Askari wa jeshi la Israel na walowezi wa kizayuni kila siku wanawaua au kuwajeruhi na kuwaweka kizuizini kwa visingizio tofauti wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina. Kwa mujibu wa ripoti Jumuiya ya kushughulikia mateka wa Kipalestina Wapalestina 12 walikamatwa katika Ukingo wa Magharibi katika muda wa saa 24 zilizopita. Tangu tarehe 7 Oktoba 2023, utawala ghasibu wa Kizayuni ulianzisha mauaji makubwa ya kimbari katika Ukanda wa Ghaza dhidi ya watu wasio na ulinzi na madhulumu wa Palestina kwa uungaji mkono kamili wa nchi za Magharibi.Kimya cha jamii ya kimataifa na taasisi za haki za binadamu kwa jinai za utawala ghasibu wa Israel, kimesababisha kuendelea kuuawa wanawake na watoto wa Kipalestina katika vita vya kinyama vilivyoanzishwa na utawala huo haramu.
342/