Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Jarida la The Atlantic limeandika kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, badala ya kuwajibika kwa kile jarida hilo linachokitaja kuwa kutofanikiwa katika vita dhidi ya Iran, ameelekeza shinikizo dhidi ya baadhi ya washirika wa Marekani.
Kwa mujibu wa jarida hilo, Trump haonekani kuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu uwepo wa makumi ya vichwa vya nyuklia vya Korea Kaskazini, huku Korea Kusini ikiwa katika mazingira ya shinikizo.
The Atlantic imedai kuwa kwa kuwa Trump hakufanikiwa kuishinda Iran au kuilazimisha Tehran kusalimu amri, sasa kuna haja ya upande mwingine kubeba gharama ya kushindwa huko, na kwamba kwa wakati huu Korea Kusini imekuwa miongoni mwa walengwa wanaofaa zaidi.
Jarida hilo limeongeza kuwa mtazamo huo unatuma ujumbe kwa washirika wa Marekani kwamba huenda wasiweze tena kutegemea ahadi na dhamana za Washington kama ilivyokuwa hapo awali.
Kwa mujibu wa The Atlantic, hali hiyo inaweza kuongeza mashaka miongoni mwa washirika wa Marekani kuhusu kiwango cha uaminifu na uthabiti wa ahadi za Washington katika masuala ya usalama.

Maoni yako