-
Marekani na Israel Baada ya Kushindwa katika Vita vya Siku 12; Wanajaribu Kuchochea Ghasia Nchini Iran / Vyombo vya Habari Vihangaike Kutoa Ukweli
Baada ya kushindwa katika vita vya siku 12, Marekani na Israel wanajaribu kuhamishia shinikizo ndani ya Iran kwa kuchochea ghasia za kiuchumi na kijamii; wachambuzi wakisisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kusambaza ukweli na kutofautisha kati ya madai halali na machafuko.
-
Rais wa Cuba: Mataifa ya Amerika ya Kusini Lazima Yaungane
Rais wa Cuba ametoa wito kwa mataifa ya Amerika ya Kusini kuimarisha umoja wao kufuatia operesheni ya kijeshi ya Marekani iliyosababisha kukamatwa kwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, akitaja hatua hiyo kuwa ni “shambulio la kinyama” dhidi ya taifa huru.
-
Sayyid Khamenei: Kiongozi Aliyesimama Kidete Dhidi ya Ubeberu wa Kimataifa
Baada ya hatua thabiti na za kishujaa za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran dhidi ya kambi za kijeshi za Israel na Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, dunia iliamka asubuhi ikiwa inazungumzia wasifu mpya wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei—kiongozi wa kiroho aliyeonesha ujasiri, busara na msimamo usiotetereka mbele ya madola ya kibeberu.
-
Ayatullah Khamenei:Mazungumzo na Waandamanaji Halali Yapokelewe na Kusikilizwa, Wachochezi wa Fujo na Ghasia Hawastahili Kusikilizwa Bali Wadhibitiwe
Ayatullah Khamenei amesisitiza utayari wa mazungumzo na waandamanaji halali, huku akionya kuwa wachochezi wa fujo—aliowataja kuwa mamluki wa adui—hawastahili mazungumzo na wanapaswa kuzuiwa kwa sababu ya kueneza kauli mbiu dhidi ya Uislamu, Iran na Jamhuri ya Kiislamu.
-
Muundo Mpya wa Ukuta wa Uwanja wa Palestina Tehran Wabeba Ujumbe Mkali wa Kiebrania katika Kumbukumbu ya Shahid Soleimani | Mnazidi kukaribia kutoweka
Katika kumbukumbu ya shahidi Jenerali Qasem Soleimani, jadariya jipya katika Uwanja wa Palestina, Tehran, limeibuliwa likiwa na ujumbe wa Kiebrania unaobeba onyo la kiishara kuhusu kukaribia mwisho wa zama za ubeberu na uvamizi, likisisitiza kuendelea kwa njia ya mapambano na msimamo wa upinzani.
-
China: Uchokozi wa Marekani dhidi ya Venezuela ni ukiukaji hatari wa sheria za kimataifa
Wizara ya Mambo ya Nje ya China imetangaza kuwa Beijing inapinga vikali uchokozi wa kijeshi wa Marekani nchini Venezuela na kwamba Washington lazima ifuate sheria za kimataifa na kuacha kukiuka mamlaka na usalama wa nchi nyingine.
-
Ufaransa: Hatua ya Marekani dhidi ya Maduro inakiuka sheria za kimataifa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa amesema: "Operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela inakiuka misingi ya sheria za kimataifa."
-
Urusi na Belarus zadai kurejeshwa mara moja kwa Maduro na mkewe nchini Venezuela
Mawaziri wa mambo ya nje wa Urusi na Belarus wamelaani kitendo cha Marekani cha kumteka nyara Rais wa Venezuela.
-
Wabunge wa Marekani wapinga hatua ya kijeshi ya Trump nchini Venezuela
Idadi ya wanachama wa Kongresi ya Marekani wametangaza kupinga kwao hatua ya kijeshi ya Trump nchini Venezuela.
-
Makamu wa Rais wa Maduro akawa Rais wa mpito wa Venezuela
Chombo cha kikatiba cha Venezuela kimemteua Makamu wa Rais wa nchi hiyo kuchukua madaraka ya urais.
