-
Iraq yatangaza vituo vya mipakani kwa raia wa kigeni na wahamiaji watakaoshiriki Arubaini ya Imam Husayn (as)
Serikali ya Iraq imetangaza taratibu za kuingia na kutoka nchini kupitia vituo maalumu vya mipakani kwa raia wa kigeni na wahamiaji wanaokusudia kushiriki ibada ya Arubaini ya Imam Husayn (as) katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala.
-
Waumini Nakuru, Kenya Waadhimisha Kumbukumbu ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran kwa Dua na Maombolezo +Picha
Waumini mjini Nakuru nchini Kenya wamekusanyika katika hafla ya maombolezo na dua kwa ajili ya kumkumbuka kiongozi wa Mapinduzi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wakieleza mshikamano wao na kutoa heshima kwa mchango wake katika kutetea waliodhulumiwa na kusimamia misingi ya Uislamu na haki.
-
Marasimu ya Maombolezo na Kumbukumbu ya Imam Shahidi Yaandaliwa katika Haram ya Bibi Fatima Ma'suma (s.a) Qom +Picha
Sherehe ya kuenzi kumbukumbu ya Imam Shahidi, Sayyid Ali Khamenei (Mwenyezi Mungu ainue daraja lake), imefanyika katika Haram Tukufu ya Bibi Fatima Masuma (a.s.) mjini Qom, kwa mwaliko wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Shule ya Wasichana Yaadhimisha Shahada ya Imam Sajjad (a.s.) kwa Majlisi ya Maombolezo +Picha
Majlisi ya maombolezo ya kumbukumbu ya shahada ya Imam Ali ibn al-Husayn As-Sajjad (a.s.) imefanyika katika Shule ya Wasichana, ambapo washiriki 144 walihudhuria na kupata mawaidha kuhusu maisha, subira na urithi wa Imam wa Nne wa Ahlul-Bayt (a.s.).
-
Tazama Waombolezaji Walivyodhihirisha Mapenzi ya Dhati kwa Shahidi Sayyid Ali Hussein Khamenei (ra) Wakisubiri Kuwasili kwa Mwili Wake +Picha
Waombolezaji walikesha katika maeneo ya mazishi wakiwa wamelala huku wakikumbatia picha za Shahidi Sayyid Ali Hussein Khamenei (ra), wakionyesha upendo wao wa dhati na uaminifu kwa kiongozi wao walipokuwa wakisubiri kuwasili kwa mwili wake ili watoe heshima za mwisho.
-
Mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu na Mashahidi wa Familia Yake Wawasili Mashhad Ukisindikizwa na Ndege za Kivita +Video
Ndege za kivita za Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimesindikiza ndege iliyobeba mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi pamoja na mashahidi wa familia yake, kabla ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Shahid Hashemi Nejad mjini Mashhad, huku maandalizi ya mazishi yakiendelea.
-
Kisa cha Kihistoria:Jinsi na Kwa Nini Shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hashimi Nejad Aliuawa na Shirika la Kigaidi la Mujahideen-e Khalq /MEK
Kwa mujibu wa simulizi za kihistoria, kuuawa kwa Shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hashimi Nejad mnamo mwaka 1981 kulikuwa sehemu ya mfululizo wa mauaji yaliyotekelezwa na Shirika la Kigaidi la Mujahideen-e Khalq (MEK), likiwa na lengo la kuwaondoa viongozi waliokuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
-
Hali na Matukio mbalimbali ya Karbala Jinsi Yalivyokuwa Wakati wa Kumpokea Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra) +Picha
Mji Mukufu wa Karbala jana ulitawaliwa na huzuni kubwa na hali ya maombolezo pindi Waumini walipokuwa wakisubiri kuwasili kwa mwili wa Ayatollah Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra) kwa ajili ya shughuli za kutoa heshima zao za mwisho.
-
Wanafunzi wa Jamiat AlMustafa(s)Tanzania Washiriki Mazishi ya Ayatollah Imam Sayyid Ali Khamenei(ra) Wakifuatilia Moja kwa Moja Kupitia Mtandao+Picha
Wanafunzi wa Taasisi ya Kimataifa ya Al-Mustafa nchini Tanzania walifuatilia kwa njia ya matangazo ya moja kwa moja (live) kupitia mtandao ibada ya mazishi na maziko ya Ayatullah Imam Sayyid Ali Khamenei mjini Mashhad, wakionesha mshikamano na kuwapa pole wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Swala ya Maiti Yasalishwa kwa Mwili wa Ayatollah Sayyid Ali Husseini Khamenei katika Haram ya Amirul Muuminiin (a.s.) mjini Najaf + (Video 7 +Picha 4)
Swala ya maiti ya Ayatollah Sayyid Ali Husseini Khamenei imesaliwa katika Haram Tukufu ya Amirul Muuminiin Imam Ali (a.s.) mjini Najaf, chini ya uongozi wa Ayatollah Sayyid Muhammad Taqi Al-Hakim, huku waumini na wanazuoni wengi wakihudhuria kumuombea rehema na kutoa heshima zao za mwisho.
