-
Ziara ya Kitaaluma na Kiroho ya Dkt. Ali Taqavi kwa Walimu na Wanafunzi nchini Burundi + Picha
Dkt. Ali Taqavi, Rais wa Jamiat Al-Mustafa (s) Tanzania, ametembelea walimu na wanafunzi nchini Burundi katika ziara ya kikazi na kiroho. Katika ziara hiyo, alifanya mazungumzo na walimu pamoja na wanafunzi kuhusu masuala mbalimbali ya kielimu, hususan programu za masomo na malezi ya kiroho. Ziara hiyo imelenga kuimarisha uhusiano wa kielimu na kuboresha mifumo ya ufundishaji na malezi katika taasisi hiyo iliyopo chini ya Usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) ndani ya nchi hiyo (ya Burundi) inayopakana na Rwanda upande wa Kaskazini, na Tanzania upande wa Mashariki, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo upande wa Magharibi.
-
Matembezi ya Siku ya Quds ya Kimataifa - Iran +Picha
Shirika Ia Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Waislamu na watu wema duniani kote, leo hii - Ijumaa ya Mwisho wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan - wanahuisha Siku ya Kimataifa ya Quds kwa ajili ya kutetea Taifa la Palestina na Haki ya Wapalestina.
-
Wafungwa 86 Katika Mabadilishano Kati ya Serikali ya Syria na Vikundi vya Druze huko Suwayda
Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Yatangaza: Serikali ya Syria na jamii ya Duru katika mkoa wa Sweida zilibadilishana wafungwa (mateka) 86 Jumatano iliyopita, kama ilivyotangazwa na Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu.
-
Wanafunzi Wa Atabat Al-Abbasiya Waadhimisha Mwezi wa Ramadhan kwa kuendelea na Ratiba ya Usomaji wa Qur’an Tukufu katika Sura ya Pamoja+Picha
Kituo cha Masomo kwa Wanafunzi Afrika katika Atabat Al-Abbasiya kimeandaa hafla ya hitimisho la Qur’anil Tukufu katika Mwezi wa Ramadhan, ikiwaleta pamoja wanafunzi ili kuadhimisha Kikamilifu Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan kupitia kuisoma Qur’ani na kushiriki katika tafakari za kiroho na mafunzo ya Ramadan.
-
Jamiatul Mustafa - Tanzania | Kongamano la Kielimu Laangazia “Mkombozi Katika Mitazamo ya Dini” kama Tumaini la Ubinadamu +Picha
Wanazuoni, wasomi na viongozi wa dini mbalimbali wakutana jijini kujadili dhana ya Mkombozi kama kiungo cha pamoja cha imani na bishara ya mustakabali mwema wa wanadamu.
-
Waumini wa Shia Ithna Ashari Jijini Arusha Waadhimisha Mazazi ya Imam Mahdi (a.t.f.s) sambamba na kupandishwa kwa Bendera ya Labbaika ya Mahdi +Picha
Waumini wa Shia Ithna Ashari mkoani Arusha wameadhimisha Mazazi ya Imam Mahdi (a.t.f.s) katika Husseiniyyah ya Imam Ridha (a.s) chini ya uongozi wa Sheikh Maulid Hussein Sombi. Maadhimisho hayo yalipambwa na upandishaji wa bendera ya “Labbaika Ya Mahdi” kama ishara ya utii na mapenzi kwa Imam wa Zama.
-
Kondoa Yafanya Maadhimisho ya Mazazi ya Imam Mahdi (a.s), Sheikh Abdul-Latif Atoa Wito wa Kulinda Msingi wa Jamii +Picha
Mamia ya waumini wa Wilaya ya Kondoa, Dodoma, walikusanyika tarehe 04/02/2026 kuadhimisha Mazazi Matukufu ya Imam Mahdi (a.t.f.s). Khatibu wa Majlisi, Sheikh Abdul-Latif, aliwakumbusha Waislamu umuhimu wa kuwatambua na kuwatetea viongozi wao, akionya kuwa maadui hutumia njama kuvuruga mihimili ya jamii ili kuiharibu ustaarabu wake.
-
Moshi Yaadhimisha Kwa Kishindo Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (ATFS) – 15 Shaaban +Picha
Maadhimisho ya kuzaliwa kwa Imam Mahdi (a.t.f.s) yaliyoambatana na 15 Shaaban yalifanyika tarehe 04/02/2026 mjini Moshi, Tanzania, kwa kushirikisha waumini wengi. Khatibu, Samahat Sheikh Miraji Salim, alieleza kwa kina neema ya uwepo wa Imam Mahdi (a.t.f.s) kama Baqiyyatullah katika ardhi ya Mwenyezi Mungu, na akawahimiza waumini kujiandaa kiroho na kimaadili katika kumngojea kwa vitendo, si kwa maneno pekee.
