Taarifa ya Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani imesema: inatambua na kuruhusu kinga hiyo huku ikiashiria mamlaka iliyonayo ya kikatiba na pia sheria ya kijadi ya kimataifa. Imeongeza kuwa, katika kesi hii Waziri Mkuu bin Salman anayo kinga akiwa mamlakani kutoka katika Mahakama hii ya wilaya ya Marekani.
Itakumbukwa kuwa aliyekuwa mchumba wa Jamal Khashoggi, Hatice Cengiz alikuwa amefungua kesi kuhusu mauaji hayo ya kutisha ya Khashoggi katika mahakama ya wilaya huko Washington DC.
Ilidaiwa kwamba, Khashoggi aliyekuwa raia wa Marekani na mwandishi habari katika gazeti la Washington Post aliteswa, kuuawa na kisha kukatwa vipande vipande kwa amri ya Muhammad bin Salman. Jamal Khashoggi aliuawa ndani ya ubalozi mdogo wa Saudi Arabia huko Istanbul, Uturuki. Aidha Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) awali lilithibitisha kwamba mtawala huyo wa Saudia ndiye aliyehusika na mauaji hayo.
Mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, Muhammad bin Salman alitangazwa kuwa Waziri Mkuu wa Saudi Arabia katika hatua ambayo weledi wa mambo waliamini kuwa, ilihusishwa na kesi hiyo kwa lengo la kumkinga na hatua zozote za kisheria ambazo zingechukuliwa katika uwanja huo.
342/