-
Madai ya Waziri wa Vita wa Marekani: Trump ataweka masharti ya kuiongoza Venezuela
Wakati Delcy Rodríguez akichaguliwa kuwa Rais wa mpito wa Venezuela na kukataa ukoloni wowote wa nchi yake, Waziri wa Vita wa Marekani amedai kuwa Trump ataweka masharti ya kuiongoza Venezuela.
-
Trump: Baada ya Maduro, Marekani itaitawala Venezuela
Donald Trump wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari alisema: "Baada ya Maduro, Marekani itaitawala Venezuela."
-
Msisimko wa Netanyahu kuhusu uchokozi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Venezuela
Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, akikaribisha uchokozi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Venezuela, amempongeza Trump kwa kitendo hicho cha uchokozi na kumuelezea kama "kiongozi wa kihistoria na jasiri."
-
Yemen: Uchokozi dhidi ya Venezuela unaonyesha uonevu wa kisiasa na tabia ya uporaji ya Marekani
Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen, huku ikilaani uchokozi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Venezuela, imeeleza kitendo hicho kuwa ni kielelezo cha mbinu ya Washington inayojikita katika uonevu wa kisiasa, matumizi ya nguvu, sheria ya msituni, na uporaji wa rasilimali za watu.
-
Ayatollah Ameli: Trump anatafuta mafuta nchini Iran
Mwakilishi wa Kiongozi Mkuu katika mkoa wa Ardabil na Imamu wa Ijumaa wa Ardabil amesema: "Sasa imedhihirika kile Trump anachotafuta nchini Iran; ni kupata mafuta na si kuhudumia mataifa."
-
Trump Atangaza Kukamatwa kwa Rais wa Venezuela Nicolás Maduro katika Operesheni Maalum
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kukamatwa kwa Rais wa Venezuela Nicolás Maduro na mkewe katika operesheni maalum, akisema walihamishiwa New York kukabili mashtaka ya jinai, huku akisisitiza kuwa Marekani itaendelea kuhusika katika mustakabali wa Venezuela na kupambana na biashara ya dawa za kulevya.
-
Mabomu ya Atomiki ya Marekani: Historia ya Maangamizi na Maafa ya Kibinadamu | Msimulizi: Al-Muhtaram Salum Bendera +Video
Mashambulizi ya atomiki ya Marekani dhidi ya Hiroshima na Nagasaki mwaka 1945 yalisababisha vifo vya papo kwa papo vya zaidi ya watu laki mbili, uharibifu mkubwa wa mazingira na madhara ya kiafya yaliyoendelea kuathiri vizazi kwa miongo mingi.
-
Somalia Yasisitiza Umoja wa Kitaifa na kwamba Ukamilifu wa Ardhi na Mamlaka ya Taifa Lake Haviwezi Kugawanyika
Balozi wa Somalia katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa ukamilifu wa ardhi na mamlaka ya taifa la Somalia hauwezi kugawanywa, akieleza vipaumbele vya urais wa Somalia wa Baraza la Usalama Januari 2026 na kukataa vikali hatua zozote zinazolenga kudhoofisha umoja wa nchi hiyo.
-
Vitisho vya Trump dhidi ya Iran Vinatokana na Kukata Tamaa: IRGC
IRGC imesema vitisho vya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya Iran vinatokana na kukata tamaa baada ya kushindwa kuishinikiza Iran, ikisisitiza utii wake kwa Kiongozi wa Mapinduzi Ayatollah Ali Khamenei na kuendelea kulinda taifa la Iran na kuimarisha njia ya Shahidi Qassem Soleimani katika Mhimili wa Upinzani.
-
Simulizi la Kiongozi wa Mapinduzi kuhusu matukio ya hivi karibuni nchini Iran
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Ali Khamenei, amesisitiza kuwa malalamiko ya wafanyabiashara ni ya haki na yanapaswa kusikilizwa, lakini ghasia zinazosababishwa na vibaraka wa adui hazikubaliki. Ameahidi kuwa taifa litashikilia msimamo thabiti dhidi ya adui, likitegemea Mwenyezi Mungu na mshikamano wa wananchi.