-
Dodoma - Tanzania | Dar-ul-Muslimeen Primary School Yaadhimisha Kuzaliwa kwa Imam Muhammad al-Mahdi (a.s) +Picha
Shule ya Msingi Dar-ul-Muslimeen, Dodoma, imeadhimisha kuzaliwa kwa Imam Muhammad al-Mahdi (a.s) leo, siku ya 15 Sha’ban.
-
Shule ya Kuhifadhi Qur’ani Tukufu Zanzibar; Hatua Muhimu katika Kulea Kizazi cha Qur’ani chini ya Usimamizi wa Uwakilishi wa Jamiat AlMustafa Tanzania
Shule ya Kuhifadhi Qur’ani Tukufu Zanzibar inatambulika kama nguzo muhimu ya Qur’ani nchini Tanzania, na inatarajiwa (kwa msaada wa Mwenyezi Mungu) kuwa shughuli zake zitaendelea kupanuka na kutoa fursa kwa wanafunzi wengi zaidi kuwa walinzi wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu.
-
Darsa ya Akhlaq - Malawi | “Sheikh Abdulrashid Yusuf Awaelimisha Wanafunzi wa Al-Hadi Kuhusu Kujiandaa Dhidi ya Maadui wa Uislamu +Picha
Sheikh alieleza mbinu za maadui na wanyonyaji, akisema hutumia kanuni potofu ya kwamba “lengo huhalalisha njia”, hivyo hutumia njia zote mbaya ili kufikia malengo yao maovu.
-
Kikao cha Awali cha Mkutano wa Kimataifa wa Dhana ya Upinzani (Muqawama) wa Kiislamu katika Sayansi za Binadamu Kimefanyika Tanzania +Picha
Dr. Baqir Ali alisisitiza: Dhana ya upinzani katika fikra za Kiislamu – umuhimu wake katika tamaduni na fikra. Upinzani wa Kiislamu na uchumi – mchango wake katika maendeleo ya kiuchumi na kujitegemea kwa jamii.
-
Mwanafunzi wa Elimu Tukufu ya Dini na Umuhimu wa Kusali Sala Kwa Wakati Wake Maalum Ulioandikwa +Picha
Sala si mzigo, bali ni ufunguo wa mafanikio kiroho na kimaisha, na Mwanafunzi anayehuisha 'Sala Tano' za kila siku na akazifanyia pupa, huyo atakuwa ameunganisha baina ya mambo mawili: Kuitafuta Dunia na Kuitafuta Akhera.
-
Hadhara ya Maulidi ya Mtume (SAWW) Iliyofanyika Leo Tanzania
Miongoni mwa wageni wa heshima waliokuwepo ni Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania na Mufti wa Tanzania, Shehe Dk. Abubakar Zuberi, ambao walihudhuria tukio hilo kwa heshima na kutoa hotuba zao mbele ya umati wa waumini na wageni.
-
Uwepo wa Waliojeruhiwa katika Ghasia za Hivi Karibuni Iran katika Haram ya Imam Reza (a.s) mjini Mashhad +Picha
Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Takribani watu elfu moja waliojeruhiwa katika ghasia za hivi karibuni nchini Iran walitembelea haram tukufu ya Imam Reza (a.s) na kukutana na uongozi wa Astan Quds Razavi pamoja na mahujaji. Ziara hiyo ilifanyika katika hali ya kiroho, ambapo waliojeruhiwa walipata fursa ya kusalimiana na mahujaji na kushiriki katika dua na ibada katika haram ya Imam Reza (a.s).
-
Picha | Sherehe ya Maulidi ya Kuzaliwa kwa Imam Hussein (a.s) katika Msikiti wa Mashia mjini Yangon, Myanmar
Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-: Sherehe za Sikukuu za Sha‘baniyya na kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Imam Hussein (a.s), Hadhrat Abal-Fadhil Al-Abbas (a.s), na Imam Zaynul-A'bidin (a.s) zilifanyika kwa ushiriki wa Mashia na wapenzi wa Ahlul-Bayt (a.s) katika Msikiti wa Mji wa Yangon nchini Myanmar. Yangon inahesabiwa kuwa Mji mkubwa zaidi nchini Myanmar.
