-
Maandalizi na uhamasishaji wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan 2025 / 1446H - Hawzat Imam Ali (as) Tanga - Tanzania
Hawzat Imam Ali (a.s) iliyopo chini ya Taasisi ya Bilal Muslim Mission Tanga, Tanzania, Kitengo cha uhamasishaji wa Michango ya uwezeshaji wa masira ya Imam Husein (a.s), Leo hii Jumatatu 21/04/2025, kimekutana na Waumini wa Bilal Muslim Bushiri na kuongea nao kuhusiana na Suala la Masira ya Imam Hussein (as) mwaka huu wa 1446H. Lengo la ziara hii, ni kuhamasishana zaidi na kuelezea umuhimu wa kutoa Sadaka hasa katika kuichangia Masira ya Imam Husen (a.s).
-
Viongozi wa JMAT ngazi ya Taifa Arusha-Tanzania, wakutana na Katibu Mkuu wa JMAT-TAIFA, Dr. Maasa Ole Gabriel na Naibu wake Sh.Dr. Abdur -Razak Amir
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Mh. Dr. Maasa Ole Gabriel, pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa JMAT-TAIFA, Samahat Sheikh Dr. Abdur - Razak Amiri wamewakutanisha viongozi wote wa ngazi za juu waliopo katika Jiji la Arusha, ambapo wamekaa pamoja na kujadili masuala mbalimbali na muhimu katika Muktadha wa Maridhiano na Amani ya Taifa letu la Tanzania.
-
Mufti wa Burundi wa Madhehebu ya Ahlu-Sunna, Mh.Sheikh Ndikumagenge Masudi amtembelea Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithna Ashari TIC Sheikh H. Jalala
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Mufti Mkuu wa Burundi wa Madhehebu ya Ahlu-Sunna, Sheikh Ndikumagenge Masudi akiambatana na Mwenyekiti wake na watendaji wa Ofisi yake katika Ziara yake Nchini Tanzania, alipata fursa ya kumtembelea Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Tanzania (T.I.C), Maulana Sheikh Hemed Jalala na kubadilishana fikra na mawazo katika suala muhimu la kuutumikia Uislamu na Waislamu.
-
Kikao maalum kati ya Mkuu wa Jamiat Al-Mustafa (s) - Tanzania, Dr. Ali Taqavi na Mh.Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Kikao maalum kati ya Mkuu wa Jamiat Al-Mustafa (s) - Tanzania, Dr. Ali Taqavi na Mh.Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi. Katika Kikao Rais wa Jamiat Al-Mustafa (s) - Dares-Salam - Tanzania amejadiliana na Mheshimiwa Mufti Mkuu wa Zanzibar kuhusiana upanuzi wa Chuo cha Qur'an Tukufu ndani ya Zanzibar, kuhudhuria kwa wasomaji mahiri wa Qur'an Tukufu wa Zanzibar katika Tamasha la Qur'an Tukufu, pamoja na maandalizi na upangaji ratiba muhimu kuhusiana na Tamasha hilo la Qur'an Tukufu litakalofanyika nchini Tanzania hivi karibuni. Katika Kikao hiki Dr. Ali Taqavi aliambatana pia na Sheikh Dr. Alhad Musa Salum, Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA.
-
Habari Pichani | Ziara ya Dr.Ali Taqavi katika Chuo cha Qur'an Tukufu cha Jamiat al-Mustafa (s) - Zanzibar - Tanzania
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Hojjat al-Islam wal-Muslimin Dr.Ali Taqavi afanya Ziara muhimu katika Chuo cha Qur'an Tukufu Zanzibar - Tanzania akiambata na Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum, Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA.
-
Habari Pichani | Sherehe ya Kipekee ya Kufikia Umri wa Dini (Taklif) kwa Wasichana wa Karbala
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AhlulBayt (a.s) – ABNA – Sherehe ya bulugh kwa wasichana imefanyika kwa adhama katika mji mtakatifu wa Karbala, Iraq. Takribani wasichana 5,000 kutoka shule 121 walishiriki kwenye hafla hiyo iliyoandaliwa na Ataba ya Abbasiyya. Tukio hilo lililenga kuwapa wasichana hawa utambuzi wa kidini na kuadhimisha hatua muhimu ya kuingia katika umri wa kuwajibika kwa mujibu wa sheria ya Kiislamu. Sherehe hiyo imekuwa tukio lenye mvuto mkubwa, likiambatana na hotuba, mawaidha na maombi, na kuwapa washiriki fursa ya kuimarisha uhusiano wao na mafundisho ya AhlulBayt (a.s).
