Utiaji nguvuni wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Texas huko Austin (UT Austin) umetokea jana wakati Chuo Kikuu cha Columbia jimboni New York City kimeanza kuwasimamisha masomo wanafunzi baada ya kukaidi amri ya kutawanyika. Wanachuo wanaoandamana na kukusanyika kwenye kampasi za vyuo vikuu vyao wanautaka uongozi wa vyuo ukate uhusiano na Israel, ambayo baadhi ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanasema inafanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Ghaza, ambako hadi sasa Wapalestina wasiopungua 34,488 wameshauawa shahidi.Maandamano hayo yamesambaa na kupamba moto katika vyuo vikuu kote nchini Marekani, huku idadi ya waliokamatwa ikikaribia 1,000 wakati siku za mwisho za masomo zikikaribia kumalizika.
342/