-
Urusi: Zelensky Hataki Kujiondoa Licha ya Hasara Kubwa
Balozi wa Urusi katika Umoja wa Mataifa alisema kwamba Rais wa Ukraine hauko tayari kukubali kupoteza miji katika vita na Urusi na haitoi amri kwa vikosi vyake kujiondoa.
-
Kallas: "Tumemwekea vikwazo Dagalo"; Tunatafuta kuunga mkono Ukraine
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, akitangaza kuweka vikwazo dhidi ya kamanda namba mbili wa Kikosi cha Msaada wa Haraka nchini Sudan, alisema: "Tuna mpango wazi wa hatua mbili: kudhoofisha Urusi na kuunga mkono Ukraine."
-
Maelezo ya Mpango wa Trump wa Kusitisha Mapigano Nchini Ukraine
Vyanzo vya Ukraine vimefichua maelezo ya mpango wa Rais wa Marekani wa kusitisha mapigano nchini humo.
-
Afisa wa Marekani: Wakati Umefika wa Kumaliza Vita vya Ukraine
Mwakilishi wa Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa alisema kwamba wakati umefika wa kumaliza vita vya Ukraine.
-
Mwitikio Mkali wa Kuwait kwa Mashambulizi ya Utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza
Wizara ya Mambo ya Nje ya Kuwait imejibu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza kwa kutoa taarifa.
-
Hasira za Riyadh Juu ya Sera za Netanyahu Zisizodhibitiwa na Zisizoleta Utulivu Katika Kanda
Mashambulizi dhidi ya Gaza na kupuuza kwa utawala wa Kizayuni kwa mamlaka ya Syria kumepelekea mwitikio kutoka Riyadh.
-
Hatari za Azimio la Marekani kwa Utawala wa Gaza; Matukio Yanayokuja kwa Upinzani
Katika hali ambayo azimio lililopitishwa na Marekani katika Baraza la Usalama, likipuuza haki za watu wa Gaza, linafuata maslahi ya Wazayuni; kuna matukio kadhaa yanayowezekana kwa mmenyuko wa Upinzani wa Palestina.
-
Ziara ya Naibu Waziri Mkuu wa Lebanon mjini Damascus na Mkutano na Jolani
Rais aliyejitangaza wa Syria na Naibu Waziri Mkuu wa Lebanon walijadili faili la watu waliopotea na suala la mipaka, pamoja na njia za kuendeleza uhusiano wa pande mbili.
-
Vikwazo Vipya vya Marekani Dhidi ya Iran
Wizara ya Hazina ya Marekani imetangaza vikwazo vipya dhidi ya Iran.
-
Araghchi: Tuko tayari zaidi kuliko kabla ya vita vilivyopita; Tunaunga mkono makubaliano ya haki
Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi yetu, akisema kuwa Iran iko tayari zaidi kuliko kabla ya vita vilivyopita, alisema: "Tunaunga mkono makubaliano ya haki."
-
Kutua kwa Ndege ya Elfu Moja Iliyobeba Silaha katika Uwanja wa Ndege wa Ben-Gurion huko Tel Aviv
Ndege ya elfu moja iliyobeba silaha na rasilimali za kijeshi tangu kuanza kwa vita vya Gaza, kama sehemu ya daraja kubwa la anga la Israel, imepataja kwenye uwanja wa ndege wa Ben-Gurion.
-
Barua za Nahjul Balagha - Barua ya 32 | Mbinu za Muawiya, Njia ya Vyombo vya Habari vya Kigeni vya Leo
Mbinu za vyombo vya habari katika kueneza batili na kuunda shubha ili kuwazamisha watu ndani ya fikra zisizo za Kimungu zimekuwa zikitumiwa na wapinzani wa njia ya haki katika vipindi vyote vya historia. Ingawa njia hizi hubadilika kulingana na zama, malengo yao hubaki yale yale. Kurejea mbinu hizi katika mojawapo ya barua za Imam Ali (a.s) kwa Muawiya na kulinganisha na mbinu za vyombo vya habari vya kigeni katika ulimwengu wa leo kunadhihirisha ukweli kwamba “Muawiya na wanaofanana naye” katika historia wamejitahidi kupotosha wengine ili kufikia malengo yao wenyewe-juhudi ambazo hatimaye hupelekea maangamizi yao pamoja na maangamizi ya wale wanaowafuata.