-
Mwili wa Kiongozi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei Wafikishwa katika Haram ya Imam Hussein (a.s.) Karbala +Picha
Mwili mtukufu wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Hussein Khamenei, pamoja na miili ya mashahidi wa familia yake, umefikishwa katika Haram Tukufu ya Imam Hussein (a.s.) mjini Karbala, ambako maelfu ya waombolezaji wamejitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi huyo.
-
Malawi: Waumini Wakamilisha (Kisomo) Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Roho na Nafsi ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei +Picha
Waumini nchini Malawi wamekusanyika katika Shule ya Al-Hadi chini ya uwakilishi wa Al-Mustafa kufanya Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa ajili ya kumuombea Shahidi Sayyid Ali Khamenei.
-
Viongozi wa Dini na Serikali Waungana na Mamilioni ya Wananchi Katika Mji wa Qom kushiriki Mazishi ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei +Picha
Maulamaa, wanazuoni, viongozi wa kidini na serikali pamoja na mamilioni ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Iran wamekusanyika katika mji wa Qom kushiriki marasimu ya mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Taifa, Shahidi Sayyid Ali Khamenei.
-
Mamilioni Wafurika Qom Kumuaga na Kumuenzi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei +Picha
Mamilioni ya waombolezaji walikusanyika katika Msikiti wa Jamkaran mjini Qom kushiriki katika marasimu ya kumuaga na kumuenzi Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, huku Sala ya Maiti ikiongozwa na Ayatollah Javadi Amoli.
-
Maelfu na Mamilioni ya Waombolezaji Washiriki Katika Mazishi ya Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei nchini Iran+Picha
Mamilioni ya waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ya Iran na baadhi ya nchi nyingine walijitokeza kushiriki katika mazishi ya Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, wakionesha heshima, mapenzi na mshikamano wao kwa Kiongozi huyo.
-
Dunia Yashuhudia Mamilioni ya Waombolezaji Wakimzika Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei +Picha
Mamilioni ya watu walifurika katika mitaa ya mji mkuu wa Tehran kushiriki mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, pamoja na baadhi ya wanafamilia wake waliouawa na kufikia daraja ya shahada.
-
Upendo wa Kitaifa na Kimataifa | Maelfu Waendelea Kumiminika Jijini Tehran - Iran Kumuenzi Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei +Picha
Maelfu ya waombolezaji kutoka Iran na mataifa mbalimbali duniani wameendelea kufika kuanzia jana (Jumamosi) alfajiri hadi usiku ili kutoa heshima zao za mwisho kwa Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei, wakimkumbuka kwa unyenyekevu wake na msimamo wake wa kutetea wanyonge, hususan wananchi wa Palestina.
-
Waombolezaji waaga Mwili Mtukufu wa Kiongozi Shahidi katika Msala wa Imam Khomeini Jijini Tehran +Picha
Maelfu ya waombolezaji wamejitokeza katika Msala wa Imam Khomeini (Quds Sirruh) mjini Tehran kutoa heshima zao za mwisho na kuuaga mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei (Qudsallahu Nafsahu Az-Zakiyyah), katika mazingira ya huzuni na majonzi makubwa.
-
Hali ya Majonzi Yatanda Tehran sambamba na kuanza kwa Shughuli za Kumuaga Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Hali ya majonzi na huzuni kubwa imeendelea kutawala katika mji wa Tehran kuelekea shughuli za mwisho za kumuaga Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei(Ra), huku umma wa Kiislamu ukiendelea kutoa heshima zake kwa Kiongozi huyu Mwema na mtetezi wa Haki za Wapalestina na Haki za wanyonge popote walipo Ulimwenguni.
-
Rais wa Iran Akutana na Ujumbe wa Nje Uliohudhuria Shughuli za Maombolezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu +Picha
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na ujumbe mbalimbali wa nchi za nje uliohudhuria shughuli za maombolezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ambapo walisisitiza mshikamano na nafasi yake katika Umma wa Kiislamu.
-
Kibaha - Pwani | Waumini wa Shia Kibaha Wafanya Matembezi ya Amani ya A'shura, Wasisitiza Ujumbe wa Haki na Kupinga Dhulma+Picha
Mamia ya Waumini wa Madhehebu la Shia Ithna Ashari katika Mji wa Kibaha, Mkoani Pwani, wamefanya Matembezi ya Amani ya A'shura kwa Mwaka wa 1448 H - 2026 kwa lengo la kuhuisha kumbukumbu ya Shahada ya Imam Hussein (AS) na kuendeleza mafunzo ya haki, uadilifu na kupinga dhulma.
