• Intro
  • Kuhusu sisi
  • RSS
Arabic English Persian Turkish Urdu Spanish Indonesian Hindi French Chinese Russian German Melayu Hausa Bengali Azeri Latin Azeri Cyrillic Swahili Myanmar Bosnian Portuguese Sourani Japanese Kurmanji Philippines
  • Habari Kamili
  • Habari Muhimu
  • Iran
  • Asia
  • Ulaya
  • Amerika
  • Afrika
  • Picha
  • Makala
  • Habari maalum
Menu
  • Maskani

  • Habari Kamili

  • Habari Muhimu

  • Iran

  • Asia

  • Ulaya

  • Amerika

  • Afrika

  • Picha

  • Makala

  • Habari maalum

Marekebisho Habari za Ulaya
  • Dk Tedros Adhanom achaguliwa tena kwa muhula wa pili kuwa Mkurugenzi Mkuu wa WHO

    Mei 25, 2022 - 5:46 PM

    Nchi wanachama wa Shirika la Afya Duniani (WHO) jana Jumanne zilithibitisha kuchaguliwa tena Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa kwa kipindi kingine cha pili.

    Endelea ...
  • Mfumuko wa bei za vyakula, mgogoro wa pili kwa ukubwa UK; vikwazo vya Russia vyachangia

    Mei 25, 2022 - 5:45 PM

    Matokeo ya uchunguzi wa maoni waliofanyiwa wananchi wa Uingereza yanaonesha kuwa, mfumuko wa bei za vyakula umefikia kiwango cha juu kabisa nchini humo kuliko miaka 13 iliyopita na kwamba mfumuko huo ni mgogoro wa pili kwa ukubwa huko Uingereza baada ya kupanda vibaya bei ya nishati.

    Endelea ...
  • Indhari; hali mbaya kabisa ya uchumi wa dunia kuwahi kushuhudiwa tangu Vita vya Pili vya Dunia

    Mei 25, 2022 - 5:44 PM

    Baada ya miaka miwili ya msambao wa maradhi ya Covid-19 pamoja na matokeo mabaya yaliyosababishwa na janga hilo na katika hali ambayo, mataifa mbalimbali yalikuwa katika mkakati wa kuboresha uchumi, kutokea vita vya Ukraine na Russia kumevuruga zaidi hali ya uchumi wa dunia.

    Endelea ...
  • Nchi nne wanachama wa EU zataka fedha za Russia zilizozuiliwa zitumike kuijenga upya Ukraine

    Mei 24, 2022 - 6:06 PM

    Nchi nne wanachama wa Umoja wa Ulaya (EU) zinatazamiwa kuwasilisha rasmi katika umoja huo barua ya kutaka mali na fedha za Russia zilizozuiliwa na EU zitumiwe kuijenga upya Ukraine baada ya kumalizika vita.

    Endelea ...
  • Mabadiliko katika Baraza la Mawaziri la Macron, marekebisho yanayolenga kutafuta kukubalika na umma

    Mei 22, 2022 - 4:30 PM

    Mwezi mmoja baada ya kufanyika uchaguzi wa Rais nchini Ufaransa Emmanuel Macron Rais wa nchi hiyo akiwa na lengo la kutafuta uungaji mkono na kuwaridhisha wapigakura na hivyo serikalii yake iungwe mkono zaidi, amelifanyia mabadiliko baraza lake la mawaziri.

    Endelea ...
  • Hungary: Vikwazo dhidi ya Russia ni bomu la Atomiki

    Mei 22, 2022 - 3:45 PM

    Waziri Mkuu wa Hungary amesema kuwa, vikwazo vya nchi za Ulaya na Marekani dhidi ya Russia ni sawa na bomu la nyuklia na vitazidisha njaa duniani na kuongeza wimbi la wakimbizi.

    Endelea ...
  • Russia yachukua udhibiti kamili wa mji wa Mariupol, Ukraine

    Mei 21, 2022 - 5:48 PM

    Russia imetangaza kuchukua udhibiti kamili wa mji muhimu wa Mariupol nchini Ukraine baada ya wanajeshi wa mwisho wa Ukraine waliokuwa katika kiwanda cha chuma cha Azovstal kujisalimisha Ijumaa.

    Endelea ...
  • Vigezo vya nyuso mbili vya nchi za Ulaya katika suala la wakimbizi

    Mei 19, 2022 - 2:25 PM

    Huku mgogoro wa kiuchumi na kisiasa ukiendelea katika baadhi ya nchi za Asia na huku vita baina ya Ukraine na Russia navyo vikiendelea, wimbi la wakimbizi katika mipaka ya nchi za Ulaya nalo limeongezeka.

