-
Ufafanuzi wa Kina na Maridhawa Juu ya Suala la Unabii Baina ya Waislamu na Wakristo
Sheikh Dk.Alhad Mussa Salum: "Wakristo wanaposema, au tunaposikia ikisemwa, au anapoitwa mtu kuwa ni Nabii au Nabii Mkuu, anaitwa hivyo kwa Istilahi ipi?! Hili ndio swali la msingi kujiuliza?. Anaitwa hivyo kwa Istilahi yetu sisi Waislamu au kwa istilahi yao hao ndugu zetu Wakristo?!. Kwa sababu katika suala la UNABII kila watu wana Istilahi zao".
-
Kauli mbiu: Amani ya Palestina ni Amani ya Tanzania;
Majlis ya Siku ya Kupigwa Upanga Imam Ali (a.s), imefanyika katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Adui Ibn Muljim (laana iwe juu yake), aliyempiga Imam Ali (a.s) kwa upanga wenye sumu kali, alijua kuwa hawezi kupambana na Imam Ali (a.s) akiwa nje ya Msikiti, hivyo akaona mbinu aliyokuwa nayo ni kumuwinda akiwa katika ibada (swala), kwani awapo katika swala huwa mwili wake na hisia zake zinatoweka Duniani, na anazungumza na Mola wake Mtukufu kama vile hayupo Duniani".
-
Ripoti Pichani | Marasimu ya Mkeshi wa Mwezi 19, katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Waumini wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashari, wamejitokeza kwa wingi katika Mkesha wa Usiku wa 19 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, uliofanyika Katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), ndani ya Masjidul Ghadir, Kigogo, Post, Dar-es-Salam, Tanzania.
-
Ripoti ya Picha | Kuhuishwa kwa Usiku wa 19 Ramadhan, Jijini Arusha-Tanzania, ambao ni Usiku wa Mwanzo wa Kifo cha Kishahidi cha Sayyidna Ali (a.s)
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA-: Waumini na wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s) Jijini Arusha, Tanzania, wamehuisha Usiku Mtukufu wa wa 19 wa Ramadhan katika Husseiniyya ya Imam Ridha (as). Usiku huu ndio Usiku ambao Amirul Muuminina Ali (a.s) alipigwa upanga kichwani akiwa ndani ya Msikiti na akiswali Swala ya Al-fajiri. Laana iwe juu ya Ibn Muljim aliyefanya tukio hili lenye kuziumiza nyoyo za Waumini. Katika picha ni Mkesha wa Kwanza wa Lailatul-Qadr ambao umeambatana na Dua mbalimbali za Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
-
Maandamano yarindima Meya wa Istanbul, hasimu wa Rais wa Uturuki alipokamatwa
Maelfu ya wananchi wa Uturuki wamemiminika barabarani kulalamikiwa kutiwa mbaroni Meya wa Istanbul, Ekrem Imamoglu, mpinzani mkuu wa kisiasa wa Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ambaye amekamatwa kwa tuhuma za rushwa na ugaidi; siku chache kabla ya kuteuliwa kuwa mgombea wa urais.
-
Netanyahu: Mashambulio yalioua watoto 174 Gaza ni mwanzo tu
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ametangaza kushadidi mashambulio mabaya dhidi ya Gaza, akionya kwamba mashambulizi ya hivi karibuni ya anga, ambayo yaliua watoto wasiopungua 174 katika ukanda huo, ni mwanzo tu wa uchokozi mkubwa zaidi dhidi ya Wapalestina.
-
Saudia: Israel inahatarisha usalama na utulivu wa eneo zima
Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudia imesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unatishia usalama na utulivu wa eneo hili zima na kwamba jamii ya kimataifa na Baraza la Usalama zina wajibu wa kutekeleza majukumu yao ipaswavyo na kusimama kidete kukabiliana na hujuma za Israel huko Palestina na Syria.
-
San'a: Iran haiingilii hata chembe maamuzi ya Yemen
Waziri wa Mambo ya Nje wa Yemen amesisitiza kuwa: Iran haingilii hata chembe maamuzi ya serikali ya San’a na kwamba operesheni za Yemen dhidi ya Wazayuni ni uamuzi huru na utaendelea kutekelezwa kivitendo hadi mzingiro wa Ghaza utakapovunjwa kikamilifu.