-
Maelfu Washiriki Maombolezo ya A'shura Kigogo Post, Dar-es-Salaam, Wakisisitiza Uhuishaji wa Daima wa Mafunzo ya Imam Hussein (AS) +Picha
Waumini na wapenzi wa Ahlul-Bayt (AS) wamefanya maandamano ya amani katika eneo la Kigogo Post, Dar-es-Salaam, kuomboleza tukio la Karbala na kusisitiza kuendeleza ujumbe wa mapinduzi ya Imam Hussein (AS).
-
Arusha | Waumini Wafanya MatembezI ya ya Amani ya Kidini Wakimuitikia Imam Hussein (AS) kwa Kauli ya "Labbayka Ya Hussein" +Picha
Waumini wa Arusha wamefanya matembezi ya Amani ya Kidini kuhuisha kumbukumbu ya Imam Hussein (AS), yakianzia Husseiniya ya Imam Ridha (AS) Ngarenaro hadi Shamsi na kurejea Husseiniya, wakisisitiza kauli ya “Labbayka Ya Hussein” kwa ushiriki wa Taasisi ya Sayyid al-Shohadaa na jumuiya mbalimbali.
-
Waumini wa Kishia Moshi Waendeleza Majalisi ya Kumuomboleza Imam Hussein (a.s) katika Mwezi wa Muharram+Picha
Waislamu wa madhehebu ya Shia jijini Moshi wameendelea kufanya Majalisi za maombolezo ya Imam Hussein (a.s) katika Mwezi Mtukufu wa Muharram 1448H/2026, wakikumbuka shahada ya mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) na mashujaa wa Karbala waliopigania haki na uadilifu.
-
Sheikh Mkuu wa TIC Ashiriki Zoezi la Usafi Kigogo katika Kumuenzi Imam Hussein (a.s) +Picha
Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Tanzania (TIC), Maulana Sheikh Hemed Jalala, ameungana na waumini katika zoezi la usafi lililofanyika Kigogo, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya shahada ya Imam Hussein (a.s) na kueneza ujumbe wa huduma kwa jamii.
-
Wapenzi wa Ahlul-Bayt (as) Washiriki Maandamano ya Amani ya Kuadhimisha Kumbukumbu ya Karbala Jijini Dar es Salaam +Picha
Waumini Wapenzi wa Ahlul-Bayt (a.s.), viongozi wa dini, wanasiasa, wafanyabiashara na watu mashuhuri wameungana katika maandamano ya amani jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhuisha kumbukumbu ya mauaji ya Karbala dhidi ya Imam Hussein (a.s.) na kusisitiza ujumbe wa haki, uadilifu na kupinga dhulma.
-
Majlisi ya Tano ya Imam Hussein (a.s) Iliyofanyika Mjini Moshi, Vijana Wahimizwa Kujifunza Mafunzo ya Karbala +Picha
Majlisi ya tano ya maombolezo ya Imam Hussein (a.s.) ilifanyika katika Msikiti wa Ahlul-Bayt (a.s) mjini Moshi, ambapo Khatibu Sheikh Dkt. Abdul Razaq Amir alizungumzia mada isemayo: “Vijana wanajifunza nini kutokana na Karbala?”
-
Malawi | Majlisi ya Tasu'a ya Imam Hussein (a.s) katika Hawzah ya Al-Hadi(as), Waumini Wakumbushwa Fadhila za Imam Hussein (a.s) na Abul-Fadhli+Picha
Majlisi ya maombolezo ya Tasu'a ya Imam Hussein (a.s) imefanyika katika Msikiti wa Hawzah ya Al-Hadi(as), ambapo wanafunzi, walimu na baadhi ya wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s) walikusanyika kuhuisha kumbukumbu za Karbala na kujifunza kuhusu nafasi ya Imam Hussein (a.s) na Abul-Fadhli al-Abbas (a.s) katika historia ya Uislamu.
-
Majlisi ya Maombolezo ya Tasu'a ya Imam Hussein (a.s.) Yafanyika katika Hawzah ya Hazrat Zaynab (a.s) Jijini Dar es Salaam +Picha
Wanafunzi na walimu wa Hawzah ya Hazrat Zaynab (a.s.) iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam, wamefanya Majlisi ya maombolezo ya Tasu'a ya Imam Hussein (a.s.), iliyojumuisha hotuba, usomaji wa majonzi, Ziara ya Ashura, Ziara ya Waritha na Surah Yasin kwa lengo la kuhuisha kumbukumbu za Karbala na dhulma iliyowapata Ahlul-Bayt (a.s).
-
Wanafunzi wa Hawzat Ummul-Banin (a.s.) Wafanya Zoezi la Usafi wa Mazingira Kuadhimisha Kumbukumbu ya Imam Hussein (a.s.) Jijini Dar es Salaam +Picha
Wanafunzi wasichana wa Hawzat Ummul-Banin (a.s.) iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam, wamefanya zoezi la usafi wa mazingira kwa lengo la kuadhimisha kumbukumbu ya Imam Hussein (a.s.) na kuendeleza ujumbe wa Karbala wa marekebisho ya jamii, maadili mema na huduma kwa jamii.