Main Title
1 Aprili 2024
Corbyn: Kuendelea Uingereza kuipa Israel silaha kunaifanya mshirika katika mauaji ya kimbari Gaza
Kiongozi wa zamani wa chama cha Labour nchini Uingereza amezikosoa nchi za Magharibi - hasa Marekani na Uingereza - zinazoendelea kuipatia Israel silaha za kuwaua Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, na kusema kuwa nchi hizo zinakiuka sheria za kimataifa.
1 Aprili 2024
Msaada mpya wa silaha wa Marekani kwa Israel wa kufanyia mauaji makubwa zaidi ya kimbari ya Wapalestina
Sambamba na juhudi zinazofanywa kimataifa kwa lengo la kusimamisha mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni; na mashinikizo yanayotolewa kwa utawala huo uhakikishe unaruhusu kuingizwa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza, duru za habari za Marekani zimeripoti kuwa serikali ya Washington imeidhinisha kupatiwa Israel shehena mpya ya silaha za kisasa ili kuweza kuua idadi kubwa zaidi ya Wapalestina.
1 Aprili 2024
Kan'ani: Wazayuni wanafanya jinai Gaza mbele ya macho ya walimwengu
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema jinai za kutisha za kivita zinazofanywa na Wazayuni eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina zinaendelea mbele ya macho ya walimwengu.
1 Aprili 2024
Rais Raisi ahimiza kutekelezwa kivitendo mafundisho ya Qur'ani Tukufu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuzingatia mafundisho wa Qur'ani Tukufu katika nyuga zote ni jambo la dharura kwa ajili ya mafanikio ya wanadamu ya duniani na Akhera.
1 Aprili 2024
Iran na Misri zataka kufanyike juhudi madhubuti za kuizuia Israel isiuvamie mji wa Rafah
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Misri wametoa mwito wa kuchukuliwa hatua za maana kimataifa ili kuzuia mashambulizi ya kivamizi ya utawala wa Kizayuni katika mji wa Rafah wa kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
1 Aprili 2024
Raisi: Leo hii utawala wa Kizayuni unatumia vibaya mizozo baina ya Waislamu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, lau kama nchi za Waislamu zingeacha kuitegemea Marekani na madola ya kibeberu na badala yake kuishi kwa mujibu wa mafundisho ya Qur'ani Tukufu, basi leo hii wananchi wa Ghaza na Wapaletina wasingtelikuwa wananyanyaswa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
1 Aprili 2024
Makundi ya ukombozi ya Palestina: Hatutaruhusu jeshi lolote la kimataifa au la Kiarabu kuingia Gaza
Makundi ya ukombozi ya Wapalestina yametangaza kuwa jeshi lolote la kimataifa au la Kiarabu litakaloingia katika Ukanda wa Gaza halikubaliki na litatambuliwa kuwa ni jeshi vamizi.
1 Aprili 2024
Kwa mara nyingine, Hizbullah yazitwanga kwa mizinga kambi za kijeshi za Israel
Wanamapambano wa Kiislamu wa nchini Lebanon kwa mara nyingine wamezitwanga kwa mizinga kambi za kijeshi za utawala wa Kizayuni wa Israel kujibu jinai na mauaji ya umati yanayofanywa na Wazayuni huko Ghaza, Palestina.
1 Aprili 2024
Hamas: Kuanzisha maeneo ya kunyonga watu huko Gaza ni uhalifu wa kikatili wa kivita
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kwamba, kilichofichuliwa na vyombo vya habari vya Israel kuhusu hatua ya jeshi la utawala huo ya kuanzishwa "maeneo ya kunyonga watu" katika Ukanda wa Gaza, ambapo mtu yeyote anayetembea katika maeneo hayo anauawa, ni jinai ya kikatili ya kivita.
31 Machi 2024
Zelensky aonya: Bila msaada wa kijeshi wa Marekani, Ukraine italazimika kurudi nyuma
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema iwapo nchi yake haitopatiwa msaada wa kijeshi ulioahidiwa na Marekani ambao kwa sasa umezuiwa kutokana na mizozo iliyomo ndani ya Kongresi ya nchi hiyo italazimika kurudi nyuma katika vita na Russia hatua kwa hatua.
