Afrika imehusika kidogo mno na uchafu wa mazingira, lakini ndiyo inayoathirika zaidi duniani
Uchunguzi mpya uliofanywa na Mo Ibrahim unaonesha kuwa, nchi zote za bara la Afrika, zimechangia kwa asilimia 3.3 tu ya uzalishaji wa gesi chafu na uchafuzi wa mazingira duniani tangu mwaka 1960, lakini pamoja na hayo, nchi za bara hilo ndizo zinazoathiriwa zaidi mabadiliko ya tabianchi.