-
Ayatollah Khamenei Akutana na Familia za Mashahidi, Aisisitiza Thamani ya Damu Tukufu za Mashahidi na Sadaka yao kwa Taifa +Picha
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, amekutana na familia za mashahidi katika mkutano uliojaa heshima na hisia za kina, akithibitisha mshikamano wa uongozi wa Jamhuri ya Kiislamu na kuthamini sadaka na nafasi ya mashahidi pamoja na familia zao.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Tunazungumza na Waandamanaji, lakini Wachochezi wa Ghasia Lazima Wadhibitiwe
Kiongozi wa Mapinduzi amesisitiza kuwa maandamano ya amani ni haki ya wananchi na yanapaswa kusikilizwa, lakini akabainisha kuwa ghasia na vurugu si sehemu ya maandamano halali na zinapaswa kudhibitiwa kwa mujibu wa sheria.
-
Imam Ali (a.s) na Siri za Ukuruba Wake kwa Mtume Mm Muhammad (s.a.w.w)
Imam Ali (a.s) si tu sahaba wa karibu wa Mtume (s.a.w), bali ni zao la malezi ya moja kwa moja ya Mtume, shahidi wa mwanzo wa wahyi, na mhimili wa maadili ya Kiislamu. Upendo na ufuasi wake unabaki kuwa kipimo muhimu cha uaminifu wa kweli kwa Uislamu na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w).
-
Maandamano ya Kitaifa Iran: Wananchi Waonesha Uzalendo na Kuiunga Mkono Serikali ya Kiislamu +Picha
Wananchi wa Iran wamefanya maandamano ya amani kote nchini kuadhimisha Dey 9, wakionyesha mshikamano wa kitaifa na uungaji mkono wao kwa serikali ya Kiislamu chini ya uongozi wa Ayatollah Ali Khamenei, huku wakikataa propaganda na njama za maadui wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Afrika Mashariki Yaaga Mwanachuoni Mkubwa: Mazishi ya Sheikh Ali Jumaa Mayunga Yafanyika Jijini Dar es Salaam +Picha
Kwa kuondokewa na Sheikh Ali Jumaa Mayunga, jamii ya Kiislamu Afrika Mashariki imepoteza hazina kubwa ya elimu na hekima. Hata hivyo, elimu yake, maandiko yake na athari zake zitaendelea kuishi na kuwanufaisha vizazi vijavyo, kama sadaka jariya isiyokatika matunda yake. Mwenyezi Mungu amsamehe madhambi yake, ampanulie kaburi lake, na amjaalie daraja za juu katika Pepo pamoja na waja Wake wema.
-
Maneno mapya ya kejeli ya Trump dhidi ya Iran kwa lugha ya kinafiki
Rais wa Marekani, katika matamshi ya kuingilia mambo ya ndani ya Iran, amedai: "Ikiwa Iran itafyatua risasi dhidi ya waandamanaji wenye amani, Marekani itaingilia kati ili kuwaokoa."
-
Marekani: Manuva ya China karibu na Taiwan yameongeza mivutano
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ikikosoa shughuli za kijeshi za China karibu na Taiwan, imeitaka Beijing kuacha shinikizo la kijeshi na kuingia katika mazungumzo yenye tija.
-
Abdulsalam: Kurudi nyuma mbele ya Israel na Marekani ni jambo lisiloweza kurekebishika
Mkuu wa ujumbe wa mazungumzo wa kitaifa wa Yemen, akisisitiza kuunga mkono mhimili wa mapambano huko Palestina, alionya kuwa kurudi nyuma kote mbele ya utawala wa Israel na Marekani kuna matokeo yasiyoweza kurekebishika.
-
Madai ya utawala wa Julani kuhusu kuzima mpango wa Daesh wa kushambulia sherehe za Mwaka Mpya
Wizara ya mambo ya ndani ya utawala wa Julani imetangaza kuwa imezima mpango wa kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) wa kushambulia sherehe za kuanza kwa mwaka mpya katika mikoa kadhaa ya Syria, haswa mji wa Aleppo.
-
Waziri Mkuu wa Lebanon: Hakuna anayetaka kutupa silaha za Hezbollah baharini
Waziri Mkuu wa Lebanon, akikanusha uvumi wa kutupa silaha za Hezbollah baharini au kuzikabidhi kwa utawala wa Israel, amesisitiza kuwa serikali inafanya kazi kuzuia kuongezeka kwa mvutano na kuhakikisha wanajeshi wa Israel wanajiondoa.