Main Title

source : Parstoday
Ijumaa

3 Mei 2024

14:09:00
1455920

Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Operesheni ya Ahadi ya Kweli iliyonyesha uwezo wa kijeshi wa Iran

Imamu wa muda Swala ya Ijumaa mjini Tehran amesema: Iran ilionyesha uwezo wake wa usimamizi wa masuala ya kijeshi katika operesheni pana na ya kiwango cha juu zaidi ya ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya utawala wa Kizayui wa Israel.

Hujjatul Islam Muhammad Hassan Abu Turabifard khatibu wa Swala ya ya Ijumaa ya wiki hii mjini Tehran ameashiria operesheni hiyo iliyopewa jina la "Ahadi ya Kweli" na kusema: Katika operesheni hiyo, Iran ilionyesha sehemu ya uwezo wake wa usimamizi wa masuala ya kijeshi  na kuongeza kwamba, hii leo mafanikio ya operesheni hiyo ya ushindi yanapaswa kubainishwa.

Hujjatul Islam Muhammad Hassan Abu Turabifard ameendelea kusema kuwa Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kwamba operesheni hii ingeweza kuwa zaidi ya ilivyokuwa, lakini ilipunguzwa ili kuenda sambamba na ukhabiti wa adui.

Khatibu wa Swala ya Ijumaa wiki hii mjini Tehran ameendelea kusema: 'Kwa mtazamo wa maadui, "Operesheni ya Ahadi ya Kweli" ilikuwa pana sana na imekuwa mwanzo wa mabadiliko ya mligano wa nguvu kieneo."Ikumbukwe kuwa, Jumatatu, Aprili 1, 2024, utawala wa Kizayuni wa Israel ulishambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus katika shambulio la kigaidi lililopelekea kuuawa shahidi washauri saba wakuu wa kijeshi wa Iran.

Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Iran aliitaja hatua hiyo ya Israel kuwa ni shambulio dhidi ya ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kusisitiza kuwa, utawala wa Kizayuni "utaadhibiwa".
Katika kutekeleza ahadi hiyo, Jumapili asubuhi (tarehe 14 Aprili 2024), Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu lilichukua hatua ya kuuadhibu utawala huo wa Kizayuni kwa kuvurumisha ndege zisizo na rubani na makombora kuelekea ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) kupitia operesheni ya kuiadhibu Israel iliyopewa jina la "Ahadi ya Kweli."


342/