-
Moto mpya wa vita wawashwa na utawala wa Kizayuni huko Gaza kwa msaada wa Marekani
Kwa kukiuka makubaliano ya usitishaji vita huko Ghaza yaliyoanza kutekelezwa tarehe 19 Januari, utawala wa Kizayuni umeanzisha tena vita vya umwagaji damu dhidi ya eneo hilo lililoharibiwa na vita, kwa kufanya mashambulizi makubwa ya kinyama ambayo yamesababisha mauaji ya mamia ya mashahidi wa Kipalestina na kujeruhi wengine wengi katika ukanda huo.
-
Israel yaua watu wengine 71 katika mashambulizi dhidi ya Gaza na kuikalia tena Netzarim
Ripoti zinaonyesha kuwa ndani ya saa 24 zilizopita wanajeshi wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina zaidi ya 71 katika miji ya Beit Lahiya, Rafah na Khan Yunis, huku wengine wengi wakijeruhiwa.
-
Makundi ya muqawama yasisitiza kuunganisha juhudi ili kukabiliana na mashambulizi ya Israel
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) na Harakati ya Wananchi kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina (PFLP) zimesisitiza juu ya haja ya kuunganisha juhudi makundi ya muqawama ya Palestina na nchi za Kiarabu ili kukabiliana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni na kuunga mkono mapambano ya ukombozi katika Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza na kupinga mipango ya Marekani na utawala wa Kizayuni ya kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina.
-
Onyo la Iran kwa Marekani kuhusu matokeo mabaya ya uchokozi wa aina yoyote
Amir Saeed Irvani, Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa alitahadharisha katika barua yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatatu kwamba, hatua zozote za kichokozi zitakazofanywa na Marekani zitakuwa na matokeo mabaya na hatari mno.
-
Mkesha wa kwanza wa Laylatul Qadr waadhimishwa Iran na maeneo mengine duniani
Usiku wa kuamkia leo Alkhamisi yaani mwezi 19 Ramadhani, ulikuwa ni mkesha wa kwanza wa Laylatul Qadr na umeadhimishwa katika kona zote za Iran na maeneo mengine duniani.
-
Baqaei alaani hujuma za kijeshi dhidi ya Yemen na mauaji ya kimbari Ukanda wa Gaza
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani kuendelea mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen na mauaji ya utawala wa Kizayuni dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
-
Salamu za Nouruzi za Rais Pezeshkian kwa Wairan: Tutaifanya qadar yetu iwe bora na tukufu zaidi
Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza katika ujumbe na salamu zake za Nouruzi kwa wananchi wa Iran kwamba, Nouruz na Usiku wa Qadar (Lailatul-Qadr) ni miale miwili ya nuru moja na madhihirisho mawili ya hakika moja, na akafafanua kwa kusema: "katika mzunguko mpya wa masiku, tutaifanya qadari yetu iwe bora na tukufu zaidi kuliko ilivyo hivi sasa".
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mwaka 1404 ni "Mwaka wa Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji"
Ayatullah Khamenei Kiongozi Muadhamu uwa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma ujumbe kwa mnasaba wa kuanza mwaka mpya wa 1404 hijria shamsia na kuutaja mwaka huu mpya kuwa ni "Mwaka wa Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji."
-
Mdororo wa uchumi Ujerumani; Siemens kuwafuta kazi watu 6,000
Kampuni kubwa ya masuala ya uhandisi na teknolojia ya Siemens imesema inapania kupunguza kazi karibu 6,000 duniani kote, zikiwemo 2,850 nchini Ujerumani.
-
Ripoti ya Picha | Marasimu ya hisia kuhuisha Usiku wa 19 wa Ramadhani huko Mazar-i-Sharif
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahl al-Bayt (A.S) - Abna - Hafla ya ya kuhuisha Usiku wa 19 wa Ramadhan imefanyika kwa hisia na shauku kubwa ya wafuasi wa Amirul Momineen (a.s) katika Msikiti wa Soltanieh huko Mazar-e-Sharif, Afghanistan.
-
Tutajitahidi kufanya thamani yetu kuwa bora zaidi na ya juu zaidi kuliko ilivyo kwa sasa katika mzunguko mpya wa nyakati
Akisema kwamba Nowruz na na Nyusiku za Lailat al-Qadr ni miale miwili ya nuru moja na madhihirisho mawili ya ukweli uleule (ulio sawa), Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Tunakesha katika usiku huu ili kuwa Wanadamu wapya kwa kuzisafisha nafsi zetu na kufikia hatima (makadirio) yetu katika siku mpya, lakini hatima (makadirio) yetu na nchi yetu si mahali hapa tuliposimama; Uthamani wetu ni wa juu kuliko hali yetu ya sasa.
