Main Title
24 Machi 2024
Bajeti ya muda ya US yaidhinisha msaada wa kijeshi kwa Israel, yazuia ufadhili kwa UNRWA
Bunge la Marekani limepitisha pendekezo la bajeti ya muda ambayo imeidhinisha msaada mpya wa kijeshi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusitisha ufadhili kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) hadi Machi 2025.
24 Machi 2024
Idadi ya waliofariki katika shambulio la Moscow yapindukia 130, ISIS-K yadai kuhusika
Vyombo vya sheria na usalama vya Russia vimesema idadi ya watu waliouawa katika shambulio la kigaidi la siku ya Ijumaa kwenye ukumbi wa tamasha la muziki wa Crocus City Hall nje kidogo ya jiji la Moscow imepindukia watu 130.
24 Machi 2024
Ugaidi, changamoto ya pamoja ya kieneo na wajibu wa kuwa macho
Katika kipindi cha chini ya wiki moja kumetokea miripuko miwili na shambulio kubwa la kigaidi na la umwagaji damu huko Kandahar Afghanistan na kwenye viunga vya mji mkuu wa Russia, Moscow.
24 Machi 2024
Iran: Tuko pamoja na Russia baada ya shambulio la kigaidi la Moscow
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mwito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua kali za kuwaadhibu magaidi waliohusika na shambulio la kigaidi kwenye jumba moja la starehe katika viunga vya Moscow, mji mkuu wa Russia.
24 Machi 2024
Ndege ya kivita isiyo na rubani ya Iran ijulikanayo kama 'Gaza' yavuma kimataifa
Iran imeanza kusambaza bidhaa zake za kijeshi na ulinzi kimataifa, huku gazeti moja la Marekani likisema kuwa sekta ya ulinzi ya Iran imeingia rasmi katika soko la kimataifa kwa kushiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Silaha ya Doha nchini Qatar ambapo imeonyesha ndege ya kisasa ya kivita isiyo na rubani iliyopewa jina la 'Gaza'.
24 Machi 2024
Wapalestina 72 wameuawa shahidi Ukanda wa Gaza katika masaa 24 yaliyopita
Wizara ya Afya ya Palestina jana ilitangaza kuwa Wapalestina wasiopungua 72 wameuawa shahidi na wengine 114 kujeruhiwa katika masaa 24 yaliyopita kufuatia mauaji ya kimbari yanayondelea kufanywa na Israel dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
24 Machi 2024
Muqawama wa Iraq: Tumeshambulia kwa droni makao makuu ya wizara ya masuala ya kijeshi ya Israel
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Iraq imetangaza kuwa imeshambulia makao makuu ya wizara ya masuala ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kutumia ndege isiyo na rubani mapema leo Jumapili.
24 Machi 2024
Katibu Mkuu wa UN alaani Israel kuzuia malori ya misaada yasiingie Ghaza, 7,000 yamepanga safu Misri
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani kuzuiwa kwa malori ya misaada yaliyoko katika upande wa Misri wa mpaka na Ukanda wa Ghaza, akiielezea hatua hiyo kuwa inasababisha "ghadhabu ya kimaadili."
24 Machi 2024
Jeshi la Anga la Syria latungua makombora ya Israel karibu na Damascus
Vikosi vya ulinzi wa anga vya Syria vimefanikiwa kutungua makombora mengi yaliyovurumishwa na jeshi la Israel karibu na mji mkuu wa nchi hiyo Damascus.
24 Machi 2024
Hamas yalaani kimya cha dunia kuhusu uvamizi wa Israel kwenye hospitali ya al-Shifa ya Gaza
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (muqawama) ya Palestina, Hamas, imelaani vikali jamii ya kimataifa kwa "ukimya wake wa aibu" juu ya uvamizi wa jeshi la utawala wa Israel dhidi ya hospitali ya al-Shifa ya Gaza ambako maelfu ya Wapalestina waliokimbia makwao wanapata hifadhi.
23 Machi 2024
Majeshi ya India, Msumbiji, Tanzania katika mazoezi ya pamoja Bahari ya Hindi
Mazoezi ya pamoja kati ya majeshi ya majini ya Msumbiji, Tanzania na India yalianza Alhamisi katika pwani ya Afrika Mashariki katika Bahari ya Hindi.
23 Machi 2024
Russia, China zalipigia turufu azimio la US kuhusu Gaza lenye kuunga mkono Israel
Azimio la Marekani la kutaka kusitishwa kwa mapigano huko Gaza linalohusishwa na mpango wa wafungwa na mateka limepingwa na Russia na China katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kutokana na msimamo wake wa kuiunga mkono Israel.
23 Machi 2024
Wito wa maseneta 19 wa Marekani wa kuundwa taifa huru la Palestina
Maseneta 19 wa chama cha Democratic wametoa wito wa kuundwa taifa huru la Palestina katika barua yao iliyotumwa kwa Rais wa Marekani, Joe Biden.
23 Machi 2024
Kula mweleka njama za Marekani za kuunga mkono mauaji ya kimbari ya Israel kwenye UN
Azimio lililopendekezwa na Marekani la kuunga mkono mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ghaza limegonga ukuta baada ya kupigiwa kura ya veto na Russia na China ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
23 Machi 2024
Russia: Umoja wa Ulaya unahusika na mashambulizi ya kigaidi ya Ukraine dhidi ya Warusi
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, Maria Zakharova, amesema kuwa mipango ya Umoja wa Ulaya ya kutenga euro bilioni 50 kama msaada wa kifedha na kiuchumi kwa ajili ya Ukraine "haitauokoa utawala wa Kinazi huko Kiev."
23 Machi 2024
The Washington Post: Kauli za Kushner kuhusu Gaza ni dalili ya sera ya baadaye ya Trump
Gazeti la Marekani la The Washington Post limeripoti kuwa muhula wa pili wa Donald Trump, iwapo atashinda uchaguzi ujao wa rais nchini Marekani, "huenda ukamaanisha uungaji mkono mkubwa zaidi wa Washington kwa watawala wa sasa wa Israel wanaotaka kuwafukuza Wapalestina kutoka Gaza na kulikalia tena kwa mabavu eneo hilo."
23 Machi 2024
Washukiwa wanne wakuu wa shambulizi la kigaidi la Moscow wakamatwa, idadi ya wahanga imefika 93
Ikulu ya Rais wa Russia, Kremlin, imetangaza habari ya kukamatwa watu 11, wakiwemo wanne waliohusika moja kwa moja katika shambulio lililolenga jumba la tamasha mjini Moscow jana Ijumaa, na kuua makumi ya watu.
23 Machi 2024
Iran yalaani shambulizi la kigaidi lililoua makumi ya watu nchini Russia
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali shambulio la kigaidi lililoua na kujeruhi makumi ya watu katika mji mkuu wa Russia, Moscow.
23 Machi 2024
Msemaji wa AEOI: Iran inahitaji vituo 20 vya nyuklia
Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema Jamhuri ya Kiislamu inapasa kuwa na vituo kati ya 15 na 20 vya nyuklia ili kujidhaminia mahitaji yake ya nishati.
23 Machi 2024
"Mauaji ya kimbara Gaza yamefichua dhati na unafiki wa Wamagharibi"
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mauaji ya kimbari yanayoshuhudiwa katika Ukanda wa Gaza yameweka bayana kuwa nchi za Magharibi zinatumia suala la 'haki za binadamu' kama wenzo wa kisiasa tu.