Main Title
17 Aprili 2024
NYT yaagiza waandishi wake: Msitumie misamiati ya 'mauaji ya kimbari', 'uangamizaji wa kizazi' katika vita vya Israel
Taasisi ya uchunguzi wa taarifa za mitandaoni nchini Marekani ya Intercept imefichua kuwa gazeti la New York Times limewaagiza waandishi na maripota wake wa habari wanaoripoti vita vya mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza, wajizuie kutumia misamiati ya "mauaji ya kimbari" na "uangamizaji wa kizazi" na kupeuka kutumia neno “eneo linalokaliwa kwa mabavu” kumaanisha ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel.
17 Aprili 2024
Rais wa Uturuki: Israel imempiku Hitler kwa kuua watoto 14,000 wasio na hatia Ghaza
Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema, Israel tayari imempiku kiongozi wa Wanazi Adolf Hitler kwa kuua zaidi ya watoto 14,000 wasio na hatia katika Ukanda wa Ghaza.
17 Aprili 2024
Grossi asisitiza tena kutokuwepo shughuli za kijeshi za nyuklia nchini Iran
Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA amesisitiza kuwa, hakuna nyaraka zozote zinazothibitisha utengenezaji wa silaha za nyuklia nchini Iran na kuwa, mivutano ya hivi sasa haijavuruga mchakato wa ufuatiliaji wa wakala huo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.
17 Aprili 2024
'Operesheni ya Ahadi ya Ukweli' ya Iran imesambaratisha dhana potofu ya kutoshindwa Israel
Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Brigedia Jenerali Kioumars Haydari amesema operesheni ya kulipiza kisasi ya Iran dhidi ya utawala haramu wa Israel imeondoa zaidi dhana potofu kwamba utawala huo khabithi na muuaji watoto hauwezi kushindwa.
17 Aprili 2024
Amir-Abdollahian: Mgogoro wa Asia Magharibi umesababishwa na mashambulizi ya Israel
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan na kusisitiza kuwa, mgogoro uliopo katika eneo la Asia Magharibi hivi sasa umesababishwa na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni kwenye Ukanda wa Ghaza.
17 Aprili 2024
Ebrahim Raisi: Wazayuni wataelewa maana halisi ya majibu ya Iran
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, iwapo Israel itafanya kosa jingine lolote dhidi ya Iran, basi Wazayuni na waungaji mkono wao wataelewa maana halisi ya majibu ya Jamhuri ya Kiislamu.
17 Aprili 2024
Iran iliwasiliana na nchi za eneo katika kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli dhidi ya Israel
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema: Iran ilikuwa ikiwasiliana na nchi za eneo katika mchakato wa kutoa jibu kwa utawala wa Kizayuni na utekelezaji wa Operesheni ya Ahadi ya Kweli.
17 Aprili 2024
Rais Raisi: Operesheni ya "Ahadi ya Kweli" ilikuwa hatua ya kiwango maalumu na ya kuwatia adabu tu Wazayuni
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Operesheni ya Ahadi ya Kweli ilikuwa hatua ya kiwango maalumu na ya kuutia adabu tu utawala wa Kizayuni na akasisitiza kwamba, endapo utawala huo utafanya uchokozi mdogo kabisa dhidi ya ardhi ya Iran utakabiliwa na jibu kali zaidi na la nguvu kubwa zaidi.
17 Aprili 2024
Kujitetea kwerevu kwa Iran kwa ajili ya Gaza
Hatua ya Iran kujitetea kihalali dhidi ya shambulio la kichokozi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wake nchini Syria, ambayo ilifanyika kwa utaratibu wa hali ya juu na kupitia silaha tofauti za mashambulio, imekuwa na athari na matokeo ya kieneo na kimataifa angalau imepelekea wakaazi wa Gaza kupata usiku mmoja wa amani na utulivu.
17 Aprili 2024
UN: Israel imeua wanawake 10,000 Gaza
Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza tangu utawala haramu wa Israel uanzishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya eneo hilo Oktoba mwaka jana.