-
Qur'an Tukufu Zanzibar - Tanzania + Video
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Sheikh Ridha Dosa akitoa Somo la Qur'an Tukufu Zanzibar - Tanzania, katika Chuo cha Qur'an Tukufu cha Jamiat Al- Mustafa (s) kinachoongozwa na kusimamiwa na Rais wa Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-salaam - Tanzania, Hojjat al-Islam wal Muslimin, Dr.Ali Taqavi.
-
Ujue wajibu wako katika kuiongoza familia yako + Video
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Samahat Sheikh Reihan Yasin, akifafanua mada Muhimu kuhusu mtu kuujua Wajibu wake katika kuiongoza familia yake.
-
Putin aidhinisha Makubaliano ya kina ya kimkakati na Iran
Mkataba huo unalenga kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili katika maeneo yote yenye maslahi ya pamoja.
-
Papa Francis afariki dunia akiwa na umri wa miaka 88
Papa Francis, kiongozi wa Kanisa Katoliki, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 88, katika makazi yake ya Casa Santa Marta, ndani ya jiji la Vatikan.
-
Hilali Nyekundu ya Palestina: Ripoti ya Israel ya mauaji ya wahudumu wa tiba 'imejaa uwongo'
Shirika la Hilali Nyekundu la Palestina limekanusha vikali ripoti ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu mauaji liliyofanya mwezi uliopita ya zaidi ya wafanyakazi 15 wahudumu wa sekta ya tiba huko Ghaza, ambayo utawala huo umedai waliuawa kimakosa.
-
Shambulio la anga la Marekani katika mji mkuu wa Yemen laua raia wasiopungua 12, lajeruhi 30
Marekani imefanya mashambulizi mengine ya anga dhidi ya mji mkuu wa Yemen, Sana’a na kuwaua shahidi raia wasiopungua 12 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 30.
-
Mkuu wa Umoja wa Maulamaa wa Muqawama: Kuitetea Ghaza ni jukumu la Waislamu wote
Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Muqawama amesema, kuitetea na kuiunga mkono Ghaza ni jukumu la watu wote, na akatoa wito kwa mataifa ya Kiislamu na wanazuoni wa Kiislamu kuwasaidia ndugu zao wanaodhulumiwa huko Palestina na katika Ukanda wa Ghaza, wakati huu ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel unaendeleza jinai zake dhidi yao.
-
Iran yafungua Maonyesho ya Kaligrafia ya Qur'ani Jeddah
Maonyesho ya Kaligrafia ya Qur'ani na Mashairi ya Kiarabu, yaliyoandaliwa na Ubalozi Mdogo wa Iran mjini Jeddah, yamefunguliwa rasmi katika mji huo wa bandari wa Saudi Arabia.
-
Vikosi vya Yemen vyashambulia Israel na meli za kivita za Marekani
Vikosi vya Jeshi la Yemen vimeendesha msururu wa operesheni kulipiza kisasi kutokana na mashambulizi yanayoendelea ya Marekani katika nchi hiyo ya Kiarabu, vikishambulia ngome muhimu za Isarel katika ardhi zinazikaliwa kwa mabavu pamoja na meli za kivita za Marekani katika Bahari Nyekundu ya Kaskazini na Bahari ya Arabia.
-
IRGC kuzindua manowari mpya kama za US, au bora zaidi
Kamanda wa Kikosi cha Majini cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Admeli Alireza Tangsiri amesema yumkini SEPAH ikazindua manowari mpya ambazo muundo wake unashabihiana au utakuwa bora zaidi kuliko wa Marekani.
-
Araghchi: Wamarekani hawakuzungumzia suala jengine ghairi ya kadhia ya nyuklia
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuhusu mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana yanayofanyika kati ya Iran na Marekani kwa kusema: "mazungumzo yetu yanahusu masuala ya nyuklia na hatutakubali maudhui nyingine yoyote".
