shirika la habari la abna
-
Mwenyekiti wa Baraza la Ulamaa wa Pakistan: Mahali pa mwisho pa mradi wa "Israeli Kubwa" ni Makka na Madina
Mkuu wa Baraza la Ulamaa wa Pakistan alionya kwamba mradi wa "Israeli Kubwa" unatafuta udhibiti wa mwisho juu ya Madina na Makka.
-
Gaza katika moto, dunia katika ukimya; Wanazuoni wa Bahrain wanapiga kelele / wanapaza sauti dhidi ya jinai na ulegevu wa aibu wa nchi za Kiislamu
Huku Ghaza ikipamba moto kutokana na uvamizi wa utawala ghasibu wa Kizayuni, wanazuoni wa Bahrain kwa kauli iliyo wazi wamepongeza kusimama kidete wananchi wa Palestina na kulaani mauaji ya kudumu na kimya cha kutisha cha taasisi za kimataifa na nchi za Kiarabu.
-
Jeshi la Israel linapanga njama ya kuteka 50% ya Ukanda wa Gaza
Jeshi la Israel linapanga kudhibiti asilimia 50 ya Ukanda wa Gaza ikiwa kutakuwa hakuna maendeleo katika mazungumzo ya pande mbili.
-
Kushindwa kwa Marekani nchini Yemen kumezusha wasiwasi miongoni mwa nchi za Kiarabu. Nini kitatokea ikiwa San'a itakuwa Mamlaka yenye Nguvu Kikanda?
Kwa kuzingatia chaguzi ndogo za Amerika, mashaka yameongezeka miongoni mwa maadui wa Yemen katika nchi za Ghuba ya Uajemi, na hii imefanya kazi ya vyombo vyao vya habari - ambavyo vinaendana kikamilifu na (riwaya) simulizi ya Marekani na Israel - kuwa ngumu; Hadi wanakimbilia kuwatuhumu “Ansarullah” kwa kutumia vita vibaya.
-
Ulinganisho kati ya Maisha ya Seminari (Hawza) za Kiislamu na Maisha ya Vyuo Vikuu vya Kisekula (Kidunia).
Watu wengi wanatamani Maisha ya Hawza na wanachukua uamuzi wa kujiunga katika Seminari/ Hawza ili kupata Elimu na Maarifa yenye uwezo mkubwa wa kumuongoza Mwanadamu na hatimaye kuchukua kikamilifu mtindo wa Maisha ya Hawza.
-
Hatua Tano na Muhimu Kabla ya Kuingia Katika Mjadala au Kabla ya Kufanya Mjadala na Mtu yeyote | Bila hatua hizi huo sio Mjadala Bali ni Kupoteza Muda
Kabla hujafanya mjadala wowote na mtu yeyote, unapaswa kuzingatia nukta za kimjadala na muhimu ili uepuke mapema kupoteza muda wako kwa kuingia katika mjadala usiokuwa na matunda yoyote.
-
Mahusiano ya Kijamii ya Kituo cha Utamaduni cha Iran Nchini Tanzania - Dar-es-salaam
Kituo cha Utamaduni cha Iran kipo tayari kutoa Ushirikiano katika nyanja za Utamaduni na Elimu.
-
Al_Itrah Foundation, Dar-es-salaam - Tanzania yampa zawadi ya Tafsiri ya Kiswahili ya Qur'an Tukufu Mwenyekiti wa JMAT - TAIFA Sh.Dr Alhad Mussa Salum
"Kitabu Hicho Hakina Shaka ndani yake, ni Muongozo kwa Wacha Mungu".
-
Samahat Sheikh Kadhim Abbas, Mudir wa Hawza za Bilal Muslim Tanga - Tanzania, amefanya ziara muhimu katika Hawza ya Imam Ali (a.s)
Sheikh Kadhim ametoa akitoa nasaha kwa nasaha kwa Wanafunzi amesema: "Wanafunzi wa Kidini wanapaswa kusoma kwa bidii na kuzingatia masomo yao ili kuhakikisha wanayafikia malengo matukufu ya kuchuma Elimu na Maarifa ya Dini Tukufu ya Kiislamu".
-
Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria yalaani Serikali kwa mauaji ya Waandamanaji 26 wanaounga mkono Palestina, na kuwaweka kizuizini 274
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, matukio kadhaa ya amani ya kidini yaliyoandaliwa na Harakati ya Kiislamu ya Nigeria chini ya uongozi wa Sheikh Zakzaky, likiwemo Kongamano la Mwaka la Mauaji ya Zaria ya mwaka 2015 na programu ya Nisfu / Nusu Sha’ban kwa ajili ya kuadhimisha Maulid ya Imam Mahdi (a.t.f.s), yaliripotiwa kuvurugwa na vikosi vya usalama.
-
Nukta 7 na Muhimu za Tabia Njema, Zilizosheheni Hekima na Busara
"Mwenyezi Mungu ameumba Viumbe Tofauti tofauti, na kila kimoja amekipa sifa zake , Ni Tatizo sana unapo taka Sifa za Kuku awenazo Bata".
