-
Jeshi la Israel wafanya mashambulizi mapya Gaza baada ya siku ya mauaji makubwa
Jeshi la Israel limefanya mashambulizi ya anga mashariki mwa Khan Yunis na kuua na kuwajeruhi makumi ya raia. Vikosi vya uokoaji viliopoa miili ya mashahidi na kuwahamisha waliojeruhiwa, huku hospitali zikithibitisha vifo 28, wakiwemo watoto 17.
-
Habari Pichani | Mkutano wa Mkuu wa Taasisi ya Basij ya Walioonewa na Maulamaa na Marjaa
Shirika Ia Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Asubuhi ya Alhamisi, tarehe 29 Aban 1404, Kanali Gholamreza Soleimani, Mkuu wa Taasisi ya Basij ya Walioonewa nchini Iran, katika mnasaba wa kukaribia Wiki ya Basij, alifanya ziara katika mkoa wa Qom na kukutana na baadhi ya maulamaa na marjaa na kufanya mazungumzo nao.
-
Hizbullah: Ulegevu wa serikali ya Lebanon unaongeza ukatili wa Wazayuni
Hizbullah imesisitiza katika taarifa yake kwamba serikali ya Lebanon inapaswa kufahamu kuwa kila aina ya ulegevu, udhaifu au kujisalimisha mbele ya utawala wa Kizayuni kutawafanya waongeze ukatili na tamaa zao za kupindukia.
-
Umoja wa Ulaya wakaribia kumuadhibu “Abdulrahim Dagalo” Naibu Kamanda wa Kikosi cha Mwitikio wa Haraka Sudan
Umoja wa Ulaya unakusudia kumuwekea vikwazo Abdulrahim Dagalo, Naibu Kamanda wa Kikosi cha Mwitikio wa Haraka (RSF) nchini Sudan, kwa tuhuma za ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Dkt. Khamehyar: Uturuki ya baadae haitakwenda kuelekea Uislamu wa kisiasa wa kiwango cha juu, wala haitarudi kwenye msimamo mkali wa kisekula
Mshauri wa masuala ya kimataifa wa Chuo Kikuu cha Dini na Madhehebu: Kudumu kwa chama cha AKP kwa kipindi cha miaka ishirini iliyopita kumebadilisha kabisa sura ya Uislamu wa kisiasa nchini Uturuki. Ushindani kati ya Waislamu wa kisiasa na wasekula utaendelea.
-
Dar-es-salaam | Kikao cha kufunga mwaka wa 2025 cha Jamiat Al-Mustafa International Foundation baina ya Wanafunzi na Mkuu wa Chuo
Washiriki walipata nafasi ya kutoa maoni na mapendekezo ya kuboresha utendaji wa Taasisi. Mazungumzo yalikuwa ya kujenga baina ya Mkuu wa Chuo na Wanafunzi, na yalilenga kuweka mikakati madhubuti kwa ajili ya mwaka mpya wa masomo unaofuata.
-
Kwa nini droni ya Shahed-161 ya inaashiria hatua kubwa ya Iran katika teknolojia ya ulinzi ya kujitegemea
Droni hii inaonekana kama ishara ya kuruka kwa teknolojia ya ulinzi ya Iran, ikionyesha kuwa nchi imepiga hatua kubwa katika kutengeneza mifumo ya kijeshi ya kisasa kwa kutumia ujuzi na rasilimali zake za ndani.
-
Habari Pichani | Ziara ya Naibu Mwenyekiti wa Majlisi ya Wahdatul Muslimin Pakistan katika Shirika la Habari la Kimataifa la ABNA
Hujjatul-Islam Sayyid Ahmad Iqbal Rizvi, Naibu Mwenyekiti wa Majlisi ya Wahdatul Muslimin Pakistan, katika Ziara yake alikagua idara mbalimbali za shirika hilo la ABNA na kisha kufanya mahojiano na waandishi wa habari wa ABNA.
-
Kuendelea kwa Mapigano Makali kati ya Jeshi la Sudan na Vikosi vya Mwitikio wa Haraka Kaskazini mwa Kordofan
Mapigano makali kati ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Mwitikio wa Haraka (RSF) yanaendelea katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Kordofan Kaskazini.
-
Gavana wa Texas Atangaza Ikhwanul Muslimin na Taasisi Kubwa ya Kiislamu Marekani kuwa Mashirika ya Kigaidi
Katika taarifa aliyotoa, Abbott pia ametangaza kizuizi cha umiliki wa ardhi ndani ya Texas kwa Baraza la CAIR. Haya yanajiri huku serikali ya shirikisho ya Marekani ikiwa haijawahi kuiweka Ikhwanul Muslimin au CAIR katika orodha ya mashirika ya kigaidi.