    Endelea ...
  • Russia: Hatutoruhusu kutokea Vita vya Tatu vya Dunia

    Mei 19, 2022 - 2:24 PM

    Naibu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia amesisitiza kuwa, Moscow haitoruhusu kutokea Vita vya Tatu vya Dunia.

    Endelea ...
  • Benki ya Dunia yatenga dola bilioni 30 kukabili mgogoro wa chakula uliosababishwa na vita vya Ukraine

    Mei 19, 2022 - 2:20 PM

    Benki ya Dunia imetangaza kuwa, imetenga dola bilioni 30 za misaada kwa ajili ya kudhibiti mgogoro wa chakula duniani uliosababishwa na vita vya Ukraine.

    Endelea ...
  • Njama za Magharibi za kuanzisha NATO ya dunia nzima

    Mei 18, 2022 - 11:24 PM

    Katika hali ambayo suala la uwanachama wa nchi mbalimbali hasa Ukraine katika Jeshi la Nchi za Magharibi NATO limeitumbukiza dunia kwenye mgogoro wa kimataifa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza ameona kama hiyo haitoshi na hivi sasa amezungumzia wajibu wa kuweko mkataba wa NATO ya dunia nzima.

    Endelea ...
  • Kushindwa Umoja wa Ulaya kuiwekea vikwazo vya mafuta Russia

    Mei 18, 2022 - 11:20 PM

    Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya kikao cha mawaziri wa umoja huo mjini Brussels Ubelgiji kwamba, hakuna uwezekano wa kufikiwa makubaliano kuhusiana na kifurushi cha sita cha vikwazo dhidi ya Russia.

    Endelea ...
  • Marekani na NATO zafanya mazoezi ya kijeshi karibu na mipaka ya Russia

    Mei 17, 2022 - 9:25 PM

    Mazoezi ya kijeshi ya pamoja baina ya Marekani na Jeshi la Nchi za Magharibi NATO yanaendelea hivi sasa katika ardhi ya Estonia, karibu na kambi za kijeshi za Russia.

    Endelea ...
  • Lavrov: Nchi za Magharibi zimehodhiwa na kudhibitiwa na Marekani

    Mei 17, 2022 - 9:24 PM

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov, ametahadharisha kuhusu uamuzi ilioamua kuchukua Sweden wa kujiunga na shirika la kijeshi la NATO na kueleza kwamba nchi za Magharibi zimehodhiwa na kudhibitiwa na Marekani.

    Endelea ...
  • Russia: Tumeteketeza vituo 104 vya kiijeshi vya Ukraine hadi hivi sasa

    Mei 16, 2022 - 7:03 PM

    Wizara ya Ulinzi wa Russia imetangaza kuwa, hadi hivi sasa operesheni maalumu ya kijeshi ya nchi hiyo huko Ukraine iimeshateketeza vituo 104 vya kijeshi vya Ukraine.

    Endelea ...
  • Polisi ya Ujerumani yamweka kizuizini mratibu wa EU katika mazungumzo ya nyuklia akitokea Iran

    Mei 14, 2022 - 9:57 PM

    Polisi ya Ujerumani jana ilimkamata na kumweka kizuizini kwa muda Enrique Mora, mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya anayehusika na uratibu wa mazungumzo ya nyuklia ya Vienna wakati anaelekea Brussels akitokea Iran.

    Endelea ...
  • EU yalegeza kamba mbele ya Russia yaachana na mpango wa kuzuia meli zake za mafuta

    Mei 11, 2022 - 11:13 PM

    Vyombo vya habari vya barani Ulaya vimetangaza kuwa nchi za bara hilo zimelegeza msimamo mbele ya Moscow na sasa hazitoendelea na mpango wake wa kutaka kuzizuia meli za mafuta za Russia.

    Endelea ...
  • Putin: Tulizuia Ulaya kuvamia Russia kwa kuanzisha oparesheni ya kijeshi Ukraine

    Mei 10, 2022 - 4:43 PM

    Rais Vladimir Putin wa Russia ametetea oparesheni za kijeshi ambazo nchi yake ilianzisha dhidi ya Ukraine na kusema ilibidi afanye hivyo kwani nchi za Ulaya zilikuwa zinapanga kuishambulia Russia kijeshi.

    Endelea ...
  • Ugomvi baina ya Russia na Wazayuni waongezeka, Moscow yakabidhi kambi zake kwa Iran

    Mei 10, 2022 - 4:08 PM

    Gazeti la Times la linalochapishwa mjini Moscow limeandika kuwa, Russia imeanza kuondoa wanajeshi wake nchini Syria na inakabidhi kambi zake kwa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.

