Main Title
20 Aprili 2024
UNICEF: Utawala haramu wa Israel umeua zaidi ya watoto elfu 14,000 wa Gaza
Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) amesema kuwa zaidi ya watoto elfu 14,000 wa Kipalestina wameuawa hadi sasa katika mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.
20 Aprili 2024
UN: Moto wa vita vya Sudan unachochewa na silaha zitokazo nje za wakiukaji wa vikwazo
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kisiasa na Ujenzi wa Amani, Rosemary Anne DiCarlo ameliambia Baraza la Usalama kwamba vita nchini Sudan vimesababisha "hali mbaya ya kiwango cha kipekee" inayochochewa na silaha kutoka kwa waungaji mkono wa kigeni ambao wanaendelea kukiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa
20 Aprili 2024
Mvua kali za mafuriko zaua watu wasiopungua 168 Pakistan na Afghanistan
Watu wasiopungua 168 wamepoteza maisha katika matukio yaliyosababishwa na mvua, baada ya mvua kali na mafuriko kuikumba Pakistan na nchi jirani ya Afghanistan.
20 Aprili 2024
Marekani; kizuizi kikuu kwa Palestina kuwa mwanachama kamili katika Umoja wa Mataifa
Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu wa Israel kwa mara nyingine imetumia kura ya turufu (Veto) na kuzuia kupasishwa uanachama kamili wa Palestina ndani ya Umoja wa Mataifa.
20 Aprili 2024
Iran na Uturuki zatilia mkazo wajibu wa kukomeshwa haraka mashambulizi huko Ghaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki wamehimiza na kutilia mkazo udharura wa kukomeshwa mara moja mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza.
20 Aprili 2024
Iran yalaani veto ya Marekani dhidi ya uanachama kamili wa Palestina UN
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kura ya turufu ya Marekani dhidi ya rasimu ya azimio iliyotaka Palestina ipewe uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
20 Aprili 2024
Tehran: Vyombo vya habari vya Magharibi vinajaribu kugeuza kushindwa Israel kuwa ushindi
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian amesema kuwa quadcopter tatu za kigeni (videge vigogo visivyo na rubani) zilizotunguliwa na walinzi wa anga wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mji wa kati wa Isfahan hazikusababisha uharibifu wala majeruhi yoyote ndani ya nchi.
20 Aprili 2024
Mashtaka ya Saudia dhidi ya Imarati, hatua ya aina yake katika uhusiano wa nchi mbili
Saudi Arabia imewasilisha malalamiko dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutokana na mzozo wa mpaka.
20 Aprili 2024
OIC yalaani hatua ya Marekani kuzuia azma ya Palestina kuwa mwanachama kamili wa UN
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani hatua ya Marekani ya kuzuia ombi la Palestina la kutaka uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa, huku Israel ikiendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza kwa msaada wa baadhi ya nchi za Magharibi hususan Marekani.
20 Aprili 2024
Harakati ya Kiislamu Iraqi yashambulia mji wa Eilat
Harakati ya Kiislamu ya Iraq imetangaza kuwa imeshambulia maeneo muhimu katika mji wa Eilat, ulioko kusini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
20 Aprili 2024
Hizbullah ya Lebanon yafanya mashambulio sita dhidi ya ngome na vituo vya kijeshi vya Israel
Muqawama wa Kiislamu wa Lebanon umefanya mashambulio sita dhidi ya ngome na vituo vya kijeshi vya utawala wa Kizayuni wa Israel.
20 Aprili 2024
Wapalestina wengine 37 wauawa shahidi kutokana na Israel kuendeleza mashambulizi Ghaza
Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa, Wapalestina wengine 37 wameuawa shahidi na 68 wajeruhiwa katika muda wa saa 24 zilizopita, wakati jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel lilipoendeleza mashambulizi yake kwenye Ukanda wa Ghaza uliozingirwa.
19 Aprili 2024
Galloway akosoa sera za kinafiki za London kuhusu Iran
Mwanasiasa maarufu wa Uingereza amejibu mashambulizi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akihoji: "Kwa nini hukulaani vikali shambulio la Israel kwenye sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria."
19 Aprili 2024
Marekani yalipigia kura ya veto azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili wa Umoja wa Mataifa
Marekani, ambayo ni muungaji mkono mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, imeendeleza sera yake ya kudhoofisha kupatikana haki za Wapalestina kwa kutumia vibaya haki yake ya kura ya turufu na kukwamisha azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
19 Aprili 2024
Kukiri Pentagon kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran katika kuujibu utawala wa Kizayuni
Patrick Ryder Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri juu ya nguvu za kijeshi za Iran katika kutoa jibu la kijeshi kwa utawala wa Israel.
19 Aprili 2024
Gharibabadi: Nchi za Magharibi ziache sera za kinafiki na ubaguzi kuhusiana na ugaidi
Katibu wa Baraza Kuu la Haki za Kibinadamu la Iran amesema kuwa, Marekani na nchi za Magharibi kwa ujumla zinapaswa kuachana na siasa zao za kindumakuwili na ubaguzi kuhusiana na ugaidi.
19 Aprili 2024
Ustawi wa biashara ya nje yenye mlingano chini ya uongozi wa serikali ya 13 ya Iran
Kituo cha Takwimu cha Kamisheni ya Ulaya kimetangaza kuwa Katika mwezi wa kwanza wa mwaka huu wa 2024, uagizaji wa bidhaa wa Ugiriki kutoka Iran uliongezeka mara 3 na Uholanzi mara 2, nayo mauzo ya Uhispania kwa Iran yakaongezeka kwa asilimia 62 na Italia kwa asilimia 13.
19 Aprili 2024
Iran yalaani madai ya viongozi wa Ulaya na mawaziri wa fedha wa G7 dhidi yake
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekanusha madai ya viongozi wa nchi za Ulaya na mawaziri wa fedha wa kundi la G7 pamoja na matamshi ya baadhi ya wakuu wa Marekani na kusema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitosita hata mara moja kujihami na kulinda maslahi yake ya kitaifa.
19 Aprili 2024
Vyombo vya habari: Iran imetungua ndege tatu zisizo na rubani katika mji wa Esfahan
Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, mfumo wa ulinzi wa anga wa Iran umetungua ndege tatu ndogo zisizo na rubani katika mkoa wa Esfahan ulioko katikati mwa nchi saa kadha baada ya vyombo vya habari vya Marekani kuwanukuu maafisa waandamizi wa nchi hiyo wakidai kwamba makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamepiga eneo la Iran.
19 Aprili 2024
Sheikh Akbari: Operesheni ya Ahadi ya Kweli ni Kimbunga cha al Aqsa cha Iran
Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa Tehran amesema kuwa, operesheni iliyofanywa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kulipiza kisasi jinai za Israel ilikuwa ni kimbunga cha al Aqsa cha Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni na ni operesheni ya kujivunia na kujifakharisha nayo.