Main Title
20 Machi 2024
Rais wa Russia awapongeza Wairani kwa mnasaba wa Ramadhani na Mwaka Mpya
Rais wa Russia Vladimir Putin amelipongeza taifa la Iran kwa kwa minasaba miwili ya mwezi mtukfuu wa Ramadhani na kuwadiawaka mpya wa Kiirani wa Hijria Shamsiya ambao umeanza leo.
20 Machi 2024
Qatar: Tuna matumaini ya kupatikana usitishaji vita Ukanda wa Ghaza
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar amesema kuwa, kumeshuhudiwa maendeleo mazuri kwenye mazungumzo ya kusimamisha vita na ana matumaini mazungumzo hayo yatazaa matunda mazuri.
20 Machi 2024
Mshauri wa zamani wa White House ametaka Wapalestina wahamishwe Ghaza na kupelekwa jangwani
Mshauri wa zamani wa Ikulu ya Marekani (White House) Jared Kushner amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel inapasa uwaondoe Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na kuwahamishia kwenye jangwa la Negev kusini mwa ardhi zilizopachikwa jina bandia la Israel.
19 Machi 2024
Forensic Architecture yaishutumu Israel kwa "kufanya mauaji ya kimbari" huko Gaza
Shirika la Forensic Architecture limesema kuwa Israel inatekeleza "ugaidi wa kijiografia" ili kupanua operesheni ya kuwahamisha wakazi wa Ukanda wa Gaza kwa mabavu, likibainisha kuwa hatua hizi zinaonyesha mwelekeo wa kufanya uhalifu wa mauaji ya kimbari.
19 Machi 2024
BBC kuchunguza matumizi ya mitandao ya kijamii ya wafanyakazi wake baada ya ripota 'kuunga mkono' ujumbe dhidi ya Israel
Shirika la Utangazaji la Serikali ya Uingereza, BBC litachunguza matumizi ya mitandao ya kijamii baada ya mwandishi wake "kuunga mkono" jumbe zinazoilaumu Israel kama utawala wa "mauaji ya kimbari" na kuunga mkono haki ya Wapalestina kupinga uvamizi wa Israel.
19 Machi 2024
WHO: Oparesheni za kijeshi dhidi ya Rafah zitasababisha maafa halisi
Msemaji wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ameitahadharisha Israel kuhusu oparesheni yoyote ya kijeshi katika mji wa Rafah na kusema, misaada ambayo imewasili Ukanda wa Gaza haitoshi kukidhi mahitaji ya wakazi wa eneo hilo.
19 Machi 2024
Abdollahian: Iran ina azma ya kuimarisha uhusiano na Niger
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa serikali ya Rais Ebrahim Raisi ina hamu ya kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na nchi za Afrika ikiwemo Niger.
19 Machi 2024
Kuwekwa vikwazo vipya dhidi ya Iran
Wizara ya Fedha ya Marekani kwa mara nyingine imeamua kuweka vikwazo vipya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
19 Machi 2024
Iran: Shutuma za USA na UK kuhusu Bahari Nyekundu na Yemen hazina msingi wowote
Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amekanusha tuhuma zisizo na msingi za Marekani na Uingereza dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu hali ya Bahari Nyekundu na Yemen.
19 Machi 2024
Iran yalaani shambulio katika hospitali ya Al Shifa Ukanda wa Gaza
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kitendo cha ukatili na kinyama cha utawala wa Kizayuni cha kuishambulia hospitali ya al Shifa huko Ukanda wa Gaza.
19 Machi 2024
Jeshi la Israel lashambulia tena Hospitali ya Al-Shifa, laua na kujeruhi kadhaa
Vikosi vya jeshi la utawala wa Israel vilivyojizatiti kwa silaha nzito vimevamia hospitali ya al-Shifa katika mji wa Ghaza kwa kutumia vifaru na ndege zisizo na rubani na kuwafyatulia risasi watu waliokuwa ndani ya jengo hilo.
19 Machi 2024
UN yasema 'imeshtushwa' na mashambulizi mabaya ya anga dhidi ya Waislamu wa Rohingya
Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema Katibu Mkuu wa umoja huo, António Guterres, "amesikitishwa" na ripoti za mashambulizi ya anga yanayoendelea nchini Myanmar ambayo yameua zaidi ya raia 20 katika kitongoji cha Minbya katika Jimbo la Rakhine siku ya Jumatatu.
19 Machi 2024
Thomas Friedman: Netanyahu ndiye kiongozi mbaya zaidi katika historia ya Kiyahudi
Mwandishi na mwanahabari wa Marekani, Thomas Friedman, amesema kuwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ataingia katika historia kama kiongozi mbaya zaidi katika historia ya Kiyahudi.
19 Machi 2024
Borrell: Gaza limegeuka kaburi kubwa zaidi la wazi duniani
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya huku akieleza wasiwasi mkubwa alionao kuhusu mgogoro wa kibinadamu katika Ukanda wa Gaza amesema kuwa, eneo hilo la Wapalestina lililozingirwa limegeuka na kuwa kaburi kubwa zaidi la wazi duniani.
19 Machi 2024
Yemen: Oparesheni dhidi ya meli za Israel zitaendelea
Wizara ya Mambo ya Nje ya serikali ya uokovu wa kitaifa ya Yemen imesisitiza leo katika radiamali yake kwa taarifa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu oparesheni za kijeshi za vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo katika Bahari Nyekundu kuwa oparesheni hizo zitaendelea dhidi ya utawala wa Kizayuni hadi hapo utawala huo utakapositisha jinai zake katika Ukanda wa Gaza.
17 Machi 2024
Waangalizi wa uchaguzi wa OIC: Russia imeandaa fursa za kupiga kura kwa makundi yote ya raia
Mkurugenzi Mkuu wa Masuala ya Kisiasa katika Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) amesema kuwa Russia imeandaa fursa nzuri kwa raia kwa ajili ya kupiga kura.
17 Machi 2024
Kim Jong-un avitaka vikosi vya ulinzi kujiweka tayari kwa ajili ya vita
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ametoa wito kwa vikosi vya jeshi la nchi hiyo kujiweka tayari kikamilifu kukabiliana na mzozo wowote unaoweza kutokea.
17 Machi 2024
Vikwazo vya upande mmoja; ukiukaji wa haki za binadamu
Balozi na Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika makao ya Umoja wa Mataifa barani Ulaya huko Geneva Uswisi amesema kuwa leo hii madhara ya vikwazo haramu vya upande mmoja yamedhihirika wazi mbele ya walimwenu ambapo vimefanya hali ya migogoro ya kibinadamu kuwa mbaya zaidi sambamba na kuchochea ukiukwaji wa haki za kimsingi za binadamu.
17 Machi 2024
Iran yaipongeza Afrika Kusini kwa kuishtaki Israel katika mahakama ya ICJ
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameipongeza na kuishukuru Afrika Kusini kwa uamuzi wake wa kihistoria wa kuwasilisha kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
17 Machi 2024
Waziri wa Ulinzi: Iran iko tayari kuisaidia Syria kuimarisha nguvu zake za kiulinzi na za kuzuia mashambulio
Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Mohammad Reza Ashtiani amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kutumia uwezo wake wote kuisaidia Syria katika kuimarisha ulinzi na uwezo wake wa kuzuia hujuma za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.