Balozi za Iran na Saudia zinafunguliwa rasmi leo na kesho, Tehran na Riyadh
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, balozi za Saudi Arabia na Iran zinafunguliwa rasmi leo Jumanne na kesho Jumatano katika miji mikuu ya nchi hizi mbili ikiwa ni utekelezaji wa makubaliano ya pande mbili ya kurejesha kikamilifu uhusiano wao wa kidiplomasia.