-
Jeshi la Yemen limeushambulia uwanja wa ndege wa "Ben Gurion"
Jeshi la Yemen limetangaza shambulizi la kulipiza kisasi la kombora kwenye uwanja wa ndege wa Ben Gurion mjini Tel Aviv.
-
Ujumbe wa Waziri wa Miongozo katika hafla ya Nowruz na Nyusiku za Lailat -ul- Qadr
Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu, kwa mnasaba wa kuwasili kwa Nowruz ya mwaka mpya wa 1404 unaosadifiana na Mikesha ya Nyusiku Tukufu za Lailatul Qadr, katika ujumbe wake, alizingatia fahari ya Iran kuwa ni faraja kwa maisha ya kila mmoja wa Wananchi.
-
Ujumbe wa Nowruz wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mnasaba wa Mwaka Mpya
Mwaka 1404, ni Mwaka wa "Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji"
Katika ujumbe wake kwa mnasaba wa mwanzo wa mwaka mpya wa 1404 Hijria Shamsia, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameutaja mwaka mpya kuwa ni mwaka wa "Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji".
-
Sehemu ya Fadhila za Kipekee za Imam Ali (a.s):
Imam Ali (a.s) ni Mtu wa Kwanza kuzaliwa ndani ya Msikiti na Kuuliwa ndani ya Msikiti
Imam Ali (a.s), Maisha yake yote yalikuwa ni Maisha ya kuweka uthabiti na kuimarisha nguzo na misingi ya Uislamu, pia kujitolea muhanga kwa kitu ghali na chenye thamani kubwa, ili kuhakikisha neno la Mwenyezi Mungu linakuwa juu, na neno la makafiri linakuwa chini.
-
Adhanom: Kukatwa misaada ya Marekani kunatishia maisha ya mamilioni ya watu
Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ameonya kwamba kukatwa ufadhili wa Marekani kwa shirika hilo, mipango yake ya afya na mashirika mengine kunatishia uhai wa mamilioni ya watu.
-
"Jina langu ni Mahmoud Khalil, mimi ni mfungwa wa kisiasa"
Mahmoud Khalil, mwanafunzi wa Kipalestina katika Chuo Kikuu cha Columbia nchini Marekani, amejieleza kama mfungwa wa kisiasa katika maoni yake ya kwanza tangu alipokamatwa na vyombo vya usalama vya Marekani kwa madai ya kuhusika katika maandamano ya watetezi wa Palestina.
-
'Waislamu wachukue msimamo wa maana dhidi ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na Wazayuni'
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Iraq ya An-Nujabaa imelaani mashambulizi ya kinyama yaliyoanzishwa tena na utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza na kuwataka Waarabu na Waislamu duniani kote wachukue misimamo thabiti dhidi ya hujuma hizo.
-
Maafisa 5 waandamizi wa HAMAS wauawa shahidi katika mashambulio ya Israel Ghaza
Maafisa watano waandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS wameuawa shahidi kufuatia mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Hamas: Marekani ni mshirika wa moja kwa moja katika vita dhidi ya watu wa Gaza
Msemaji wa harakati ya Hamas amesema harakati hiyo inatekeleza kikamilifu masharti ya makubaliano ya usitishaji vita na kwamba Wazayuni wameyakiuka akisisitiza kuwa, uratibu wa awali wa utawala huo ghasibu na Washington wa kuanzisha tena vita dhidi ya watu wa Gaza unaashiria ushiriki wa moja kwa moja wa Marekani katika jinai zinazofanywa Wazayuni.
-
Al Houthi: Israel inapanga kushambulia nchi zingine ikiwa itaangamiza Palestina
Kiongozi wa harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen ameonya kuwa utawala ghasibu wa Israel utaanza kushambulia nchi nyingine ikiwa utafanikiwa kuangamiza juhudi za ukombozi za Palestina dhidi ya ukaliaji na uchokozi wake, huku akipendekeza hatua za kijeshi na nchi za Kiarabu na Kiislamu dhidi ya utawala huo.
-
Dunia yakasirishwa na hatua ya Israel kuendeleza vita dhidi ya Gaza
Jamii ya kimataifa imebainisha hasira yake baada ya utawala katili wa Israel kuendelea na mashambulizi ya anga dhidi ya Gaza, huku ikivunja makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyokuwa na lengo la kumaliza mzozo wake wa miezi 17 na Hamas.