-
Umuhimu wa Hijab kwa Mwanamke: Ni kwa nini Hijab ni Wajibu kwa Mwanamke wa Kiislamu?
Katika zama hizi, Hijabu imelinganishwa na kutoendelea kwa jamii na inafikiriwa kuwa ni ishara ya kifungo cha wanawake. Wahubiri wengi wanafikiria kuwa ni bora kutolizungumzia jambo hili katika majlisi zao. Lakini Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Inapotokea Bid’ah na Mwanachuoni asikiseme kile akijuacho (dhidi ya Bid’ah hiyo), basi (Mwanachuoni huyo) hulaaniwa na Mwenyezi Mungu, Malaika na Wanadamu.”
-
Kuchapishwa kwa kitabu cha kwanza kuhusu Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah kwa ajili ya Watoto
Kitabu cha kwanza cha Watoto na Vijana kuhusu Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, kilichoitwa "Baba Hadi" kilichoandikwa na: Elaheh Akherati, kimechapishwa na sasa kinapatikana kwa wale wanaotaka.
-
Maisha Mazuri:
Maisha kwa mtindo wa Wahyi: Je! Qur'an Inatuonyeshaje Njia ya Maisha ya Furaha (Saada)?
Kuelewa mtindo wa maisha katika zama za sasa, ambazo ni zama za Ghaiba, ni swali muhimu. Kwa sababu kazi muhimu ni kuelimisha kizazi kinacholingana na zama za wahyi ili kumsaidia Imamu wa Zama (Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake na faraja yake). Kwa kuzichunguza kwa makini Aya na riwaya, kudhihiri na kuonekana kwa maisha mazuri na hatimaye kufikia maisha sahihi katika kipindi cha kudhihiri, kutadhihirika katika mwanga au kivuli cha elimu na marifa juu ya Hojja wa Mwenyezi Mungu.
-
Ripoti juu ya hali ya hivi punde huko Gaza / Kwa mara ya kwanza katika historia, watu milioni 2 wamezingirwa katika ukanda mmoja (Ukanda wa Gaza)
Katika ripoti ya hivi punde kuhusu hali ya Ukanda wa Gaza, Mwanaharakati wa Kipalestina amesema: "Kwa ujumla, zimepita takriban siku 45 tangu hata kilo 1 ya unga au chupa 1 ya maji iingie Gaza, na mzingiro huo uko katika hali mbaya zaidi."
-
Zaidi ya watu 25 waliouawa Shahidi na wengine kujeruhiwa katika shambulio la Marekani katika eneo la Magharibi mwa Yemen
Idadi ya Mashahidi katika shambulio la jana usiku la Marekani katika Mkoa wa Hodeidah Magharibi mwa Yemen imeongezeka na kufikia watu 10, na zaidi ya watu 16 wameripotiwa kujeruhiwa.
-
Mjumbe wa Jumuiya ya Walimu wa Seminari ya Qom ametembelea Shirika la Habari la ABNA | Ayatollah Faqihi amesisitiza umuhimu wa uaminifu katika Habari
Akiashiria umuhimu wa ukweli na uaminifu katika vyombo vya habari, Ayatollah Faqihi alisema: "Ikiwa tutadumisha ukweli na uaminifu katika uwanja wa taarifa na usambazaji wa habari, basi kwa hakika tunaweza kutoa huduma kubwa katika uwanja huu."
-
Ni kwa namna ipi Sala hukataza maovu?
Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema ndani ya Qur'an Tukufu anasema: (اتْلُ مَا أُوحِيَ إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ وَأَقِمِ الصَّلَاةَ ۖ إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ۗ وَلَذِكْرُ اللَّهِ أَكْبَرُ ۗ وَاللَّهُ يَعْلَمُ مَا تَصْنَعُونَ). "Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumdhukuru Mwenyezi Mungu ndilo jambo kubwa kabisa. Na Mwenyezi Mungu anayajua mnayo yatenda".
-
Mwanaume Mkristo aliyesilimu kwa sababu ya tabia nzuri ya Ali (AS)
Je, Hadhrat Ali (AS) alifanya nini wakati Mwanaume mmoja Mkristo aliposilimu? Kwa heshima ya kusilimu kwake, alimpa ngao yake (inayovaliwa vitani) na kumpa nafasi katika Serikali.
-
Wito wa Maandamano kufuatia Mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni
Kufuatia mashambulio hayo ya kinyama ya utawala wa Kizayuni, Baraza la Uratibu wa Tabligh za Kiislamu limetoa taarifa likiwaalika Wananchi Watukufu wa Tehran kushiriki katika maandamano yatakayofanyika kesho katika Medani ya Palestina.
-
Safari ya Netanyahu kuelekea Marekani imeisha kwa kasi isiyo ya kawaida!
