-
serviceIRGC yadai kuharibu miundombinu ya mawasiliano ya kambi ya Marekani na gati la kijeshi nchini Kuwait
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limedai kuharibu kituo cha mawasiliano ya satelaiti, rada za tahadhari ya mapema katika Kambi ya Anga ya Ali Al Salem pamoja na gati linalotumiwa…
Habari za hivi punde
-
serviceIRGC yadai kuharibu miundombinu ya mawasiliano ya kambi ya Marekani na gati la kijeshi nchini Kuwait
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limedai kuharibu kituo cha mawasiliano ya satelaiti, rada za tahadhari ya mapema katika Kambi ya Anga ya Ali Al Salem pamoja na gati linalotumiwa na wanajeshi wa Marekani katika Bandari ya Shuaiba, Kuwait.
-
serviceMakao Makuu ya Khatam al-Anbiya yaionya Marekani: Mkishambulia miundombinu ya Iran, tutaharibu iliyosalia katika eneo
Msemaji wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s) amesema Iran haitaruhusu Marekani kuingilia Mlango wa Hormuz na ameonya kuwa endapo miundombinu ya Iran itashambuliwa, Vikosi vya Ulinzi vya Iran vitajibu kwa mashambulizi makubwa dhidi ya miundombinu iliyosalia katika eneo.
-
serviceChuo cha Kimataifa cha Al-Mustafa (s) Dar es Salaam Chaendelea Kuimarisha Elimu ya Qur'an Tukufu +Picha
Darasa la mafunzo ya Qur'an Tukufu limeendelea katika Chuo cha Kimataifa cha Al-Mustafa (s) Jijini Dar es Salaam, Tanzania likiongozwa na Al-Haj Sheikh Muhammad Ja'far huku usomaji wa Qur'an ukifanywa na Sheikh Khamis Mpili.
-
serviceKamanda wa Walinzi wa Mipaka wa Iran awasili Pakistan kwa mkutano wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai
Kamanda wa Vikosi vya Walinzi wa Mipaka wa Iran, Brigedia Jenerali Ali Akbar Javidan, amewasili Islamabad kushiriki mkutano wa makamanda wa walinzi wa mipaka wa nchi wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai (SCO).
-
serviceAfisa wa Iraq: Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliwakilisha shule ya Jihadi, elimu, msimamo na kujitolea
Mkuu wa Ofisi ya Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq mjini Tehran, Majid Al-Ghammas, amesema Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliwakilisha shule ya jihadi, elimu, uwajibikaji, uthabiti na kujitolea, akisisitiza kuwa maisha yake yamekuwa mfano kwa vizazi vijavyo.
-
serviceYemen yatangaza kurejesha safari za ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sana'a, yasema imevunja mzingiro
Mamlaka za Yemen zimetangaza kuwa ndege ya Iran itarejea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sana'a na safari za kila siku zitaanza tena, zikisisitiza kuwa zimeamua kuvunja mzingiro na kwamba hakuna nchi itakayozuia haki yao ya kutumia uwanja huo wa ndege.
-
serviceJeshi la Yemen ladai kuidungua droni ya kivita ya Saudi Arabia katika anga la Al-Baydah
Jeshi la Yemen limedai kuwa limedungua ndege isiyo na rubani ya kivita aina ya Wing Loong-2 UCAV inayodaiwa kumilikiwa na Jeshi la Anga la Saudi Arabia katika anga la mkoa wa Al-Baydah nchini Yemen.
-
serviceMarekani yaiondoa ndege yake ya upelelezi MQ-4C Triton kutoka Jordan kuelekea Italia baada ya mashambulizi ya Iran
Ripoti zinaeleza kuwa Marekani imeiondoa ndege yake ya kisasa ya upelelezi aina ya MQ-4C Triton kutoka Jordan na kuihamishia Italia, hatua inayokuja baada ya mashambulizi ya Iran dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
serviceWanazuoni wa Bahrain Wataka Kuachiliwa Mara moja kwa Wanazuoni wa Dini Waliokamatwa
Wanazuoni wa Bahrain wametoa wito wa kuachiliwa mara moja na bila masharti kwa wanazuoni wa dini waliokamatwa, wakiiwajibisha serikali ya Bahrain kwa madhara yoyote ya kimwili au kisaikolojia yatakayowapata wakiwa mahabusu.
-
serviceKiongozi wa Wanazuoni wa Imamiyya Pakistan: Vikwazo kwa Mazuwwari wa Arubaini ni Sehemu ya Mardi wa Kuwadhoofisha Mashia
Kiongozi wa Baraza la Wanazuoni wa Imamiyya Pakistan, Hujjatul Islam Dkt. Sayyid Shafaqat Hussein Shirazi, amesema vikwazo vinavyowakabili mahujaji wa Pakistan kuelekea Arubaini si suala la kiusalama pekee, bali ni sehemu ya mpango wa kudhoofisha uhusiano wa wafuasi wa Ahlul-Bayt (as) na Iran, Iraq pamoja na utamaduni wa A'shura.