ABNA swahili
  • HABARI KAMILI
  • HABARI MUHIMU
  • Iran
  • ASIA
  • ULAYA
  • AMERIKA
  • AFRIKA
  • PICHA
  • MAKALA
العربية English فارسی Türkçe اردو Español bahasa Indonesia हिन्दी français 汉语 русский Deutsch Melayu Hausa বাংলা Азәрбајҹан Азәрбајҹан әлифбасы Kiswahili မြန်မာဘာသာ bosanski português سورانی 日本語 Kurmancî Pilipinas Тоҷик italiano 한국어
×
filterToday News
  • Video | Tizama Mwili Mtukufu wa Shahidi Abu Ubaida, Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - "Imma Ushindi au Shahada"

    Video | Tizama Mwili Mtukufu wa Shahidi Abu Ubaida, Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - "Imma Ushindi au Shahada"

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Shahidi Abu Ubaidah alitumikia maisha yake yote akiwa Mujahidi dhidi ya dhulma na batili, akipigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na hatimaye akastahiki zawadi Nono ya Shahada akiwa katika mapambano hayo ya kuitetea Haki. Mwenyezi Mungu Amrehemu, yeye pamoja na Mashahidi wote, hasa wale wa Mashahidi waliokufa Kishahidi wakiwa katika Njia ya Quds. Kauli ya Daima ya Shahidi Abu-Ubaida ilikuwa ni hii: "Imma Ushindi au Shahada". Alikuwa akisema kauli hiyo kila alizokuwa akifika Mwisho wa Hotuba yake kwamba hakuna Jambo la Tatu, Bali mambo ni Mawili: Imma kupata Ushindi au Kupata Shahada. Na alikuwa akijuwa kabisa kuwa Mwenyezi Mungu atamruzuku Shahada kama zawadi ya Mapambano yake Matukufu.

    2026-01-01 02:32
  • Hafla ya Kutimiza Maonyesho ya Orchestra ya "Iranmard" kwa Heshima ya Askari Qasem Soleimani +Picha

    Hafla ya Kutimiza Maonyesho ya Orchestra ya "Iranmard" kwa Heshima ya Askari Qasem Soleimani +Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Hafla ya kutimiza maonyesho ya Orchestra ya Iranmard, iliyopangwa kuenzi kumbukumbu ya askari shujaa wa Uislamu, Marehemu Jenerali Qasem Soleimani, kwa mtazamo wa kuhifadhi utambulisho wa taifa, kujitolea, na mshikamano wa kitamaduni, ilifanyika asubuhi ya siku Jumanne (30 Desewmba, 2025) katika Ukumbi wa Vahdat. Katika sherehe hii, Seyed Abbas Salehi, Waziri wa Utamaduni na Elimu ya Sanaa ya Uislamu, alikuwa miongoni mwa waliohudhuria na kutoa hotuba.

    2026-01-01 01:04
  • Video | Maelfu ya watu walihudhuria mazishi ya Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh

    Video | Maelfu ya watu walihudhuria mazishi ya Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh

    Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA-, maelfu ya watu walikusanyika kushiriki katika mazishi ya Khaleda Zia, Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh. Khaleda Zia alikuwa kiongozi wa kisiasa wa Bangladesh, aliyeshika nafasi ya Waziri Mkuu kuanzia 1991 hadi 1996, na tena kutoka 2001 hadi 2006 katika nchi hiyo ya Asia.

    2026-01-01 00:11
  • Video | Machozi ya Bloga wa Kimarekani katika Maombolezo ya Shahada ya Abu Ubaida

    Video | Machozi ya Bloga wa Kimarekani katika Maombolezo ya Shahada ya Abu Ubaida

    Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA-, “Hailey Rothschild”, Bloga wa Kimarekani, alilia mbele ya kamera katika maombolezo ya shahada ya Abu Ubaida, msemaji wa Brigedi za Izzuddin al-Qassam, tawi la kijeshi la harakati ya Hamas.

    2025-12-31 23:53
  • Theluthi moja ya Waisraeli wanahitaji msaada wa kitaalamu wa kisaikolojia

    Theluthi moja ya Waisraeli wanahitaji msaada wa kitaalamu wa kisaikolojia

    Matokeo ya utafiti mpya yanaonyesha kuwa takriban theluthi moja ya Waisraeli wanahitaji msaada wa kitaalamu wa kisaikolojia, huku athari za vita vya Gaza kwa zaidi ya miaka miwili sasa zikiendelea kuliweka jamii ya Israel chini ya shinikizo kubwa.

    2025-12-31 23:44
  • Maadhimisho Makubwa ya Siku ya Mwenyezi Mungu (Yawmullah) 9 Dey (30 Desemba) huko Isfahan +Picha

    Maadhimisho Makubwa ya Siku ya Mwenyezi Mungu (Yawmullah) 9 Dey (30 Desemba) huko Isfahan +Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Hafla ya maadhimisho ya Siku ya Mwenyezi Mungu (Yawmullah) 9 Dey (30 Desemba), iliyojikita katika kuimarisha uelewa (basira) na kulinda thamani za Mapinduzi ya Kiislamu, ilifanyika leo asubuhi, Jumanne, kwa ushiriki mkubwa wa wananchi wa mapinduzi pamoja na viongozi na maafisa, katika Uwanja wa Mapinduzi (Meydan-e Enqelab) jijini Isfahan.

    2025-12-31 23:39
  • Mkutano wa Diplomasia na Muqawama katika Msingi wa Shule ya Haji Qasem SoleimanI

    Mkutano wa Diplomasia na Muqawama katika Msingi wa Shule ya Haji Qasem SoleimanI

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Mkutano wa Kimataifa wa Diplomasia na Muqawama katika Shule ya HajI Qasem ulifanyika kwa mnasaba wa maadhimisho ya miaka sita tangu kuuawa shahidi Luteni Jenerali Haj Qasem Soleimani, siku ya Jumatatu tarehe 29 Desemba 2025, kwa ushiriki wa Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje, pamoja na idadi ya viongozi waandamizi wa kisiasa, wataalamu wa taasisi za utafiti (think tanks), na wasomi wa vyuo vikuu. Mkutano huo ulifanyika katika Kituo cha Tafiti za Kisiasa na Kimataifa cha Wizara ya Mambo ya Nje.

    2025-12-31 23:32
  • Uvumilivu wa Kishujaa wa Imam Jawad (a.s); Mwingiliano na Mke Asiyeelewana

    Uvumilivu wa Kishujaa wa Imam Jawad (a.s); Mwingiliano na Mke Asiyeelewana

    Migogoro ni fundo linaloweza kukalia maisha ya mtu binafsi na ya kijamii; lakini ufunguo wa kulitatua si nguvu, bali ni haki (uadilifu). Mwenendo wa Imam Jawad (a.s) unaonesha kuwa hata katika migongano mikali zaidi, inawezekana kubaki binadamu, kuhifadhi heshima na kufungua njia ya uadilifu.

    2025-12-31 20:56
  • “Ukanda wa vizuizi wa Israel dhidi ya Uturuki kupitia makubaliano ya pande tatu Mediterania / Siku ngumu za kiuchumi kwa Uturuki zinakuja”

    Mtaalamu wa Kituruki katika mazungumzo na ABNA:

    “Ukanda wa vizuizi wa Israel dhidi ya Uturuki kupitia makubaliano ya pande tatu Mediterania / Siku ngumu za kiuchumi kwa Uturuki zinakuja”

    Ali Haidari, mtaalamu wa masuala ya Uturuki, amesema katika mazungumzo na ABNA kuwa Israel inajaribu kuunda ukanda wa vizuizi dhidi ya Uturuki ili kuizuia kuwasiliana na Afrika na Ulaya kupitia magharibi mwa Uturuki, na pia kuzuia Ankara kunufaika na rasilimali kubwa za Mediterania.

    2025-12-31 20:32
  • Hadhramaut; Moyo wa Mafuta wa Yemen na Kitovu cha Ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu (UAE)

    Hadhramaut; Moyo wa Mafuta wa Yemen na Kitovu cha Ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu (UAE)

    Mkoa wa Hadhramaut, eneo kubwa zaidi na lenye utajiri mkubwa wa mafuta nchini Yemen, kwa sasa umegeuka kuwa kitovu cha ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu. Licha ya vita vilivyoendelea kwa zaidi ya muongo mmoja, Hadhramaut kwa kiasi kikubwa imeepuka mapigano ya moja kwa moja kati ya serikali ya Yemen iliyojiuzulu na serikali inayoungwa mkono na Harakati ya Ansarullah; hata hivyo, mkoa huu haujaepuka athari za vita na mashindano ya ushawishi wa ndani na kikanda.

    2025-12-31 20:20
  • Kuangamiza mpango wa nyuklia wa Iran ni ndoto / Tishio la kijeshi la Marekani dhidi ya Iran lina gharama kubwa kuliko uwezo wa Washington

    Mwanasayansi wa Nyuklia wa Lebanon katika mazungumzo na ABNA:

    Kuangamiza mpango wa nyuklia wa Iran ni ndoto / Tishio la kijeshi la Marekani dhidi ya Iran lina gharama kubwa kuliko uwezo wa Washington

    Mkuu wa Kituo cha Ushauri wa Kimkakati cha Usalama wa Nishati ya Nyuklia nchini Lebanon amesisitiza kuwa Marekani—hasa katika kipindi cha Donald Trump—haina nia ya kuingia katika vita hatari dhidi ya Iran, huku Israel ikijaribu kuibebesha Washington mzigo wa gharama za makabiliano hayo.

    2025-12-31 18:30
  • waandamanaji wakataa wito wa wapinzani / juhudi za vyombo vya habari vya mapinduzi-pinzan i kupotosha madai halisi

    Kuanzia mkusanyiko wa jana hadi hali ya utulivu leo;

    waandamanaji wakataa wito wa wapinzani / juhudi za vyombo vya habari vya mapinduzi-pinzan i kupotosha madai halisi

    Inaonekana wazi kuwa vyombo vya habari pinzani, hususan mitandao ya Kifarsi inayohusishwa na Wazayuni na Magharibi, kwa makusudi vimeepuka kuzingatia madai halisi ya wafanyabiashara na badala yake vinalenga kuchochea mivutano na machafuko ya kijamii.

    2025-12-30 23:59
  • Iran yaangazia nafasi ya Jenerali Soleimani kama “mbunifu wa Mhimili wa Mapambano”

    Iran yaangazia nafasi ya Jenerali Soleimani kama “mbunifu wa Mhimili wa Mapambano”

    2025-12-30 23:50
  • Mwenyezi Mungu Akiwa Upande Wako, Hakuna Awezaye Kukudhuru

    Mwenyezi Mungu Akiwa Upande Wako, Hakuna Awezaye Kukudhuru

    Lengo na makusudio ya kauli hii inayosapoti na Aya hizo Tukufu ni kuondoa hofu moyoni, kwa kutomwogopa yeyote anayenuia kuwa “juu yako” au kukudhuru kwa lolote, kwani Mwenyezi Mungu akiwa pamoja nawe, hakuna mwenye uwezo juu yako isipokuwa kwa idhini Yake.

    2025-12-30 16:59
  • Afisa wa Urusi: Marekani iache kuunga mkono wanaotaka kujitenga wa Taiwan

    Afisa wa Urusi: Marekani iache kuunga mkono wanaotaka kujitenga wa Taiwan

    Afisa mmoja wa bunge la Urusi amesema kuwa Marekani na China zinaweza tu kuwa karibu ikiwa Washington itaacha kusaidia wanaotaka kujitenga wa Taiwan.

    2025-12-30 13:51
  • Afisa wa usalama wa Urusi: Zelensky lazima aishi mafichoni maisha yake yote

    Afisa wa usalama wa Urusi: Zelensky lazima aishi mafichoni maisha yake yote

    Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi amesema kuwa Rais wa Ukraine lazima aishi kwa siri maisha yake yote yaliyosalia.

    2025-12-30 13:51
  • Mbunge wa Belarus: Kyiv inaelekea kusambaratika kutokana na kuongeza mivutano

    Mbunge wa Belarus: Kyiv inaelekea kusambaratika kutokana na kuongeza mivutano

    Mbunge mmoja wa Belarus amesema kuwa utawala wa Ukraine unaelekea kusambaratika kwa kuongeza mivutano na Moscow.

    2025-12-30 13:50
  • Trump: Mazoezi ya kijeshi ya China karibu na Taiwan hayatii wasiwasi

    Trump: Mazoezi ya kijeshi ya China karibu na Taiwan hayatii wasiwasi

    Rais wa Marekani amepuuzia uwezekano wa China kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya vikosi vya wanaotaka kujitenga wa Taiwan katika siku za usoni.

    2025-12-30 13:50
  • Mwitikio wa Ansarullah kwa harakati za Imarati na Saudi Arabia kusini mwa Yemen

    Mwitikio wa Ansarullah kwa harakati za Imarati na Saudi Arabia kusini mwa Yemen

    Mmoja wa maafisa wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amejibu maendeleo ya kusini mwa nchi hiyo na harakati za Imarati (UAE) na Saudi Arabia.

    2025-12-30 13:49
  • Mamluki wa Imarati: Shambulio la Saudi Arabia nchini Yemen lilikuwa la kichokozi

    Mamluki wa Imarati: Shambulio la Saudi Arabia nchini Yemen lilikuwa la kichokozi

    Naibu Mwenyekiti wa baraza linalofungamana na Imarati (UAE) nchini Yemen ameelezea shambulio la leo la muungano wa Saudia dhidi ya Hadramout kama uchokozi.

    2025-12-30 13:48
  • Axios: Trump na Netanyahu wakubaliana kutekeleza hatua ya pili ya usitishaji vita Gaza

    Axios: Trump na Netanyahu wakubaliana kutekeleza hatua ya pili ya usitishaji vita Gaza

    Tovuti moja ya Marekani imeandika kuwa Netanyahu na Trump katika mkutano wao huko Florida, licha ya tofauti ndogo za kimaoni, wamekubaliana kutekeleza hatua ya pili ya usitishaji vita huko Gaza.

    2025-12-30 13:48
  • Mwitikio wa Ansarullah ya Yemen kuhusu kifo cha kishahidi cha Abu Obeida

    Mwitikio wa Ansarullah ya Yemen kuhusu kifo cha kishahidi cha Abu Obeida

    Ofisi ya kisiasa ya Ansarullah nchini Yemen, ikisisitiza kuendeleza njia ya mashahidi mashujaa wa upinzani, imetoa pongezi na rambirambi kwa kuuawa kishahidi kwa kundi la makamanda wa Brigedi za Al-Qassam huko Gaza katika mashambulizi ya adui wa Kizayuni.

    2025-12-30 13:48
  • Onyo la Saudi Arabia kwa Imarati (UAE): "Ondoa majeshi yako Yemen"

    Onyo la Saudi Arabia kwa Imarati (UAE): "Ondoa majeshi yako Yemen"

    Kuongezeka kwa mapigano nchini Yemen na jukumu la Imarati katika kuunga mkono waasi wa kusini mwa nchi hiyo kumepelekea Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia kutoa onyo kwa Abu Dhabi.

    2025-12-30 13:47
  • Jenerali Abdollahi: Utawala wa Kizayuni unadhibiti takwimu za mapigo uliyopata

    Jenerali Abdollahi: Utawala wa Kizayuni unadhibiti takwimu za mapigo uliyopata

    Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya alisema: "Utawala wa Kizayuni ulipata mapigo makali sana katika vita vya siku 12, lakini utawala huo unadhibiti na kuficha takwimu za vifo na mapigo uliyopata."

    2025-12-30 13:46
  • Sa‘yi kati ya Safa na Marwa: Alama ya Imani na Nguzo Muhimu ya Hija na Umra

    Sa‘yi kati ya Safa na Marwa: Alama ya Imani na Nguzo Muhimu ya Hija na Umra

    Aya hii tukufu inathibitisha kuwa sa‘yi baina ya Safa na Marwa ni sehemu muhimu ya ibada ya Hija na Umra, na kwamba hakuna dhambi wala lawama katika kuitekeleza. Kinyume chake, ni ibada iliyoidhinishwa na Qur’ani na kusisitizwa na Sunna ya Mtume ﷺ, na aya imekuja mahsusi kuondoa shaka na uzito uliokuwepo katika nyoyo za watu kuhusu ibada hii.