-
Urusi Inapanga Kuanzisha Kambi 9 za Kijeshi Katika Eneo la Kusini mwa Syria
Urusi, kwa lengo la kurejesha ushawishi wake wa kijeshi hadi mpaka wa kusini mwa Syria, inapanga kuanzisha vituo 9 vipya vya kijeshi katika mikoa ya Quneitra na Daraa.
-
Habari Pichani | Uchambuzi wa Utafiti Kuhusu Nafasi ya Mwanamke katika Kuandaa Njia ya Kufufuka kwa Imam
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Jumuiya ya Kimataifa ya Hazrat Ali Asghar (a.s) kwa mara ya kwanza imewasilisha na kuchambua matokeo mapya ya utafiti wake kuhusu (mchango au) jukumu la malezi na maandalizi la Mwanamke katika kufanikisha kudhihiri kwa Imam wa zama (atfs), pamoja na matokeo mapya ya utafiti kuhusu Kanzu ya Imam Hussein (a.s). Hafla hiyo ilifanyika asubuhi ya leo Ijumaa, 21 Novemba 2025, katika chumba cha ibada cha Hazrat Zahra (sa), katika Haram ya Hazrat Fatima Masoumeh (sa), kwa ushiriki wa wanawake wenye elimu na maarifa pamoja na heshima kubwa.
-
Utekelezaji wa programu 2,000 kwa wakati mmoja sambamba na Wiki ya Basiji katika jiji la Rasht
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (Sepah) katika eneo la kati la Rasht alisema kuwa zaidi ya programu maalumu 2,000 za Wiki ya Basiji zimepangwa kutekelezwa katika vituo vya usalama vya Basiji pamoja na maeneo ya akina kaka na dada. Alisema kuwa Basiji ni nguvu madhubuti ya nchi kwa nyanja zote.
-
Mkataba wa mabilioni kadhaa ya dola wa Israel kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa ngao ya Chuma (Iron Dome)
Wizara ya Ulinzi ya Israel imetiliana saini mkataba mkubwa na Kampuni ya Rafael ili kuongeza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa makombora ya kukinga ya mfumo wa Iron Dome (Gombo la Chuma).
-
Kufungwa kwa Uwanja wa Ndege wa Sana’a kumeweka maisha ya maelfu ya wagonjwa katika hatari
Kwa kuendelea kwa mzingiro na kusitishwa kwa shughuli za Uwanja wa Ndege wa Sana’a, maelfu ya wagonjwa wa Yemen wamenyimwa upatikanaji wa dawa na fursa ya kutibiwa nje ya nchi.
-
Jeshi la Israel wafanya mashambulizi mapya Gaza baada ya siku ya mauaji makubwa
Jeshi la Israel limefanya mashambulizi ya anga mashariki mwa Khan Yunis na kuua na kuwajeruhi makumi ya raia. Vikosi vya uokoaji viliopoa miili ya mashahidi na kuwahamisha waliojeruhiwa, huku hospitali zikithibitisha vifo 28, wakiwemo watoto 17.
-
Habari Pichani | Mkutano wa Mkuu wa Taasisi ya Basij ya Walioonewa na Maulamaa na Marjaa
Shirika Ia Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Asubuhi ya Alhamisi, tarehe 29 Aban 1404, Kanali Gholamreza Soleimani, Mkuu wa Taasisi ya Basij ya Walioonewa nchini Iran, katika mnasaba wa kukaribia Wiki ya Basij, alifanya ziara katika mkoa wa Qom na kukutana na baadhi ya maulamaa na marjaa na kufanya mazungumzo nao.
-
Hizbullah: Ulegevu wa serikali ya Lebanon unaongeza ukatili wa Wazayuni
Hizbullah imesisitiza katika taarifa yake kwamba serikali ya Lebanon inapaswa kufahamu kuwa kila aina ya ulegevu, udhaifu au kujisalimisha mbele ya utawala wa Kizayuni kutawafanya waongeze ukatili na tamaa zao za kupindukia.
-
Umoja wa Ulaya wakaribia kumuadhibu “Abdulrahim Dagalo” Naibu Kamanda wa Kikosi cha Mwitikio wa Haraka Sudan
Umoja wa Ulaya unakusudia kumuwekea vikwazo Abdulrahim Dagalo, Naibu Kamanda wa Kikosi cha Mwitikio wa Haraka (RSF) nchini Sudan, kwa tuhuma za ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Dkt. Khamehyar: Uturuki ya baadae haitakwenda kuelekea Uislamu wa kisiasa wa kiwango cha juu, wala haitarudi kwenye msimamo mkali wa kisekula
Mshauri wa masuala ya kimataifa wa Chuo Kikuu cha Dini na Madhehebu: Kudumu kwa chama cha AKP kwa kipindi cha miaka ishirini iliyopita kumebadilisha kabisa sura ya Uislamu wa kisiasa nchini Uturuki. Ushindani kati ya Waislamu wa kisiasa na wasekula utaendelea.