17 Aprili 2024
Wapalestina 16 wa Ukanda wa Ghaza wameuawa shahidi kwenye jela za utawala wa Kizayuni
Kamati inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa na walioachiwa huru kutoka kwenye magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa, mateka 16 wakazi wa Ukanda wa Ghaza wameuawa shahidi wakiwa wanashikiliwa kwenye magereza ya utawala huo.
16 Aprili 2024
Bunge la Marekani laionya Washington isijiingize kwenye vita vya kijeshi na Iran
Mkuu wa Kamati ya Kijasusi ya Bunge la Marekani amewaonya viongozi wa Washington kuhusu matokeo mabaya ya kujiingiza katika hatua yoyote ya kijeshi inayoweza kuchukuliwa dhidi ya Iran.
16 Aprili 2024
Ramaphosa: Kama Israel haitodhibitiwa, vita vya Ghaza vinaweza kuenea ukanda mzima
Rais wa Afrika Kusini kwa mara nyingine ameonya kuhusu hatari ya vita vya Ghaza na kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wasio na hatia akisisitiza kuwa kama Israel haitodhibitiwa, basi vita hivyo vinaweza kuenea katika nchi zote za eneo hili.
16 Aprili 2024
Russia yakumbwa na mafuriko; nyumba zaidi ya elfu 15 zazama majini
Maafisa wa Russia wa Idara ya Kukabiliana na Majanga ya Kimaumbile wameeleza kuwa idadi ya nyumba zilizozama kutokana na mafuriko nchini humo imepindukia 15,000.
16 Aprili 2024
Mienendo ya chuki dhidi ya Uislamu yaongezeka nchini Ujerumani
Vyombo vya habari vya Ujerumani, vimenukuu ripoti zilizochapishwa na serikali ya nchi hiyo, na kuripoti kuwa uhalifu dhidi ya Waislamu nchini humo uliongezeka mwaka 2023 ikilinganishwa na miaka ya kabla yake.
16 Aprili 2024
Trump, rais wa kwanza wa zamani Marekani kuhukumiwa katika kesi ya jinai
Kesi ya Donald Trump katika mashtaka ya jinai ilianza jana, Jumatatu, mjini New York na kumfanya kuwa rais wa kwanza wa zamani wa Marekani kufika mbele ya mahakama ya jinai kujibu mashtaka yanayohusiana na kulipa pesa kwa mwigizaji wa filamu za ngono ili kumnyamazisha na kumtaka afiche uhusiano wake wa kingono na mwanamke huyo.
16 Aprili 2024
Kikao cha Baraza la Usalama: Uwanja wa makabiliano kati ya waungaji mkono wa Iran na Wamagharibi wanaounga mkono utawala wa Kizayuni.
Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujadili mashambulizi ya Iran ya kuuadhibu utawala wa Israel kilifanyika Jumapili jioni tarehe 14 Aprili, kikao ambacho kilibadilika na kuwa uwanja wa makabiliano kati ya nchi zinazounga mkono Iran na kambi ya Magharibi waitifaki wa utawala wa Kizayuni.
16 Aprili 2024
Tehran yaitaka UN ilaani shambulio la Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina wajibu wa kulaani shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.
16 Aprili 2024
Abdollahian amwambia Guterres: Hatukuwa na njia nyingine isipokuwa kuiadhibu Israel
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, operesheni ya jeshi la Iran dhidi ya maeneo ya kijeshi ya utawala ghasibu wa Israel imefanyika ndani ya fremu ya kujilinda na kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
16 Aprili 2024
Amir-Abdollahian: Iran haitoruhusu Israel kuhatarisha usalama wa ukanda huu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaamini kwamba usalama na utulivu wa nchi za eneo hili zima ni muhimu sana kwake, bali ni sawa kabisa na usalama wake yenyewe na haitoruhusu utawala wa Kizayuni kuhatarisha usalama wa eneo hili kwa chokochoko zake.