Main Title
14 Aprili 2024
Kamanda wa IRGC: Iwapo Israeli itashambulia tena, itapokea jibu kubwa zaidi
Kamanda mwandamizi wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameonya kwamba uvamizi wowote zaidi wa kijeshi utakaofanywa na utawala wa Israel utakabiliwa na jibu kubwa zaidi kutoka Iran.
14 Aprili 2024
Hatua ya kijeshi ya Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni; mfano halisi wa "kujitetea halali"
Katika kujibu shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran huko Damascus, mji mkuu wa Syria, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alfajiri ya Jumapili ya leo tarehe 14 April 2024 imefanya mashambulizi ya moja kwa moja ya ndege zisizo na rubani na makombora katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel).
14 Aprili 2024
Rais Raisi: Hatua yoyote ya kifidhuli itakabiliwa na jibu kali zaidi la Iran
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya harakati yoyote ya kifidhuli utakabiliwa na jibu madhubuti, zito na kali zaidi.
14 Aprili 2024
Kukiri Wazayuni kuhusu uwezo mkubwa wa kistratijia wa Iran
Viongozi wa utawala wa Kizayuni wamekiri kutokuwa na uwezo wa kukabiliana na nguvu na uwezo mkubwa wa kistratijia wa Iran.
14 Aprili 2024
Watu wenye silaha waua abiria 11 kusini magharibi mwa Pakistan
Watu wenye silaha wameua abiria wasiopungua 11 katika matukio mawili tofauti yaliyojiri kusini magharibi mwa Pakistan.
14 Aprili 2024
Biden amwambia Netanyahu kwamba Marekani haitashiriki katika vita vya Israel dhidi ya Iran
Rais Joe Biden wa Marekani amemwambia Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel kwamba Marekani haitashiriki katika mashambulizi yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran.
14 Aprili 2024
Tangu Oktoba 7, jeshi la Israel limefanya mauaji 16 ya halaiki kila siku katika Ukanda wa Ghaza
Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limefanya kwa wastani, mauaji 16 ya halaiki kila siku katika Ukanda wa Ghaza tangu Oktoba 7, 2023 ambako limekuwa likiendesha vita vya kinyama vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo kwa mwezi wa sita sasa.
14 Aprili 2024
HAMAS: Shambulio la Iran ni haki ya kimaumbile na jibu linalostahiki dhidi ya Israel
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, shambulio lililofanywa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) dhidi ya utawala wa Kizayuni ni jibu la kimaumbile na linalostahiki.
14 Aprili 2024
Uamuzi wa Pakistan dhidi ya harakati ya Zainabiyyun; malengo na matokeo yake
Serikali ya Pakistan imechukua uamuzi wa kushtukiza na uliowashangaza na kuwapiga butwaa watu wengi, nao ni wa kuiweka harakati ya Zainabiyyun kwenye orodha yake ya tasisi za kigaidi licha ya kwamba harakati hiyo muda wote imekuwa ikipigania amani na usalama kwa Pakistan.
12 Aprili 2024
Umoja wa Mataifa wabainisha 'wasiwasi mkubwa' kuhusu Israel kuua wafanyakazi wa misaada Gaza
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema limetiwa "wasiwasi mkubwa" na shambulio la anga la hivi karibuni lililofanywa na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza na kuua wafanyakazi saba wa shirika la misaada lenye makao yake makuu nchini Marekani.
12 Aprili 2024
Kwa upinzani wa Marekani, UNSC haijaweza kufikia mwafaka wa kuipatia Palestina uanachama kamili
Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) amesema, japokuwa baraza hilo limefufua matumaini ya Palestina kujiunga na Umoja wa Mataifa kwa kupatiwa uanachama kamili, lakini muafaka juu ya suala hilo bado haujaweza kufikiwa.
12 Aprili 2024
Euro-Med: Zaidi ya Wapalestina 13,000 hawajulikani waliko tangu vilipoanza vita vya Ghaza hadi sasa
Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Mediterranean Human Rights Watch limetangaza kuwa Wapalestina zaidi ya 13,000 wametoweka na hawajulikani waliko tangu vilipoanza vita katika Ukanda wa Ghaza hadi sasa.
12 Aprili 2024
Amir Abdollahian: Kujilinda kwa lengo la kumuadhibu mchokozi ni jambo la lazima
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Jamhuri ya Kislamu ya Iran amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unapokiuka kikamilifu kinga ya watu binafsi na maeneo ya kidiplomasia kwa kukanyaga sheria za kimataifa na Mikataba ya Vienna, inakuwa lazima kujihami kwa lengo la kumuadhibu mchokozi.
12 Aprili 2024
Mwakilishi wa Iran UN asisitiza ulazima wa kuuadhibu utawala vamizi wa Israel
Ofisi ya Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa imesema Baraza la Usalama lilipaswa kulaani mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya maeneo ya kidiplomasia ya Iran huko Damascus, mji mkuu wa Syria.
12 Aprili 2024
Raisi: Madola ya kibeberu yanazusha fitna ili kuvuruga usalama kati ya Iran na Pakistan
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kustawishwa uhusiano wa Iran na Pakistan hakufurahishi madola ya kibeberu na kwa hivyo yanazusha fitna ili kuleta mpasuko kati ya mataifa hayo mawili na nchi hizo mbili za Kiislamu.
12 Aprili 2024
Imamu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Utawala wa Kizayuni unakaribia kutoweka
Imamu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amelaani mauaji na jinaii zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza na kusema: Utawala huo unaelekea kuporomoka.
12 Aprili 2024
UN: Israel inaichezea tu misamiati kama "ngao ya binadamu" na "maeneo yenye usalama"
Ripota wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu amesisitiza kuwa, viongozi wa utawala wa Kizayuni na askari wa utawala huo wanapotosha na wanaichezea misingi ya sheria za kimataifa ili kuhalalisha ukatili na uchokozi wao.
12 Aprili 2024
Haaretz: Serikali ya Netanyahu imeshindwa vibaya kwenye vita vya Ghaza
Chombo kimoja cha habari cha utawala wa Kizayuni kimekiri kwamba Wazayuni wote wanakiri kuwa serikali ya Benjamin Netanyahu imeshindwa vibaya kwenye vita vya Ghaza.
12 Aprili 2024
Haniyeh: Hamas haitalegeza kamba baada ya mauaji ya Israel dhidi ya wanangu
Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema mauaji yalitofanywa na Israel dhidi ya watoto wake hayataifanya harakati hiyo na ukombozi wa Palestina kulegeza kamba katika malengo na matakwa yake katika mazungumzo yenye lengo la kufikia mwafaka kuhusu vita vya Gaza.
12 Aprili 2024
Kuongezeka kimataifa uungaji mkono kwa kampeni ya kususia bidhaa za Israeli
Huku mauaji ya kimbari yakiwa yanaendelea kufanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya watu wa Gaza, nchi nyingi duniani zinaendelea kujiunga na kampeni ya kususia bidhaa za Israel na vilevile za makampuni mengi ya Kimarekani yanayouunga mkono utawala huo wa kibaguzi.