Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la habari la ABNA, polisi ya utawala wa Kizayuni ilitangaza kwamba mmoja wa wanajeshi wa utawala huu ameuawa kwa mkono wa mwanajeshi mwingine.
Kulingana na ripoti hii, polisi ya utawala wa Kizayuni iliongeza kuwa mwanajeshi huyo aliuawa kutokana na kupigwa risasi ya makosa kichwani mwake.
Siku chache zilizopita, jeshi la utawala wa Kizayuni pia liliripoti kuuawa kwa mmoja wa wanajeshi wa kijasusi wa utawala huu, aliyehusishwa na vikosi vya wanajeshi wa kuruka kwa miamvuli (paratroopers), kwa risasi za wanajeshi wengine wa Kizayuni huko Khan Yunis iliyoko kusini mwa Ukanda wa Gaza.
Redio ya jeshi la utawala wa Kizayuni pia iliripoti kwamba, inaonekana wanajeshi wa Israel walifyatua risasi katika maeneo yanayoitwa mstari wa njano kwa walengwa wawili wanaohusishwa na kikosi cha paratroopers ambao walikuwa wakitekeleza misheni katika eneo hilo.
Mwanajeshi huyu wa Kizayuni baada ya kujeruhiwa vibaya kabisa alifariki kabla ya kufikishwa hospitalini.
Hii si mara ya kwanza kwa wanajeshi wa Kizayuni kufyatuliana risasi wakati wa vita vya Gaza.
Polisi ya utawala wa Kizayuni imeripoti kuuawa kwa mwanajeshi mwingine wa utawala huu kwa risasi ya makosa.
Your Comment