Main Title
3 Aprili 2024
Baraza la Usalama laitisha kikao cha dharura kuhusu shambulio la Israel kwenye ubalozi wa Iran
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitisha kikao cha dharura cha kujadili shambulizi la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria kikao ambacho kimeshuhudia kulaaniwa vikali Israel kwa shambulio lake hilo la kigaidii.
3 Aprili 2024
Mtaalamu wa UN: Israel 'iliwaua kimakusudi' wafanyakazi wa misaada Gaza
Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu anasema jeshi la Israel "limewaua kimakusudi" wafanyakazi wa misaada wa Kundi la Misaada la World Central Kitchen, WCK katika Ukanda wa Gaza.
3 Aprili 2024
Dunia yaendelea kulaani shambulio la kigaidi la Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria
Dunia imeendelea kulaani vikali sambulio la utawala haramu wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria huku Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya mkutano wa dharura kuhusu mgomo huo mbaya.
3 Aprili 2024
Salwan Momika, Muiraki aliyiivunjia heshima Qur'an mara kadhaa, aripotiwa kufariki akiwa Norway
Mkimbizi wa Iraq, Salwan Momika, ambaye alivunjia heshima nakala za Qur'ani Tukufu mara kadhaa mwaka jana, ameripotiwa kupatikana amefariki nchini Norway.
3 Aprili 2024
Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la Israel lililolenga ubalozi mdogo wa Iran Damascus
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria na kuonya kwamba mahesabu yoyote ya kimakosa yanaweza kusababisha mapigano yenye wigo mpana zaidi katika eneo hili tete na lisilo na uthabiti na kusababisha matokeo haribifu kwa raia.
3 Aprili 2024
Rais Ebrahim Raisi: Israel iko kwenye sakaratul mauti, inakata roho
Rais Ebrahim Raisi amesema kuwa, shambulio la juzi Jumatatu la utawala wa Kizayuni kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria ni ushahidi kuwa Israel iko kwenye sakaratul mauti na inakata roho hivi sasa.
3 Aprili 2024
Baraza la Usalama UN lalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran, Damascus
Wawakilishi waliohudhuria kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran huko Damascus (mji mkuu wa Syria) wamelaani kitendo hicho cha kinyama cha Wazayuni.
3 Aprili 2024
Mazishi ya washauri wa kijeshi wa Iran waliouawa katika hujuma ya Israel jijini Damascus
Maelfu ya watu wameshiriki katika msafara wa mazishi ya washauri wa kijeshi wa Iran, waliouawa shahidi katika shambulizi la makombora la utawala haramu wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria Damascus.
3 Aprili 2024
Hatua mpya ya BRICS kufuta sarafu ya dola ya Marekani
Jumuiya ya BRICS ya mataifa yanayoibukia kiuchumi inajadili uwezekano wa kubuni mfumo huru wa malipo unaozingatia sarafu za kidijitali ili kupunguza utegemezi kwa mifumo ya fedha ya nchi za magharibi.
3 Aprili 2024
Tofauti ya Siku ya Quds ya mwaka huu na ya miaka iliyopita
Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu inakaribia katika hali ambayo siku hiyo itakuwa tofauti kabisa na siku nyingie za Quds za karne hii ya 21.
2 Aprili 2024
Mbunge wa Marekani ataka kadhia ya Ghaza imalizwe kama zilivyofanyiwa Hiroshima na Nagasaki
Tim Walberg, Mbunge wa jimbo la Michigan Kusini nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican amelazimika kufuta kauli aliyotoa ya kutaka Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, ambao ni makazi ya zaidi ya watu milioni mbili, ushughulikiwe kama ilivyofanyiwa miji ya Nagasaki na Hiroshima ya Japan ambayo ilishambuliwa na Marekani kwa mabomu ya nyuklia.
2 Aprili 2024
Utawala wa Kizayuni washambulia jengo la ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria
Utawala ghasibu wa Kizayuni umetekeleza shambulio la anga dhidi ya jengo la ubalozi mdogo wa Iran karibu na ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huko Damascus Syria.
2 Aprili 2024
Naibu Katibu Mkuu wa UN: Jaribio la kuitenga UNRWA lazima likome
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na uratibu wa misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura Martin Griffiths amesema shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ni uti wa mgongo wa operesheni za kibinadamu Ghaza, hivyo jaribio la kulitenga shirika hilo lazima likome.
2 Aprili 2024
Iran: Uchunguzi wa kimataifa ufanyike kuhusu jinai ilizofanya Israel katika Hospitali ya Al-Shifa
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitizia ulazima wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na uharibifu, utesaji na mauaji yaliyofanywa na jeshi la Kizayuni katika Hospitali ya Al-Shifa huko Ukanda wa Ghaza.
2 Aprili 2024
Shambulio la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran Damascus lalaaniwa kimataifa
Russia, Pakistan, Oman, Imarati na Qatar zimeungana na mataifa mengine kuulaani utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kufuatia shambulio la kigaidi ulilofanya utawala huo katika ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus, Syria.
2 Aprili 2024
Balozi wa Iran Syria: Tutajibu mapigo kwa Israel sawa na ilivyoshambulia ubalozi wetu mdogo
Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Syria amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo sawa na utawala wa Kizayuni wa Israel ulivyoshambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.
2 Aprili 2024
Iran: Utawala wa Kizayuni ni tishio kwa usalama na amani ya dunia nzima
Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa na taasisi nyinginezo za kimataifa huko Geneva Uswisi amelaani vikali jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria na kusema kuwa Israel ni utawala unaohatarisha usalama wa dunia nzima na unapuuza kikamilifu hati ya Umoja wa Mataifa.
2 Aprili 2024
Rais Raisi: Wazayuni kamwe hawatofikia malengo yao haramu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumzia jinai na ugaidi uliofanywa jana Jumatatu na utawala wa Kizayuni wa kushambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria na kusema kuwa, Wazayuni wanapaswa kutambua kwamba ugaidi wao wa kinyama kama huo hauwezi kuwafanikishia malengo yao maovu.
2 Aprili 2024
Kiongozi Muadhamu: Iran itaufanya utawala wa Israel ujutie uhalifu nchini Syria
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu za rambirambi kufuatia kuuawa shahidi Majenerali walioongoka wa Kiislamu katika shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria na kusisitiza kwamba: "Taifa la Iran litawafanya Wazayuni wajutie jinai hiyo na jinai zingine kama hiyo."
2 Aprili 2024
Sababu za utawala wa Kizayuni kulazimisha vita katika upande wa kaskazini
Yoav Gallant, Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni, amesema kwamba utawala huo haramu utapanua operesheni zake za kijeshi katika eneo la kaskazini la ardhi zinazokaliwa kwa mabvu na kushambulia kila sehemu ya Beirut na Damascus ambapo Hizbullah ya Lebanon inaendeshea shughuli zake.