-
Mkutano wa Fedha za Saudia na Madai ya Marekani Ikulu ya White House / Trump Arudia Maneno ya Kutishia dhidi ya Iran
Katika jitihada za kuimarisha uhusiano wa kifedha na kisiasa na Riyadh, Trump alimpongeza Bin Salman na hata kugusia mauaji ya mwandishi wa habari Jamal Khashoggi, akidai bila ushahidi kwamba: “Ben Salman hakuwa na taarifa yoyote kuhusu tukio hilo!”
-
Mazishi ya Mashahidi 300 Wasiojulikana Kufanyika Siku ya Kumbukumbu ya Shahada ya Bi.Fatima(sa); Dalili ya Umoja wa Kitaifa Baada ya Vita vya Siku 12
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (IRGC) wa Mkoa Mkuu wa Tehran, Sardar Hassanzadeh, amesema kuwa miili ya mashahidi 300 wasiojulikana—ikiwa ni pamoja na 200 kwa mikoa mbalimbali na 100 kwa jiji la Tehran—iko tayari kwa ajili ya mazishi ya kitaifa. Mazishi haya yatafanyika Jumatatu tarehe 3 Azar, sambamba na kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a.s), ambapo msafara maalumu wa “Lale za Fatima” utaanza saa 2:00 asubuhi mbele ya Chuo Kikuu cha Tehran kuelekea kwenye kituo cha "Meraje’ Shohada".
-
Putin: Ushirikiano wa Urusi na China Haupingani na Upande Wowote wa Tatu
Rais wa Urusi alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa China: "Ushirikiano kati ya Moscow na Beijing hauendi kinyume na upande wowote wa tatu."
-
Msimamo wa Tusk Kuhusu Waliosababisha Mlipuko wa Reli nchini Poland
Waziri Mkuu wa Poland amefichua kuwa raia kadhaa wa Ukraine walilipua reli katika nchi hiyo.
-
White House: Trump Atatia Saini Muswada wa Kufichua Nyaraka za Epstein
White House imetangaza kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, atatia saini muswada wa kufichua nyaraka za kesi ya Jeffrey Epstein (bilionea aliyelaaniwa na mfanyabiashara wa ngono haramu).
-
Marekani: Mkataba wa Ushirikiano wa Nyuklia na Uuzaji wa F-35 kwa Saudi Arabia Umekamilika
Ikulu ya White House imetangaza kuwa Rais wa Marekani Donald Trump na Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman wamekamilisha mfululizo wa mikataba, ikiwemo ushirikiano wa nyuklia na uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Riyadh.
-
Yemen: Azimio la Marekani ni Kuhalalisha Ulezi wa Nje Juu ya Watu wa Palestina
Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imetangaza kuwa azimio la Marekani kuhusu Gaza ni kuhalalisha ulezi wa nje juu ya watu wa Palestina.
-
Hamas: Ulimwengu Umuunge Mkono Mwathirika Badala ya Kuungana na Mtesaji
Hamas, katika taarifa yake, imepongeza operesheni ya kupinga Uzayuni huko "Gush Etzion" kusini mwa Bethlehem, na kutangaza: "Ulimwengu unapaswa kumuunga mkono mwathirika, badala ya kuambatana na mtesaji."
-
Majigambo ya Netanyahu: Tumeipiga Mhimili wa Iran kutoka Pande Zote
Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, akidai kuwa utawala wake umepiga mhimili wa Iran kutoka pande zote, alijigamba: “Mkono wetu uko wazi kwa mashambulizi zaidi.”
-
Upinzani wa Palestina: Mlipuko wa Lebanon ni Pigo Kali kwa Wafuasi wa Amani na Israel
Kamati za Upinzani wa Palestina zimeelezea shambulio la Israel dhidi ya kambi ya wakimbizi ya Palestina kuwa ni pigo kubwa kwa wale wote walioegemea kwenye amani na utawala wa Kizayuni.
-
Maelezo ya Rasimu ya Azimio la Ulaya Dhidi ya Iran Katika Shirika la Nguvu za Atomiki
Chombo kimoja cha habari cha Magharibi kimetangaza maelezo mapya ya rasimu ya azimio la Marekani na Troika ya Ulaya dhidi ya Iran katika Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA).
-
Sehemu Kubwa ya Azimio la Baraza la Usalama kuhusu Gaza Inapingana na Haki za Watu wa Palestina
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaona uhalalishaji wowote wa uvamizi wa Ukanda wa Gaza na utawala dhalimu wa Kizayuni, kugawanywa kwa Gaza, na kuitenga kutoka kwenye jiografia moja ya Palestina, kuwa kinyume na matarajio ya watu wa Palestina na inaonya juu ya matokeo yake hatari.
