Main Title

source : Abna
Jumatano

11 Desemba 2024

19:05:16
1513097

Ujumbe kutoka kundi la Tahrir al-Sham ulitembelea Madhabahu / Haram Tukufu ya Hazrat Ruqayyah (s.a) + Video

Ujumbe kutoka kundi la Tahrir al-Sham ulitembelea Madhabahu / Tukufu ya Hazrat Ruqayyah (s.a) katika Mji wa Damascus.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Uongozi wa Haram Tukufu ya Hazrat Ruqayyah (s.a) umetoa taarifa juu ya ziara ya ujumbe wa kundi la Tahrir al-Sham katika Haram hii Tukufu huko katika mji wa Damascus.

Imeelezwa katika taarifa hii kama ifuatavyo: Tunapenda kuwafahamisha Wapenzi wa Haram Tukufu ya Hadhrat Ruqayyah (amani iwe juu yake) kwamba wajumbe kutoka kundi la Tahrir al-Sham walitembelea Haram hiyo Tukufu kwa kuchunga heshima kamili, adabu na desturi za Kiislamu, na kisha kuondoka kwenye Haram hiyo baada ya muda saa moja.

Inafaa kuashiria kuwa katika Harakati za kubadilisha Serikali ya Syria na kuchukua Madaraka ya Kundi la Tahrir al-Sham katika nchi hii, hapakuwa na uvamizi wowote kwenye Madhabahu / Haram ya Hadhrat Ruqayyah (s.a) na eneo hili Tukufu liko katika usalama kamili katikati mwa Mji wa Damascus.