-
Mipango na malengo makubwa ya Iran kwa ajili ya kushirikiana na nchi za Kiafrika
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeratibu mipango na kuainisha malengo yake kwa ajili ya ushirikiano wa kisiasa na kiuchumi na bara la Afrika.
-
Mufti wa Al-Quds aonya kuhusu nakala zisizoidhinishwa za Qur'ani
Mufti Mkuu wa al-Quds na Maeneo ya Palestina ametoa wito wa kukusanywa kwa nakala za Qur'ani ambazo hazijaidhinishwa rasmi.
-
Mkuu wa IAEA asema ana mtazamo chanya kwa mazungumzo ya nyuklia ya Iran na Marekani
Rafel Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki, IAEA amesema katika mahojiano na gazeti la Italia la Repubblica kwamba ana matumaini kuhusu mazungumzo ya nyuklia yanayoendelea kati ya Iran na Marekani.
-
-
-
Iran yasema Afrika itakuwa kitovu cha uchumi wa dunia
Msemaji wa Serikali Iran amesema Mkutano wa Tatu wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika utafanyika wiki ijayo sambamba na Maonyesho ya Saba ya Uwezo wa Biashara ya Nje ya Iran.
-
Kiongozi wa Wakatoliki Papa Francis aaga dunia akiwa na umri wa miaka 88
Papa Francis, kiongozi wa Kanisa Katoliki, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 88, katika makazi yake ya Casa Santa Marta, ndani ya jiji la Vatikan.
-
Habari Pichani | Darsa za Tafsiri ya Qur'an Tukufu, Hawzat Imam Ali (a.s) - Zanzibar
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Hawzat Imam Ali (a.s) Zanzibar, ikiendelea na Darsa za Tafsiri ya Qur'an Tukufu. Darsa hizi zinaendelea kila siku ya Jumatatu.
-
Mazungumzo yasokuwa ya moja kwa moja ya Iran na Marekani
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Mazungumzo yasokuwa ya moja kwa moja ya Iran na Marekani.
-
Habari Pichani | Taasisi ya Furqan Foundation itoa msaada kwa ndugu Jafar wa Zaizo Lushoto - Tanga ambaye ni mgonjwa wa viungo
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) - ABNA - Taasisi ya Furqan Foundation imefanikiwa kutoa chakula, mafuta, mchele na shuka za kujifunika kwa ndugu yetu Jafar wa Zaizo Lushoto, Tanga - Tanzania. Huyu ni mgonjwa wa viungo. Familia yake wamefurahi sana na wanawaombea dua njema wafadhili kwa kitendo chao hiki kizuri cha upendo na huruma kwa mtoto wao.
-
Picha za mwisho za Papa Francis kabla ya kifo chake
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul Bayt (a.s) - ABNA -, Papa Francis alishiriki ibada ya jana ya Pasaka, na picha za uwepo wake kwenye sherehe hizo zilichapishwa. Kiongozi wa Wakatoliki duniani amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 88.
-
Palestina lazima ibaki / Watawala wetu wamepotoka kutoka kwenye Misingi ya Umma wa Kiislamu
Mwenyekiti wa Majlisi ya Umoja wa Waislamu wa Pakistan akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuiunga mkono Palestina amesema kuwa, watawala na wanasiasa wa sasa wa nchi hiyo wamejitenga na thamani halisi za Umma wa Kiislamu.
-
Watu waliodhaifu kwako unawatendea vipi? Uislamu unasisitiza kuwatendea watu wema
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as.) - ABNA - Samahat Sheikh Hemed Jalala, Mudir wa Hawzat Imam Sadiuq (a.s) - Kigogo - Post na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithna Ashari Tanzania (T.I.C), amekumbusha umma wa waislamu kuzingatia kuwatendea wema watu hasa wale waliodhaifu, na kuhakikisha kwamba hakuna mtu yeyote anayedhulumiwa na kutendewa ndivyo sivyo. Uislamu unalingania wema na haki kwa watu. Katika maneno yake mafupi na yenye hekima, amesema: "Ukitaka kujua ukweli wa mtu, basi tizama ni jinsi gani anavyowatendea wale waliodhaifu kwake"