    Endelea ...
  • Russia yasema imeharibu silaha ambazo Ukraine ilipokea kutoka Marekani, Ulaya

    Mei 8, 2022 - 6:38 PM

    Wizara ya Ulinzi ya Russia inasema imefanikiwa kuharibu idadi kubwa ya silaha na zana za kivita ambazo Ukraine imepokea kutoka Marekani na Ulaya.

    Endelea ...
  • Nebenzia: Dunia imo katika vita vya kiuchumi vya dunia

    Mei 7, 2022 - 10:17 PM

    Balozi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa vita vya dunia katika upeo wa kiuchumi vinaendelea sasa dhidi ya Russia kwa ajili ya kukabiliana na operesheni maalumu ya kijeshi ya Russia nchini Ukraine.

    Endelea ...
  • Lavrov: Vikwazo vya Magharibi haviwezi kuvunja irada ya wananchi wa Russia

    Mei 7, 2022 - 10:16 PM

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov amesema, vikwazo vya Magharibi havina athari yoyote mbele ya irada ya watu wa nchi hiyo.

    Endelea ...
  • Emmanuel Macron aapishwa kuhudumu kwa muhula wa pili

    Mei 7, 2022 - 10:14 PM

    Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron leo ameapishwa kwa ajili ya kuhudumu kwa muhula wa pili kufuatia ushindi wake alioupata katika uchaguzi wa hivi karibuni.

    Endelea ...
  • WHO yazindua ripoti ya kwanza ya kimataifa kuhusu kuzuia na kudhibiti maambukizi

    Mei 7, 2022 - 10:12 PM

    Shirika la Afya la Duniani (WHO) limezindua ripoti ya kwanza kabisa ya kimataifa kuhusu njia ya vitendo, yenye msingi wa ushahidi wa kulinda wagonjwa na wahudumu wa afya wasidhuriwe na maambukizi yanayoweza kuepukika.

    Endelea ...
  • Russia yawafukuza wanadiplomasia 7 wa Denmark kulipiza kisasi

    Mei 6, 2022 - 6:50 PM

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetoa taarifa na kutangaza kuwa, nchi hiyo inawatambua wanadiplomasia saba wa ubalozi wa Denmark huko Moscow kuwa watu wasiofaa na imechukua uamuzi wa kuwafukuza nchini humo.

    Endelea ...
  • Kuongezeka upinzani barani Ulaya dhidi ya kuwekewa vikwazo vya mafuta Russia

    Mei 6, 2022 - 6:48 PM

    Licha ya vitisho vya Umoja wa Ulaya kuhusiana na kuiwekea vikwazo vya mafuta Russia katika fremu ya kifurushi cha sita cha vikwazo dhidi ya nchi hiyo, lakini jambo hilo linaonekana kukabiliwa na upinzani mkali barani humo na hata baadhi ya viongozi wa Marekani kutoa onyo dhidi ya hatua hiyo.

    Endelea ...
  • Russia yapongeza kuimarika uhusiano wake na nchi za Asia ya Kati

    Mei 6, 2022 - 6:46 PM

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia ameelezea kufurahishwa na kuzidi kuimarika uhusiano wa Moscow na nchi za Asia ya Kati.

    Endelea ...
  • WHO: Vifo vilivyosababishwa na corona duniani ni mara tatu zaidi ya vilivyotangazwa

    Mei 6, 2022 - 6:43 PM

    Ripoti mpya ya Shirika la Afya Duniani (WHO) inaonesha kuwa idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 ni mara 3 zaidi ya idadi iliyorekodiwa katika data rasmi, ikimaanisha kuwa karibu watu milioni 15 zaidi wameaga dunia kutokana na virusi vya corona.

    Endelea ...
  • Russia: Mamluki wa Kizayuni wanapigana bega kwa bega na Waukraine

    Mei 6, 2022 - 1:21 AM

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema kuwa, mamluki wa Israel wanapigana bega kwa bega na vikosi vya jeshi la Ukraine.

    Endelea ...
  • Russia kusitisha vita kwa muda mjini Maripoul, Ukraine ili raia waondoke

    Mei 6, 2022 - 1:18 AM

    Russia imetangaza usitishaji vita wa siku tatu katika mji wa bandarini wa Mariupol nchini Ukraine ili kuruhusu raia waliokwama katika kiwanda kimoja cha chuma waondoke.

    Endelea ...
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • Next
Haki zote zimehifadhiwa

All Content by AhlulBayt (a.s.) News Agency - ABNA is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License