-
serviceBaada ya Malalamiko ya Taasisi ya Mashia wa Marekani, Mjumbe wa Bodi ya Elimu ya Baltimore Aomba Msamaha
Taasisi ya Waislamu Mashia wa Marekani, ikisisitiza athari za kauli za maafisa wa elimu kwa wanafunzi Waislamu, ilitangaza kwamba kuomba msamaha kwa mjumbe wa Bodi ya Elimu ya Baltimore pekee…
Habari za hivi punde
-
servicePalestina; Kipimo cha Kupima Uaminifu wa Umoja wa Kiislamu
Mkurugenzi Mkuu wa Uenezi wa Kiislamu wa Fars amesema: Ikiwa Umma wa Kiislamu hautaweza kuwa “mkono mmoja” katika suala la Palestina, basi kuzungumzia umoja kutabaki katika kiwango cha dhana ya kiitifaki tu. Umoja wa kweli hupata maana pale ambapo Waislamu wanapoona maslahi yao ya pamoja na hatima yao ya pamoja mbele ya dhulma na uchokozi.
-
special-issueWanafunzi wa Kishia Kabul: Kwa Miezi Miwili Sasa Milango ya Msikiti na Shule Yetu Imefungwa
Wanafunzi wa Chuo cha Kidini cha Khatam al-Nabiyyin (s) mjini Kabul, wakipinga kuendelea kufungwa kwa sehemu kuu za kituo hiki, wamemwambia mwakilishi wa Wizara ya Sheria ya Taliban kwamba kwa karibu miezi miwili sasa wamelazimika kusoma katika maeneo ya wazi, na wameuliza: “Dhambi yetu ni ipi? Je, Mashia hawana haki ya kuwa na Msikiti na shule?”
-
special-issueKwa nini Hizbullah ya Lebanon ilikataa kukabidhi maeneo ya miinuko ya Ali al-Taher?
Pendekezo ambalo kwa msingi wake Hizbullah ingeyaondoa majeshi yake katika maeneo ya miinuko ya Ali al-Taher na Jeshi la Lebanon kuchukua nafasi yake, kwa mtazamo wa Hizbullah si mpangilio wa kijeshi wa uwanjani tu, bali linaweza kuunda mfano wa kulazimisha madai zaidi ya utawala wa Kizayuni katika maeneo mengine ya Lebanon.
-
serviceBaada ya Malalamiko ya Taasisi ya Mashia wa Marekani, Mjumbe wa Bodi ya Elimu ya Baltimore Aomba Msamaha
Taasisi ya Waislamu Mashia wa Marekani, ikisisitiza athari za kauli za maafisa wa elimu kwa wanafunzi Waislamu, ilitangaza kwamba kuomba msamaha kwa mjumbe wa Bodi ya Elimu ya Baltimore pekee hakuwezi kurekebisha madhara na ukosefu wa imani uliosababishwa baada ya kuchapishwa kwa ujumbe wenye chuki dhidi ya Uislamu.
-
serviceMashambulizi ya Jeshi la Kigaidi la Marekani dhidi ya Maeneo ya Kusini mwa Nchi ya Iran
CENTCOM imetangaza: Vikosi vya Marekani leo saa 12:00 mchana kwa saa za Mashariki mwa Marekani vilianza mashambulizi dhidi ya malengo ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) nchini Iran.
-
serviceMpango Mpya wa Jimbo la Tamil Nadu, India, wa Kurahisisha Masomo ya Vyuo Vikuu kwa Wanawake Waislamu
Serikali ya Jimbo la Tamil Nadu nchini India imetangaza kwamba italipia ada za masomo ya chuo kikuu kwa wanawake Waislamu wanaokidhi vigezo.
-
serviceUpole na Huruma ya Mtume Muhammad (saww); Siri ya Kuenea kwa Uislamu
Mtume Muhammad (saww), kupitia tabia yake njema na tukufu, huruma yake isiyo na mipaka, pamoja na subira na uvumilivu wake dhidi ya matendo mabaya aliyofanyiwa, aliwabadilisha maadui wakubwa kuwa marafiki waaminifu. Maadili haya matukufu, ambayo Mwenyezi Mungu ameyasifu kupitia aya: “Na hakika wewe una tabia tukufu kabisa” na “Kwa sababu ya rehema kutoka kwa Mwenyezi Mungu umekuwa mpole kwao”, yalikuwa siri kuu ya kuenea kwa Uislamu duniani. Msamaha wa jumla wakati wa Ushindi wa Makka, kuwatendea mateka kwa heshima na kuwafanyia mema, kuheshimu utu wa mwanadamu hata katika kilele cha uadui, unyenyekevu na maisha ya kawaida licha ya cheo chake cha juu cha Utume, pamoja na huruma yake kwa watoto na wanyonge, vilikuwa miongoni mwa ukamilifu wa maadili yake yaliyotekwa nyoyo za watu na kuvunja safu za wapinzani. Mwenendo huu wa Mtume (saww), uliojaa rehema na huruma na ambao ulikuwa udhihirisho kamili wa “rehema kwa walimwengu”, haukusababisha tu makundi makubwa ya watu kusilimu katika zama za mwanzo za Uislamu, bali utaendelea milele kuwa mfano wa kudumu wa kuwaalika watu kwenye haki na kuangaza njia ya watafuta ukweli.
-
serviceNoor Centre Dar es Salaam Yaandaa Kikao Maalum cha Kujadili Utume wa Mtume (saw) Katika Dunia ya Kisasa
Sheikh Ali Asad Esmail aongoza kikao maalum cha “Utume wa Mtume (saww) Katika Dunia ya Kisasa” kilichoandaliwa na Noor Centre Dar es Salaam, Tanzania.
-
serviceT.I.C Yaandaa Zafa la Maulidi ya Mtume Muhammad (saww) Kigogo Post: “Amani, Upendo na Huruma Ndiyo Mafunzo ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)” +Picha
Jumuiya ya Shia Ithna'ashariyyah Tanzania (T.I.C) imeandaa zafa maalumu ya kusherehekea Maulidi ya Mtume Muhammad (saww), iliyofanyika tarehe 30 Agosti 2026 katika eneo la Kigogo Post, Dar es Salaam, chini ya kaulimbiu ya “Amani, Upendo na Huruma” ikiwa ni miongoni mwa mafundisho muhimu ya Mtume Muhammad (saww).
-
serviceTaliban yakosoa kuondolewa kwa Afghanistan katika mkutano wa Shanghai
Zabihullah Mujahid amesema kuwa maamuzi ya kikanda ya Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai bila ushiriki wa Afghanistan yatakuwa “hayajakamilika”; wakati huohuo, viongozi wa jumuiya hiyo katika mkutano wa Bishkek kwa mara nyingine wamesema kuwa kuundwa kwa serikali jumuishi nchini Afghanistan ni sharti la kufikiwa kwa amani na utulivu wa kudumu.