-
Dar-es-salaam | Kikao cha kufunga mwaka wa 2025 cha Jamiat Al-Mustafa International Foundation baina ya Wanafunzi na Mkuu wa Chuo
Washiriki walipata nafasi ya kutoa maoni na mapendekezo ya kuboresha utendaji wa Taasisi. Mazungumzo yalikuwa ya kujenga baina ya Mkuu wa Chuo na Wanafunzi, na yalilenga kuweka mikakati madhubuti kwa ajili ya mwaka mpya wa masomo unaofuata.
-
Kwa nini droni ya Shahed-161 ya inaashiria hatua kubwa ya Iran katika teknolojia ya ulinzi ya kujitegemea
Droni hii inaonekana kama ishara ya kuruka kwa teknolojia ya ulinzi ya Iran, ikionyesha kuwa nchi imepiga hatua kubwa katika kutengeneza mifumo ya kijeshi ya kisasa kwa kutumia ujuzi na rasilimali zake za ndani.
-
Habari Pichani | Ziara ya Naibu Mwenyekiti wa Majlisi ya Wahdatul Muslimin Pakistan katika Shirika la Habari la Kimataifa la ABNA
Hujjatul-Islam Sayyid Ahmad Iqbal Rizvi, Naibu Mwenyekiti wa Majlisi ya Wahdatul Muslimin Pakistan, katika Ziara yake alikagua idara mbalimbali za shirika hilo la ABNA na kisha kufanya mahojiano na waandishi wa habari wa ABNA.
-
Kuendelea kwa Mapigano Makali kati ya Jeshi la Sudan na Vikosi vya Mwitikio wa Haraka Kaskazini mwa Kordofan
Mapigano makali kati ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Mwitikio wa Haraka (RSF) yanaendelea katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Kordofan Kaskazini.
-
Gavana wa Texas Atangaza Ikhwanul Muslimin na Taasisi Kubwa ya Kiislamu Marekani kuwa Mashirika ya Kigaidi
Katika taarifa aliyotoa, Abbott pia ametangaza kizuizi cha umiliki wa ardhi ndani ya Texas kwa Baraza la CAIR. Haya yanajiri huku serikali ya shirikisho ya Marekani ikiwa haijawahi kuiweka Ikhwanul Muslimin au CAIR katika orodha ya mashirika ya kigaidi.
-
Mkutano wa Fedha za Saudia na Madai ya Marekani Ikulu ya White House / Trump Arudia Maneno ya Kutishia dhidi ya Iran
Katika jitihada za kuimarisha uhusiano wa kifedha na kisiasa na Riyadh, Trump alimpongeza Bin Salman na hata kugusia mauaji ya mwandishi wa habari Jamal Khashoggi, akidai bila ushahidi kwamba: “Ben Salman hakuwa na taarifa yoyote kuhusu tukio hilo!”
-
Mazishi ya Mashahidi 300 Wasiojulikana Kufanyika Siku ya Kumbukumbu ya Shahada ya Bi.Fatima(sa); Dalili ya Umoja wa Kitaifa Baada ya Vita vya Siku 12
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (IRGC) wa Mkoa Mkuu wa Tehran, Sardar Hassanzadeh, amesema kuwa miili ya mashahidi 300 wasiojulikana—ikiwa ni pamoja na 200 kwa mikoa mbalimbali na 100 kwa jiji la Tehran—iko tayari kwa ajili ya mazishi ya kitaifa. Mazishi haya yatafanyika Jumatatu tarehe 3 Azar, sambamba na kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a.s), ambapo msafara maalumu wa “Lale za Fatima” utaanza saa 2:00 asubuhi mbele ya Chuo Kikuu cha Tehran kuelekea kwenye kituo cha "Meraje’ Shohada".
-
Putin: Ushirikiano wa Urusi na China Haupingani na Upande Wowote wa Tatu
Rais wa Urusi alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa China: "Ushirikiano kati ya Moscow na Beijing hauendi kinyume na upande wowote wa tatu."