Chombo cha Habari cha Kiebrania kilifichua sababu iliyomfanya Waziri Mkuu wa Israel kuitwa katika Ikulu ya White House kukutana na Rais wa Marekani.
-
Hatua mpya katika kuhalalisha uhusiano wa kawaida; Mkutano kati ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati (UAE ) na utawala haram wa Kizayuni
Waziri wa Mambo ya Nje wa UAE Abdullah Bin Zayed amejadili uhusiano wa pande mbili katika mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kizayuni Gideon Sa'er huko Abu Dhabi. Katika kikao hicho amesisitiza juhudi za kidiplomasia za kufikia usitishaji vita huko Ghaza, lakini mkutano huu ulifanyika katika hali ambayo utawala wa Kizayuni unaendelea kuua na kufanya mauaji ya kimbari huko Ghaza.
-
Katuni | Hakuna njia ya kutokea na kukimbia huko Gaza
Watoto wa Kipalestina wanatamani sana Msaada kutoka kwa Mashirika ya Kimataifa.
-
Je, Makaburi ya Baqii yalizingirwa na kuharibiwa (kubomolewa) na kina nani? | Matukio yalivyotendwa katika uharibifu wa Baqii
Mnamo mwaka wa 1220 A.H., Mawahabi waliutwaa mji huo baada ya kuzingirwa kwa mwaka mmoja na nusu na kwa sababu ya njaa huko Madina. [25] Kulingana na vyanzo vilivyopo, baada ya kujisalimisha kwa Madina, Saud bin Abdul Aziz alitaifisha mali yote iliyokuwa kwenye hazina ya Madhabahu ya Mtume na pia akaamuru kuharibiwa kwa majengo na majumba yote ya Madina, pamoja na makaburi ya Baqi.[26]
-
Netanyahu amesafiri njia ndefu kutoka Budapest hadi Washington ili kukwepa kukamatwa
Vyombo vya habari vya Israel vimetangaza leo kwamba kutokana na hati ya kukamatwa iliyotolewa dhidi ya Waziri Mkuu wa utawala huu, ndege iliyombeba ilibidi ichukue njia ndefu zaidi kuelekea Washington.
-
Mwenyekiti wa Bunge la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
Kila siku huko Gaza ni Apocalypse (Zama za Mwisho / Mwsiho wa Dunia) / Ukimya wa watawala wa Kiarabu unatia uchungu zaidi kuliko uhalifu (jinai)
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan amesema: "Tukio chungu zaidi si tukio la uhalifu unaofanyika dhidi ya Gaza, bali ni kile kimya kinachojiri katika Kasri za watawala wa Kiislamu na Kiarabu." Lugha zilizokuwa zikizungumza kutetea Uislamu sasa hivi zinalamba nyayo za madola ya kibeberu.
-
Jinsi ya kuthibitisha Isma ya Maimamu 9 (a.s) kutoka ndani ya Qur’an Tukufu
“Na (Kumbukeni) Ibrahim alipojaribiwa na Mola wake kwa matamko, naye akayatimiza. Akasema: Hakika mimi nitakufanya kuwa Imam wa watu. Ibrahim akasema: Je,na Kizazi changu (pia)?.(Ndiyo, lakini) ahadi yangu haiwafikii Madhalimu.”
-
Umuhimu wa Qur'an Tukufu katika Maisha yetu kama Wanadamu
Kila Aya katika Aya za Qur’an ni chimbuko la mwangaza, muongozo na rahma, kwa hiyo mwenye kutaka mafanikio ya milele na kuokoka katika dunia yake, basi ni juu yake kushikamana na kitabu cha Mwenyeezi Mungu (s.w) usiku na mchana na kuzifanya Aya za Qur’an Tukufu kuwa mfano katika kumbukumbu zake na kituo cha fikra zake ili awe katika mwangaza wa Mwenyeezi Mungu (s.w).
-
Majukumu ya Mwalimu na Mwanafunzi:
Majukumu ya Mwanafunzi yamegawanyika katika sehemu kuu tatu (2)
Amesema Mtume (s.a.w.w): “Mfano wa anaye jifunza akiwa mdogo ni kama Anaye nakishi (anaye chora) katika jiwe, na anaye jifunza ukubwani ni kama na anayeandika katika maji”. Japokuwa kutafuta elimu ni vizuri na muhimu katika umri wote, lakini ukiwa katika umri mdogo ndio vizuri zaidi.
-
Historia | Tarehe 8 Shawwal 1345 Hijria, Mawahhabi walibomoa na kuyanajisi Makaburi ya Ahlu Bayt wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) katika Mji wa Madina
Historia inaonyesha kuwa, katika tukio hilo la kusikitisha, lililotokea tarehe 8 Mfunguo Mosi Shawwal 1345 Hijria (1925 Miladia) Mawahabi wa Saudi Arabia walibomoa makaburi ya Ahlul-Bayt -a.s- wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ambayo yanapatikana katika ardhi ya Baqi’i, katika Mji Mtakatifu wa Madina.