeo ya utawala wa Netanyahu na baraza lake la mawaziri

Kanali ya 12 ya utawala wa Kizayuni imesema kwenye tovuti yake kwamba Netanyahu ni mwongo na kwamba ameuletea madhara makubwa ya kiusalama utawala ghasibu wa Israel kwa kushindwa kijeshi katika Ukanda wa Gaza, kuzusha migogoro mbalimbali katika eneo na kuwa leo hii utawala huo unakabiliwa na matatizo ya pande zote.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:24:44
1451861

Vyombo vya habari vyafichua jinai ya Wazayuni katika Hospitali ya al-Shifa huko Gaza

Vyanzo vya habari vimevichua na kuweka wazi jinai kubwa iliyofanywa na askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Hospitali ya al-Shifa huko Gaza baada ya kufukuliwa miili ya mashahidi wa Kipalestina waliouawa na kuzikwa na wanajeshi wa utawala huo haramu.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:24:02
1451860

Wazayuni wanakwepa kurejea maeneo wanayoishi kwa kuhofia mashambulio ya Hizbullah

Televisheni ya utawala wa Kizayuni wa Israel imefichua kuwa, sehemu kubwa ya Wazayuni wanaoishi kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni, wanakwepa kurejea maeneo hayo wakihofia mashambulio ya Hizbullah ya Lebanon.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:29:37
1451638

Russia yakosoa kimya cha Baraza la Usalama baada ya shambulio la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran, Syria

Russia imekosoa hatua ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ya kushindwa kuchukua hatua inayofaa baada ya utawala wa Israel kushambulia jengo la ubalozi mdogo wa Iran huko Damascus mji mkuu wa Syria.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:28:26
1451636

Mwakilishi wa Russia UN: Baraza la Usalama linafanya kazi kinafiki

Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amekitaja kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na jibu la makombora na ndege zisizo na rubani la Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa ni msimamo wa kinafiki na hadaa wa nchi za Magharibi.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:27:55
1451634

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Iran haitasita kulinda maslahi yake

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitasita wala kuwa na shaka katika kulinda maslahi yake halali dhidi ya uchokozi wowote mpya.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:27:34
1451632

Iran yaionya tena Marekani dhidi ya kuchukua hatua za kijeshi

Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa ameionya Marekani kuhusu kuanzisha hatua za kijeshi dhidi ya Iran baada ya operesheni yake ya kisheria ya hivi karibuni ya kulipiza kisasi dhidi ya utawala ghasibu wa Israel, mshirika mkuu wa kieneo wa Washington.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:27:10
1451631

Shehena ya mbolea ya kemikali iliyotengenezwa na utawala wa Kizayuni yakamatwa kaskazini magharibi mwa Iran

idara ya Forodha ya Iran imetangaza kuwa imezuia shehena ya mbolea ya kemikali iliyotengenezwa katiika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) iliyokuwa ikisafirishwa huko kaskazini magharibi mwa Iran.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:26:47
1451630

Amir Abdollahian: Iran haikuwa na budi ila kuuadhibu utawala wa Kizayuni ndani ya fremu ya kujilinda halali

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haikuwa na budi ila kuutia adabu utawala wa Kizayuni katika fremu ya kujilinda halali kufuatia Umoja wa Mataifa kunyamaza kimya na kushindwa kuchukua hatua za kidplomasia huku Baraza la Usalama la umoja huo likishindwa hata kutoa tamko la kulaani shambulio la utawala wa Israel katika ubalozi mdogo wa Iran huko Syria.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:26:00
1451628

Onyo la Iran kwa Marekani na Magharibi kuhusu madhara yatakayozipata zikiiunga mkono Israel

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeionya na kuitahadharisha Marekani na nchi za Magharibi juu ya kuuunga mkono kijeshi utawala wa Kizayuni na kufanya chokochoko dhidi ya Iran na kutangaza kwamba, iwapo nchi hizo zitaingilia kati katika kuuunga mkono utawala wa Kizayuni, vituo vyao vyote na maeneo yote ya maslahi yao yatashambuliwa na vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu.