Main Title

source : Parstoday
Jumanne

15 Novemba 2022

16:39:05
1323352

Uingereza yaazimia kuwaondoa askari wake nchini Mali

Uingereza imetangaza habari ya kutaka kuwaondoa mamia ya askari wa nchi hiyo walioko nchini Mali chini ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa MINUSMA.

Waziri wa Vikosi vya Majeshi ya Uingereza, James Heappey ameliambia Bunge la nchi hiyo kuwa, serikali ya London haiwezi kuvumilia udhalilishaji wa nchi mwenyeji, ambayo eti haina azma ya kushirikiana na nchi hiyo ya Ulaya kurejesha uthabiti na usalama wa kudumu katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Amesema wimbi la mapinduzi yaliyoshuhudiwa hivi karibuni nchini Mali linakwamisha jitihada za kimataifa za eti kupambana na ugaidi nchini humo, na kwa msingi huo Uingereza itawaondoa wanajeshi wake 300 katika nchi hiyo ya eneo la Sahel barani Afrika.

Hii ni katika hali ambayo, mabaki ya wanajeshi wa Ufaransa waliondoka nchini Mali Agosti mwaka huu, kuashiria mwisho wa Operesheni ya Barkhane katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.

Vikosi vya wanajeshi 2,400 wa Ufaransa vimekuwepo nchini Mali kwa takriban miaka 10 kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi. Kikosi cha MINUSMA kina askari wapatao 14,000.

Viongozi wa kijeshi walioko madarakani nchini Mali tangu mwezi Agosti mwaka 2020 waliamua kusitisha ushirikiano na  Ufaransa na nchi nyingine za Magharibi, na sasa wanashirikiana na Russia katika vita dhidi ya magaidi.

342/