Main Title

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:06:50
1452778

UNICEF: Utawala haramu wa Israel umeua zaidi ya watoto elfu 14,000 wa Gaza

Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) amesema kuwa zaidi ya watoto elfu 14,000 wa Kipalestina wameuawa hadi sasa katika mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:06:18
1452777

UN: Moto wa vita vya Sudan unachochewa na silaha zitokazo nje za wakiukaji wa vikwazo

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kisiasa na Ujenzi wa Amani, Rosemary Anne DiCarlo ameliambia Baraza la Usalama kwamba vita nchini Sudan vimesababisha "hali mbaya ya kiwango cha kipekee" inayochochewa na silaha kutoka kwa waungaji mkono wa kigeni ambao wanaendelea kukiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:05:43
1452776

Mvua kali za mafuriko zaua watu wasiopungua 168 Pakistan na Afghanistan

Watu wasiopungua 168 wamepoteza maisha katika matukio yaliyosababishwa na mvua, baada ya mvua kali na mafuriko kuikumba Pakistan na nchi jirani ya Afghanistan.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:04:55
1452775

Marekani; kizuizi kikuu kwa Palestina kuwa mwanachama kamili katika Umoja wa Mataifa

Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu wa Israel kwa mara nyingine imetumia kura ya turufu (Veto) na kuzuia kupasishwa uanachama kamili wa Palestina ndani ya Umoja wa Mataifa.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:04:02
1452774

Iran na Uturuki zatilia mkazo wajibu wa kukomeshwa haraka mashambulizi huko Ghaza

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki wamehimiza na kutilia mkazo udharura wa kukomeshwa mara moja mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:03:42
1452773

Iran yalaani veto ya Marekani dhidi ya uanachama kamili wa Palestina UN

Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kura ya turufu ya Marekani dhidi ya rasimu ya azimio iliyotaka Palestina ipewe uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:03:18
1452772

Tehran: Vyombo vya habari vya Magharibi vinajaribu kugeuza kushindwa Israel kuwa ushindi

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian amesema kuwa quadcopter tatu za kigeni (videge vigogo visivyo na rubani) zilizotunguliwa na walinzi wa anga wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mji wa kati wa Isfahan hazikusababisha uharibifu wala majeruhi yoyote ndani ya nchi.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:02:41
1452770

Mashtaka ya Saudia dhidi ya Imarati, hatua ya aina yake katika uhusiano wa nchi mbili

Saudi Arabia imewasilisha malalamiko dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutokana na mzozo wa mpaka.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:02:08
1452769

OIC yalaani hatua ya Marekani kuzuia azma ya Palestina kuwa mwanachama kamili wa UN

Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani hatua ya Marekani ya kuzuia ombi la Palestina la kutaka uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa, huku Israel ikiendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza kwa msaada wa baadhi ya nchi za Magharibi hususan Marekani.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:01:36
1452768

Harakati ya Kiislamu Iraqi yashambulia mji wa Eilat

Harakati ya Kiislamu ya Iraq imetangaza kuwa imeshambulia maeneo muhimu katika mji wa Eilat, ulioko kusini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:00:53
1452767

Hizbullah ya Lebanon yafanya mashambulio sita dhidi ya ngome na vituo vya kijeshi vya Israel

Muqawama wa Kiislamu wa Lebanon umefanya mashambulio sita dhidi ya ngome na vituo vya kijeshi vya utawala wa Kizayuni wa Israel.

source :
Jumamosi

20 Aprili 2024

20:00:18
1452766

Wapalestina wengine 37 wauawa shahidi kutokana na Israel kuendeleza mashambulizi Ghaza

Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa, Wapalestina wengine 37 wameuawa shahidi na 68 wajeruhiwa katika muda wa saa 24 zilizopita, wakati jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel lilipoendeleza mashambulizi yake kwenye Ukanda wa Ghaza uliozingirwa.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:40:52
1452492

Galloway akosoa sera za kinafiki za London kuhusu Iran

Mwanasiasa maarufu wa Uingereza amejibu mashambulizi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akihoji: "Kwa nini hukulaani vikali shambulio la Israel kwenye sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria."

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:40:19
1452491

Marekani yalipigia kura ya veto azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili wa Umoja wa Mataifa

Marekani, ambayo ni muungaji mkono mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, imeendeleza sera yake ya kudhoofisha kupatikana haki za Wapalestina kwa kutumia vibaya haki yake ya kura ya turufu na kukwamisha azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:39:23
1452490

Kukiri Pentagon kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran katika kuujibu utawala wa Kizayuni

Patrick Ryder Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri juu ya nguvu za kijeshi za Iran katika kutoa jibu la kijeshi kwa utawala wa Israel.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:38:28
1452488

Gharibabadi: Nchi za Magharibi ziache sera za kinafiki na ubaguzi kuhusiana na ugaidi

Katibu wa Baraza Kuu la Haki za Kibinadamu la Iran amesema kuwa, Marekani na nchi za Magharibi kwa ujumla zinapaswa kuachana na siasa zao za kindumakuwili na ubaguzi kuhusiana na ugaidi.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:37:20
1452487

Ustawi wa biashara ya nje yenye mlingano chini ya uongozi wa serikali ya 13 ya Iran

Kituo cha Takwimu cha Kamisheni ya Ulaya kimetangaza kuwa Katika mwezi wa kwanza wa mwaka huu wa 2024, uagizaji wa bidhaa wa Ugiriki kutoka Iran uliongezeka mara 3 na Uholanzi mara 2, nayo mauzo ya Uhispania kwa Iran yakaongezeka kwa asilimia 62 na Italia kwa asilimia 13.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:36:34
1452486

Iran yalaani madai ya viongozi wa Ulaya na mawaziri wa fedha wa G7 dhidi yake

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekanusha madai ya viongozi wa nchi za Ulaya na mawaziri wa fedha wa kundi la G7 pamoja na matamshi ya baadhi ya wakuu wa Marekani na kusema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitosita hata mara moja kujihami na kulinda maslahi yake ya kitaifa.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:35:48
1452485

Vyombo vya habari: Iran imetungua ndege tatu zisizo na rubani katika mji wa Esfahan

Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, mfumo wa ulinzi wa anga wa Iran umetungua ndege tatu ndogo zisizo na rubani katika mkoa wa Esfahan ulioko katikati mwa nchi saa kadha baada ya vyombo vya habari vya Marekani kuwanukuu maafisa waandamizi wa nchi hiyo wakidai kwamba makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamepiga eneo la Iran.

source :
Ijumaa

19 Aprili 2024

18:35:25
1452484

Sheikh Akbari: Operesheni ya Ahadi ya Kweli ni Kimbunga cha al Aqsa cha Iran

Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa Tehran amesema kuwa, operesheni iliyofanywa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kulipiza kisasi jinai za Israel ilikuwa ni kimbunga cha al Aqsa cha Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni na ni operesheni ya kujivunia na kujifakharisha nayo.