-
Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha
Kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu (s.w.t), mitihani yote imeendeshwa kwa utaratibu uliopangwa na kukamilika kwa mafanikio. Uongozi wa madrasa mbalimbali umeonyesha ushirikiano mkubwa, huku walimu na wasimamizi wakifanya kazi kwa uadilifu na bidii kuhakikisha kwamba kila hatua ya zoezi hili inafanikishwa kwa ufanisi.
-
Habari Pichani | Mkutano wa Habari wa Maadhimisho ya Wiki ya Basij ya Mwaka wa 46
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Mkutano wa habari wa maadhimisho ya Wiki ya Basij ya mwaka wa 46 pamoja na uzinduzi wa kampeni ya “Khat Amin 2” ulifanyika leo Jumanne, tarehe 18 Novemba 2025, katika Jengo la Utamaduni na Mafunzo ya Hazrat Zahra (S) mjini Tehran. Mkutano huu ulihudhuriwa na Sardar Hossein Maroufi, Naibu Mratibu wa Shirika la Basij la Wanyonge, pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo vya ndani na nje ya nchi.
-
Kuendelea kwa Mjadala Mkali Kuhusu Mbio ya Hisani ya Msikiti wa East London; Wito Watolewa kwa Mapitio ya Sera ya Utenganisho wa Jinsia
Baada ya mashambulizi makubwa ya vyombo vya habari vya Uingereza dhidi ya mbio ya hisani iliyoandaliwa na Msikiti wa East London kwa sababu ya utenganishaji wa kijinsia, Tume ya Usawa na Haki za Kibinadamu ya Uingereza imeitangaza kwamba waandaaji wa tukio hilo wamekubali kupitia upya sera zake kabla ya awamu ijayo ya mashindano. Hata hivyo, msikiti huo umeeleza kwamba matukio kama hayo yapo kwa wingi katika maeneo mbalimbali ya Uingereza-ikiwemo mashindano maalumu ya wanawake na vipindi vya kuogelea vinavyoandaliwa katika vituo vya jamii ya Kiyahudi-lakini hakuna hata moja kati ya matukio hayo yaliyowahi kusababisha mjadala au msukosuko kama huu.
-
Mtindo wa Maisha | Ushauri / Wasia wa Kutoa Chakula Kuwalisha Watu
“Iwapo nyinyi mmekula na hamuhitaji, basi kuna watu wanaohitaji. Wapeni wao haya matunda badala ya kuyapoteza".
-
Nafasi ya Kupuuzia Mambo ya Kimaada na Thamani za Uongo katika Ndoa
Ndoa ya Bibi Fatima (a.s) na Amirul-Mu’minin Ali (a.s) ni kigezo cha pekee kinachoonyesha jinsi ambavyo mambo ya kimaada na thamani za uongo yalipuuzwa kabisa. Uteuzi wa mwenzi wa maisha ulitokana na taqwa, imani na maadili, si utajiri wala muonekano wa nje. Kwa kuishi kwa urahisi, unyenyekevu na mbali na anasa, walijenga nyumba iliyojaa utulivu, baraka na uimara wa kiroho. Mtindo huu wa maisha unatupa ujumbe wazi: ukombozi kutoka katika pupa ya mali na mapambo ndiyo njia ya kufikia furaha ya kweli katika maisha ya ndoa.
-
Imamu wa Ijumaa wa Michigan:Dunia imejifunza kutokana na uongozi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi /Ushindi wa kuvutia wa Iran katika vita vya siku 12
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Basim Al-Shar’i amesema kuwa hatari kuu kwa Jamhuri ya Kiislamuinatokana na mambo ya ndani, na akaongeza: “Nguvu ya wananchi wa Iran imo katika umoja wao na kushikamana kwao na uongozi wenye busara wa Ayatullah Khamenei. Umoja huu ndio heshima na mtaji halisi wa Jamhuri ya Kiislamu.”
-
Malawi | Majlis ya Kuadhimisha Kifo cha Abdul-Muttalib (a.s) +Picha
Utambulisho wa Abdul-Muttalib (a.s): Alikuwa kiongozi mashuhuri wa Quraysh, mwenye hekima, heshima na hadhi kubwa katika jamii ya wakati wake. Alisimama kama nembo ya uadilifu na busara miongoni mwa Waarabu wa zama za kabla ya Uislamu.
-
Hawzat Imam Zainul Aabidin (as) - Burundi | Mitihani ya Mwisho wa Muhula wa Pili -2025 +Picha
Kwa ujumla, mitihani ya leo imeendeshwa kwa mafanikio makubwa. Waalimu wameeleza kuridhika kwao na juhudi za wanafunzi, huku wakitarajia matokeo mazuri yatakayoendana na bidii waliyoionyesha wakati wa maandalizi.