31 Machi 2024
Watu masikini na wakimbizi wafukuzwa Paris kabla ya Olimpiki
Takriban wakimbizi 500 na watu masikini wasio na makazi wamehamishwa kwa nguvu kutoka mji mkuu wa Ufaransa na kupelekwa maaeneo ya vijijini na miji midogo nchini humo huku Paris ikijiitayarisha kuandaa Olimpiki ya Majira ya joto ya 2024 mnamo Julai na Agosti.
31 Machi 2024
Wananchi wa Uturuki washiriki katika uchaguzi muhimu wa serikali za mitaa
Vituo vya kupigia kura nchini Uturuki vilifunguliwa mapema leo asubuhi kuruhusu wananchi kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotajwa kuwa ni mtihani muhimu kwa Rais Recep Tayyip Erdogan wa nchi hiyo. Weledi wa mambo wanasema kuwa Rais wa Uturuki anakabiliwa na kibarua kigumu ili kuyarejesha maeneo muhimu ya mijini aliyoshindwa na upinzani miaka mitano iliyopita.
31 Machi 2024
Jeshi la Iran laapa kulinda usalama na uhuru wa nchi
Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimetangaza azma ya kuendeleza juhudi za kiwango cha juu ili kufikia malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu na kulinda usalama na uhuru wa taifa.
31 Machi 2024
Jihad Islami: Wapalestina hawangeweza kusimama dhidi ya Israel bila ya kuungwa mkono na Iran
Kiongozi mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina ametangaza bayana kuwa watu wa Palestina hawangeweza kusimama dhidi ya utawala haramu wa Israel kama kusingekuwa na uungaji mkono kamili wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
31 Machi 2024
Maadhimisho ya YaumuLlah, Siku ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
YaumuLlah ya tarehe 12 Farvardin mwaka 1358 Hijria Shamsia (iliyosadifiana na Aprili Mosi, 1979), yenye maana ya Siku ya Mwenyezi Mungu, si siku rasmi tu katika kalenda ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, bali ni siku kubwa pia kwa wanyonge duniani na kwa harakati za ukombozi pamoja na mataifa yanayopambana na dhulma, uistikbari na ukoloni.
31 Machi 2024
Mkurugenzi Mkuu wa IAEA: Iran haina silaha za nyuklia
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) ametenganisha baina ya kategoria ya kurutubisha madini ya urani na mchakato wa uundaji silaha za nyuklia na kutangaza kuwa Iran haitengenezi silaha za nyuklia licha ya kuwa na akiba ya urani iliyorutubishwa.
31 Machi 2024
Kwa mnasaba wa "Siku ya Ardhi", HAMAS yautolea wito Umma wa Kiislamu kuikomboa Palestina
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa taarifa maalumu kwa mnasaba wa "Siku ya Ardhi" ikisisitiza kuwa kuikomboa ardhi ya Palestina na matakatifu yake ni jukumu la Umma wote wa Kiislamu.
31 Machi 2024
61% ya Waisraeli hawaamini kama vita vya Ghaza vitamalizika kwa kusambaratishwa HAMAS
Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa Palestina inayokaliwa kwa mabavu iliyopandikizwa jina bandia la Israel yanaonyesha kuwa asilimia 61 ya Wazayuni hawaamini kama vita vya Ghaza vitamalizika kwa "kusambaratishwa harakati ya Hamas".
31 Machi 2024
Licha ya kuikosoa Israel hadharani, Biden ameidhinisha kwa siri silaha mpya za kuwaulia Wapalestina
Rais Joe Biden wa Marekani hivi karibuni ameidhinisha kwa siri kupatiwa utawala wa Kizayuni wa Israel silaha mpya za kivita zenye gharama ya mabilioni ya dola zikiwemo aina za kisasa za mabomu na ndege za kivita.
31 Machi 2024
Wapiganaji wa Muqawama Iraq washambulia kituo 'muhimu' cha kijeshi cha Israel
Kundi la Wapiganaji wa Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) Iraq limetangaza kushambulia kituo "muhimu" cha kijeshi cha utawala wa Israel kilichoko kaskazini mwa maeneo yanayokaliwa kwa mabavu katika kuendelea kuwaunga mkono Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, ambao wanastahimili vita vya mauaji ya halaiki ya Israel.