Palestina yafichua: Ulaya inatushinikiza tuchukue msimamo wa kuilaani Russia
Waziri wa Mambo ya Nje wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amefichua kuwa Ulaya inaishinikiza Palestina ichukue msimamo wa kuilaani Russia sambamba na kueleza kwamba amepokea mwaliko kutoka kwa mwenzake wa Russia wa kuzuru Moscow.