Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA likinukuu mtandao wa Russia Al-Yaum, Pete Hegseth, Waziri wa Vita wa Marekani, alitangaza: "Nilikubaliana na mwenzangu wa China, Dong Jun, juu ya umuhimu wa kuanzisha njia za [mawasiliano] za kijeshi ili kuzuia kutokea kwa migogoro na kudhibiti ongezeko lolote la mvutano kati ya nchi hizo mbili."
Katika matamshi mengine, alisema: "Nilizungumza na Rais Trump na wote wawili tunaamini kwamba mahusiano kati ya Marekani na China sasa yako katika hali yake bora zaidi."
Hegseth aliongeza: "Baada ya mkutano wa kihistoria wa Rais Trump na Rais wa China, Xi Jinping, huko Korea Kusini, pia nilikuwa na mkutano mzuri sana na Waziri wa Ulinzi wa China, Dong Jun, huko Malaysia, na usiku wa kuamkia leo tulifanya mazungumzo mapya kati yetu."
Waziri wa Vita wa Marekani alifafanua: "Nilikubaliana na Waziri wa Ulinzi wa China kwamba amani, utulivu na mahusiano mazuri ndiyo njia bora kwa nchi zetu mbili kubwa na zenye nguvu."
Pia, katika sehemu nyingine ya hotuba yake, alirudia matamshi ya "Crusader" ya Trump kuhusu mauaji ya Wakristo nchini Nigeria na kudai: "Mauaji ya Wakristo wasio na hatia nchini Nigeria na mahali popote duniani lazima yasitishwe mara moja."
Hegseth, akithibitisha matamshi ya Trump kuhusu uwezekano wa hatua za kijeshi za Marekani nchini Nigeria na kuonya nchi hiyo, alisema: "Wizara ya Vita ya Marekani inajiandaa kuchukua hatua; aidha serikali ya Nigeria itawalinda Wakristo, au tutawaangamiza magaidi wa Kiislamu wanaofanya uhalifu huu wa kutisha."
Your Comment