Katika ripoti yake, taasisi hii ya Palestina ilieleza takwimu za hivi punde kuhusiana na vita hivi vya uharibifu, ambazo unaweza kuziona hapa chini kama ifuatavyo:
- Siku 460 za vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya Gaza.
- Jinai 10,015 zilizofanywa kwa ujumla na jeshi Vamizi la Kizayuni.
- Jinai 7,182 zilizofanywa na wavamizi wa Kizayuni dhidi ya familia za Wapalestina.
- Familia 1,600 ziliharibiwa kabisa, ambapo idadi yao ilikuwa watu 5,612.
- Familia 3,471 za Wapalestina, ni mmoja tu kati yao aliyebaki hai, na idadi ya Mashahidi wa familia hizi ilikuwa ni watu 9,000.
- 57,136 wamekuwa Mashahidi na waliopotea..
- Watu 11,200 waliopotea ambao miili yao bado haijasajiliwa Hospitalini.
- Mashahidi 45,936 ambao wamesajiliwa rasmi Hospitalini.
- Watoto 17,841 waliouawa Kishahidi.
- Watoto 240 waliouawa Kishahidi baada ya kuzaliwa katika vita vya mauaji ya kimbari.
- Watoto 858 walio chini ya mwaka mmoja waliouawa katika vita hivi.
- Mashahidi 44 waliouawa kutokana na utapiamlo.
- Mashahidi 8 waliouawa kwa sababu ya baridi kali, 7 kati yao walikuwa watoto.
- Mashahidi 12,298 Wanawake.
- Mashahidi 1,668 kutoka kwa wafanyakazi wa matibabu.
- Mashahidi 94 kutoka idara ya ulinzi wa raia.
- Mashahidi 202 Wanahabari.
- Mashahidi 736 kutoka kwa vikosi vya Polisi ambao walifanya kazi kwa ajili ya usalama wa misaada ya kibinadamu.
- 149 Kwa kulenga vikosi vya Polisi vilivyofanya kazi kwa ajili ya usalama wa misaada ya kibinadamu.
- Makaburi 7 ya halaiki yaliyoundwa na Jeshi vamizi la Kizayuni katika Hospitali.
- Mashahidi 520 waliondolewa kutoka kwenye makaburi 7 ya halaiki katika Hospitali.
- Watu 109,274 walijeruhiwa ambao walikwenda Hospitalini (kupata matibabu).
- 399 ni walijeruhiwa waandishi na wana habari.
- 70% ya waliojeruhiwa walikuwa watoto na wanawake.
- Vituo 218 vya makazi ya wakimbizi vilivyolengwa na wavamizi wa kizayuni.
Asilimia 10 ya maeneo ya Ukanda wa Gaza yameteuliwa kuwa maeneo ya kibinadamu na wavamizi.
- Watoto 35,074 wamebakia bila wazazi Baba na Mama au mmoja wao.
- Wanawake 12,132 waliopoteza waume zao.
- Watoto 3,500 wako katika hatari ya kifo kutokana na utapiamlo na ukosefu wa dawa.
- Siku 246 za kizuizi cha kivuko cha mwisho cha Gaza kulichowekwa na wavamizi wa kizayuni.
- Majeruhi 12,600 wanaohitaji kuondoka Gaza kwa ajili ya matibabu.
- Wagonjwa 12,500 wa saratani ambao wanapaswa kuondoka Gaza ili kuendelea na matibabu yao.
- Wagonjwa 3,000 tofauti wanaohitaji kuondoka Gaza kwa ajili ya matibabu zaidi.
- Kesi 2,136,026 za magonjwa ya kuambukiza kwa sababu ya kuhama (kuhamasishwa na kuwa wakimbizi).
- Kesi 71,338 za hepatitis C kwa sababu ya kuhama (Kuhamasishwa na kufanywa Wakimbizi).
- Wajawazito 60,000 ambao wako hatarini kutokana na ukosefu wa usafi.
- Wagonjwa 350,000 wa muda mrefu wako hatarini kutokana na ukosefu wa dawa.
- Wafungwa 6,600 kutoka Ukanda wa Gaza tangu kuanza kwa mauaji ya kimbari ya uvamizi huo wa Kizayuni.
- 331 Ni wafanyakazi wa matibabu (madaktari) waliokamatwa, ambapo 3 kati yao waliuawa gerezani.
- Kukamatwa kwa watu 43 ambao ni waandishi wa habari na ambao utambulisho wao umebainishwa.
- Kesi 26 za kukamatwa kwa vikosi vya ulinzi wa raia.
- Watu 2,000,000 waliokimbia makazi yao katika Ukanda wa Gaza.
Mahema 11,000 yamejengwa, lakini wakati huo huo, hayafai kwa waliohamishwa (na kutolewa kwenye makazi yao).
- Majengo 214 ya Serikali yameharibiwa katika mashambulizi ya wavamizi wa kizayuni.
- Shule na vyuo vikuu 136 vimeharibiwa kabisa na wavamizi.
- Shule na vyuo vikuu 335 vimeharibiwa mfululizo.
- Wanafunzi 12,794 waliuawa katika vita.
- Wanafunzi 785,000 wamenyimwa elimu wakati wa vita.
- Walimu na wafanyakazi 756 wa sekta ya elimu wameuawa Shahidi.
- Maprofesa na watafiti 149 wa vyuo vikuu wameuawa.
- Misikiti 823 imeharibiwa kabisa.
- Misikiti 158 imeharibiwa kwa kiasi.
- Makanisa 3 yameharibiwa.
- Makaburi 19 kati ya jumla ya 60 yameharibiwa kabisa na kwa kiasi.
- Miili 23,000 imeibiwa kutoka kwenye makaburi na wavamizi wa kizayuni.
- Makazi 161,600 yameharibiwa kabisa.
- Makazi 82,000 hayafai kwa kuishi ndani yake.
- Makazi 194,000 yameharibiwa kwa kiasi.
- Tani 88,000 za vilipuzi zimedondoshwa kwenye Ukanda wa Gaza.
- Hospitali 34 ziko nje ya mzunguko wa utoaji wa huduma.
- Vituo vya matibabu 80 viko nje ya mzunguko wa utoaji wa huduma.
- Taasisi za matibabu 162 zimelengwa (kwa kushambuliwa).
- Magari 136 ya kubebea wagonjwa yalishambuliwa na wavamizi wa kizayuni.
- Athari 206 za kihistoria zimeharibiwa.
- Kilomita 3,130 za mtandao wa usambazaji umeme zimeharibiwa.
- Transfoma 125 za ardhini zimeharibiwa.
- Mita 330,000 za mtandao wa usambazaji wa maji zimeharibiwa.
- Mita 655,000 za mtandao wa maji taka zimeharibiwa.
- Mita 2835,000 za mtandao wa barabara na mitaa zimeharibiwa.
- Majengo 42 na kumbi za michezo zimelengwa na kuharibiwa.
- Visima 717 vya maji vimeharibiwa na havitumiki.
- 88% ya Gaza imeharibiwa kabisa.
- Dola bilioni 37 ni makadirio ya uharibifu wa awali wa moja kwa moja wa mauaji haya makubwa ya kimbari dhidi ya Gaza.