Main Title

source : Parstoday
Jumatatu

6 Mei 2024

16:31:11
1456597

Seneta wa Marekani: Wanafunzi wanaopinga vita vya Ghaza wamesimama upande sahihi wa historia

Bernie Sanders, Seneta wa kujitegemea anayewakilisha jimbo la Vermont nchini Marekani amewasifu wanafunzi wa vyuo vikuu vya nchi hiyo wanaopinga vita katika Ukanda wa Ghaza na kusema, wanafunzi hao wamesimama upande sahihi wa historia.

Sanders ameyasema hayo katika ujumbe alioandika kwenye mtandao wa kijamii wa X na kueleza kwamba, kuwaunga mkono watu wa Ghaza na kupinga sera za utawala wa Rais wa Marekani Joe Biden za kuuunga mkono kwa kila hali utawala wa Israel, mara hii kumeanzia kwenye matabaka tofauti ya wanafunzi katika vyuo vikuu vya Marekani. Zaidi ya watu 2,000 wametiwa mbaroni hadi sasa tangu yalipoanza maandamano ya kupinga vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza, maandamano ambayo yanafanyika kwa anuani ya "Vuguvugu la Mshikamano na Ghaza", yaliyoanzia katika Chuo Kikuu cha Columbia mjini New York na kuenea kwenye vyuo vingine vya Marekani.Maandamano hayo ya upinzani yameibuka kutokana uungaji mkono wa kila hali unaoonyeshwa na serikali ya Biden kwa Israel na mauaji ya mtawalia yanayoendelea kufanywa na jeshi la utawala huo dhidi ya Wapalestina wa Ghaza.

Utawala wa Kizayuni ulianzisha vita vya kinyama dhidi ya Ghaza kama hatua ya kulipiza kisasi baada ya kushindwa katika operesheni ya kushtukiza ya Kimbunga cha Al-Aqsa ya tarehe 7 Oktoba 2023 iliyotekelezwa na makundi ya Muqawama wa Palestina ya Ghaza. Tangu utawala huo ghasibu ulipoanzisha hujuma na uvamizi huo wa kijeshi dhidi ya Ghaza mnamo Oktoba 7, 2023, hadi sasa Wapalestina 34,654 wameuawa shahidi na wengine 77,908 wamejeruhiwa.../

342/