Shirika la habari la Ahlu Bayt (ABNA):
Katika hali ambayo Italy inahitajia msaada zaidi, Umoja wa Ulaya umeonekana kutupilia mbali mawazo ya kuisaidia hata katika misaada ya kitabibu.
Baadhi ya misaada hasa ya kitabibu ikiwa ni pamoja na vifaa maalumu vya kujikinga na virusi (mask) ambazo zilikuwa zikisafirishwa kutokea nchini China, ilionekana kuzuiliwa njiani katika nchi ya Jamhuri ya Cheki.
Italy inaonekana kuwa ni muhanga mkubwa wa janga la Corona, kiasi kwamba idadi ya wahanga nchini humo ni zaidi hata ile iliyosajiliwa nchini China.