Main Title
4 Aprili 2024
Baraza la Haki za Kibinadamu la UN lapanga vikwazo vya silaha dhidi ya Israel
Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) litachunguza rasimu ya azimio la kuweka vikwazo vya silaha dhidi ya utawala haramu wa Israel.
4 Aprili 2024
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Israel itazabwa kibao usoni kwa shambulio lake dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema utawala wa Kizayuni wa Israel utazabwa kibao usoni kutokana na shambulio lake dhidi ya majengo ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, mapema wiki hii.
4 Aprili 2024
Shambulio la kigaidi kusini mashariki mwa Iran
Alireza Marhamati, Naibu Gavana anayesimamia masuala ya usalama na utekelezaji sheria katika mkoa wa Sistan na Baluchistan, kusini mashariki mwa Iran, ametangaza kutokea shambulio la kigaidi kwenye makao makuu mawili ya kijeshi katika miji ya Rask na Chabahar mkoni humo.
4 Aprili 2024
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akosoa upuuzaji wa Umoja wa Ulaya kuhusu ugaidi wa Israel
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa misimamo ya undumakuwili ya Umoja wa Ulaya na upuuzaji wake kuhusiana na jinai na vitendo vya kigaidi vya utawala ghasibu wa Israel.
4 Aprili 2024
Raisi: Siku ya Kimataifa ya Quds ni nembo ya kuwatimua Wazayuni katika ardhi za Palestina
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameitaja Siku ya Kimataifa ya Quds kuwa ni ukumbusho wa kukaribia ushindi wa mwisho wa wananchi wa Palestina dhidi ya wavamizi wa Kizayuni na ishara ya mshikamano, umoja na uelewa wa Umma wa Kiislamu katika kutatua kadhia ya Palestina na kuwafukuza wavamizi kutoka katika ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
4 Aprili 2024
SEPAH: Magaidi 15 wameshaangamizwa hadi hivi sasa kusini mashariki mwa Iran
Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) amesema kuwa, hadi hivi sasa magaidi 15 wameshaangamizwa katika operesheni za kuzima mashambulizi matatu ya kigaidi yaliyofanywa na magaidi hao kusini mashariki mwa Iran.
4 Aprili 2024
Kufungwa kituo cha televisheni cha Al Jazeera Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel)
Radimali ya jinai za Israel dhidi ya watu wa Gaza katika vyombo vya habari vya dunia na wimbi la upinzani na lawama za kimataifa kuhusu jinai hizo zimeufanya utawala wa Kizayuni kufunga mara moja kituo cha Televisheni ya Al-Jazeera katika Ukanda wa Gaza kutokana na jinsi inavyoakisi habari za mauaji ya kimbari ya utawala huo katika vita hivyo.
4 Aprili 2024
Hassan Nasrullah: Kimbunga cha al-Aqsa kimemsukuma adui Mzayuni kwenye ukingo wa shimo la mauti
Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa, Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu ni tofauti na miaka iliyopita, na kwamba operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa imemweka adui Mzayuni kwenye ukingo wa shimo la mauti.
4 Aprili 2024
Siku ya Quds na kufichuka sura halisi ya utawala wa mauaji ya kimbari wa Israel
Siku ya Quds mwaka huu 2024 imewadia huku utawala wa Kizayuni wa Israel ukiwa umekwama kwenye kinamasi cha Gaza licha ya mauaji ya kimbari unayoendelea kufanya katika eneo hilo la Palestina.
4 Aprili 2024
Yemen: Siku ya Kimataifa ya Quds imeibakisha hai kadhia ya Palestina
Katibu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen amesema kuwa, Siku ya Kimataifa ya Quds imeyabakisha hai mapambano ya ukombozi wa Palestina.
3 Aprili 2024
Muqawama wa Iraq: Tumeshambulia Haifa kulipiza kisasi cha jinai za Wazayuni Ghaza
Makukndi ya Muqawa wa Kiislamu ya Iraq yametangaza kuwa yameshambulia kambi ya jeshi la anga ya Tel Nof ya utawala wa Kizayuni kwenye mji wa Haifa ili kulipiza kisasi cha jinai zinazofanywa na Israel katika Ukanda wa Ghaza.
3 Aprili 2024
Korea Kaskazini yafanya jaribio la kombora lenye uwezo wa kufika kambi za Marekani bahari ya Pasifiki
Korea Kaskazini imefanya jaribio la kombora la masafa ya kati (IRBM) kutoka pwani yake ya mashariki, kuonyesha dhamira yake ya kuendeleza teknolojia ya makombora yenye uwezo wa kufikia kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Magharibi mwa Bahari ya Pasifiki.
3 Aprili 2024
Baraza la Usalama laitisha kikao cha dharura kuhusu shambulio la Israel kwenye ubalozi wa Iran
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitisha kikao cha dharura cha kujadili shambulizi la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria kikao ambacho kimeshuhudia kulaaniwa vikali Israel kwa shambulio lake hilo la kigaidii.
3 Aprili 2024
Mtaalamu wa UN: Israel 'iliwaua kimakusudi' wafanyakazi wa misaada Gaza
Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu anasema jeshi la Israel "limewaua kimakusudi" wafanyakazi wa misaada wa Kundi la Misaada la World Central Kitchen, WCK katika Ukanda wa Gaza.
3 Aprili 2024
Dunia yaendelea kulaani shambulio la kigaidi la Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria
Dunia imeendelea kulaani vikali sambulio la utawala haramu wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria huku Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya mkutano wa dharura kuhusu mgomo huo mbaya.
3 Aprili 2024
Salwan Momika, Muiraki aliyiivunjia heshima Qur'an mara kadhaa, aripotiwa kufariki akiwa Norway
Mkimbizi wa Iraq, Salwan Momika, ambaye alivunjia heshima nakala za Qur'ani Tukufu mara kadhaa mwaka jana, ameripotiwa kupatikana amefariki nchini Norway.
3 Aprili 2024
Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la Israel lililolenga ubalozi mdogo wa Iran Damascus
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria na kuonya kwamba mahesabu yoyote ya kimakosa yanaweza kusababisha mapigano yenye wigo mpana zaidi katika eneo hili tete na lisilo na uthabiti na kusababisha matokeo haribifu kwa raia.
3 Aprili 2024
Rais Ebrahim Raisi: Israel iko kwenye sakaratul mauti, inakata roho
Rais Ebrahim Raisi amesema kuwa, shambulio la juzi Jumatatu la utawala wa Kizayuni kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria ni ushahidi kuwa Israel iko kwenye sakaratul mauti na inakata roho hivi sasa.
3 Aprili 2024
Baraza la Usalama UN lalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran, Damascus
Wawakilishi waliohudhuria kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran huko Damascus (mji mkuu wa Syria) wamelaani kitendo hicho cha kinyama cha Wazayuni.
3 Aprili 2024
Mazishi ya washauri wa kijeshi wa Iran waliouawa katika hujuma ya Israel jijini Damascus
Maelfu ya watu wameshiriki katika msafara wa mazishi ya washauri wa kijeshi wa Iran, waliouawa shahidi katika shambulizi la makombora la utawala haramu wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria Damascus.