Main Title

source : ABNA
Jumanne

7 Januari 2020

07:26:41
1000118

Zikiwa ni siku mbili tu toka Rais wa Marekani kutangaza vikwazo dhidi ya Iraq, hatimaye kiongozi wa mrengo wa Sadr nchini Iraq a

Kupitia ujumbe aliouweka katika ukurasa wake wa Twitter, Sayyid Muqtada Muhammad Sadr, amesema kuwa Trump asidhani kwamba ataweza kuwatishia wa Iraq kwa njaa na vikwazo.

Shirika la habari AhlulByt (a.s) ABNA: Kama ambavyo katika ujumbe huo ameashiria kwa ukali mno baadhi ya sifa ambazo kiongozi huyo wa Marekani anasifika nazo kama vile dhulma, mabavu na nyinginezo, huku akiashiria kwamba hivyo havitamsaidia pindi atakapoamua kuviwekeza tena nchini Iraq.

“...Kumbuka kwamba nyumba yako ni dhaifu kuliko hata ya buibui, na sauti yako yenye kututisha ni yenye kukera zaidi ya sauti ya punda...” aliandika Sadr.

Haya yamekuja baada ya Rais wa Marekani Bw Donald Trump kutishia kuiwekea vikwazo Iraq ikiwa tu itafanyia kazi mswada wake wa kuyatoa kinguvu majeshi ya Marekani nchini humo.

mwisho/290