    2025-12-30 12:05
  • Trump Akiri Kushiriki katika Jinai

    Trump Akiri Kushiriki katika Jinai

    Kauli ya Donald Trump, rais wa Marekani, iliyokiri wazi kiwango cha msaada mkubwa wa Marekani kwa Israel, imezua mjadala mpana katika uwanja wa siasa za kimataifa. Wachambuzi wanasema kauli hiyo inaashiria ushiriki wa moja kwa moja wa Marekani katika sera na hatua zinazohusishwa na ukaliaji wa ardhi, uvamizi na ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya wananchi wa Palestina, jambo lililoibua maswali mazito kuhusu uwajibikaji wa kimaadili na kisheria wa Washington mbele ya jumuiya ya kimataifa.

    2025-12-30 01:44
  • Ukraine Yashambulia Makaazi ya Putin kwa Ndege Droni 91 / Trump Ashtuka

    Ukraine Yashambulia Makaazi ya Putin kwa Ndege Droni 91 / Trump Ashtuka

    Ikulu ya Kremlin jioni ya Jumatatu ilitangaza kuwepo kwa mawasiliano ya simu kati ya marais wa Urusi na Marekani, na kubainisha kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, alishtushwa na shambulio la ndege zisizo na rubani (droni) la Ukraine dhidi ya makaazi ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin.

    2025-12-30 01:29
  • Abu Ubaida: Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Iliamsha Dhamiri za Ulimwengu / Hatutaweka Silaha Chini; Israel Lazima Ivuliwe Silaha +Picha-Video

    Abu Ubaida: Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Iliamsha Dhamiri za Ulimwengu / Hatutaweka Silaha Chini; Israel Lazima Ivuliwe Silaha +Picha-Video

    Msemaji mpya wa Brigedi za Al-Qassam, katika hotuba yake ya leo usiku, pamoja na kutangaza kuuawa shahidi kwa idadi ya makamanda wakuu wa harakati hiyo, amesema kuwa wanasisitiza kwamba taifa la Palestina kamwe halitaweka silaha zake chini, na kwamba mjadala unaolenga kushughulikia au kunyang’anya silaha za Wapalestina unapaswa kukomeshwa.

    2025-12-29 23:24
  • Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi Jijini Mwanza Watunukiwa Tuzo za Amani Kupitia Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026

    Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi Jijini Mwanza Watunukiwa Tuzo za Amani Kupitia Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026

    Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026 imetoa tuzo za heshima kwa viongozi wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Jeshi la Polisi, kama ishara ya kutambua mchango wao katika kudumisha amani, mshikamano na utulivu wa kijamii. Tuzo hizo zilitolewa katika hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za serikali, vyombo vya ulinzi na jamii kwa ujumla kuelekea maandalizi ya tukio hilo muhimu la Maridhiano Day 2026.

    2025-12-29 22:58
  • Mkwamo katika Bunge la Iraq; mizani ya kisiasa yameelemea kwa Waislamu wa Kishia na Wakurdi

    Mkwamo katika Bunge la Iraq; mizani ya kisiasa yameelemea kwa Waislamu wa Kishia na Wakurdi

    Wakati ambapo Waislamu wa Kisunni wameshindwa kufikia mwafaka juu ya mgombea mmoja, hatima ya urais wa Bunge la Iraq imefungamana zaidi kuliko wakati mwingine wowote na maamuzi pamoja na hesabu za kisiasa za Waislamu wa Kishia na vyama vya Kikurdi.

    2025-12-29 19:24
  • Previous
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • Next
Sauti ya Mashia wasio na Vyombo vya Habari.
Desktop version Mobile version

Nukuu ya "Maudhui" inaruhusiwa bila kutaja chanzo

Nastooh Saba Newsroom