-
Kikao cha Kielimu Kuhusu 'Mbinu za Mafanikio ya Wanafunzi wa Hawza Katika Masomo' Chafanyika Jamiat Al-Mustafa (s) Dar es Salaam +Picha
Sheikh Abdul-Majid: "Mafanikio ya Mwanafunzi yanategemea sana upangaji mzuri wa mipango, kuweka malengo ya wazi, na kuwa na nidhamu ya kujisomea. Wanafunzi wanatakiwa kuweka vipaumbele katika majukumu yao na kupanga muda wa masomo kwa utaratibu ili kuongeza tija katika safari yao ya kielimu".
-
Ayatollah Khamenei Akutana na Familia za Mashahidi, Aisisitiza Thamani ya Damu Tukufu za Mashahidi na Sadaka yao kwa Taifa +Picha
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, amekutana na familia za mashahidi katika mkutano uliojaa heshima na hisia za kina, akithibitisha mshikamano wa uongozi wa Jamhuri ya Kiislamu na kuthamini sadaka na nafasi ya mashahidi pamoja na familia zao.
-
Maandamano ya Kitaifa Iran: Wananchi Waonesha Uzalendo na Kuiunga Mkono Serikali ya Kiislamu +Picha
Wananchi wa Iran wamefanya maandamano ya amani kote nchini kuadhimisha Dey 9, wakionyesha mshikamano wa kitaifa na uungaji mkono wao kwa serikali ya Kiislamu chini ya uongozi wa Ayatollah Ali Khamenei, huku wakikataa propaganda na njama za maadui wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Afrika Mashariki Yaaga Mwanachuoni Mkubwa: Mazishi ya Sheikh Ali Jumaa Mayunga Yafanyika Jijini Dar es Salaam +Picha
Kwa kuondokewa na Sheikh Ali Jumaa Mayunga, jamii ya Kiislamu Afrika Mashariki imepoteza hazina kubwa ya elimu na hekima. Hata hivyo, elimu yake, maandiko yake na athari zake zitaendelea kuishi na kuwanufaisha vizazi vijavyo, kama sadaka jariya isiyokatika matunda yake. Mwenyezi Mungu amsamehe madhambi yake, ampanulie kaburi lake, na amjaalie daraja za juu katika Pepo pamoja na waja Wake wema.
-
Hafla ya Kutimiza Maonyesho ya Orchestra ya "Iranmard" kwa Heshima ya Askari Qasem Soleimani +Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Hafla ya kutimiza maonyesho ya Orchestra ya Iranmard, iliyopangwa kuenzi kumbukumbu ya askari shujaa wa Uislamu, Marehemu Jenerali Qasem Soleimani, kwa mtazamo wa kuhifadhi utambulisho wa taifa, kujitolea, na mshikamano wa kitamaduni, ilifanyika asubuhi ya siku Jumanne (30 Desewmba, 2025) katika Ukumbi wa Vahdat. Katika sherehe hii, Seyed Abbas Salehi, Waziri wa Utamaduni na Elimu ya Sanaa ya Uislamu, alikuwa miongoni mwa waliohudhuria na kutoa hotuba.
-
Maadhimisho Makubwa ya Siku ya Mwenyezi Mungu (Yawmullah) 9 Dey (30 Desemba) huko Isfahan +Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Hafla ya maadhimisho ya Siku ya Mwenyezi Mungu (Yawmullah) 9 Dey (30 Desemba), iliyojikita katika kuimarisha uelewa (basira) na kulinda thamani za Mapinduzi ya Kiislamu, ilifanyika leo asubuhi, Jumanne, kwa ushiriki mkubwa wa wananchi wa mapinduzi pamoja na viongozi na maafisa, katika Uwanja wa Mapinduzi (Meydan-e Enqelab) jijini Isfahan.
-
Mkutano wa Diplomasia na Muqawama katika Msingi wa Shule ya Haji Qasem SoleimanI
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Mkutano wa Kimataifa wa Diplomasia na Muqawama katika Shule ya HajI Qasem ulifanyika kwa mnasaba wa maadhimisho ya miaka sita tangu kuuawa shahidi Luteni Jenerali Haj Qasem Soleimani, siku ya Jumatatu tarehe 29 Desemba 2025, kwa ushiriki wa Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje, pamoja na idadi ya viongozi waandamizi wa kisiasa, wataalamu wa taasisi za utafiti (think tanks), na wasomi wa vyuo vikuu. Mkutano huo ulifanyika katika Kituo cha Tafiti za Kisiasa na Kimataifa cha Wizara ya Mambo ya Nje.
-
Kundi la Handala Ladai Kudukua Taarifa Nyeti Katika Simu ya Mkuu wa Ofisi ya Netanyahu na Kufichua Nyaraka Zenye Usiri Mkubwa +Picha
Handala hivi karibuni pia walidukua simu ya waziri mkuu wa zamani wa Israel, Naftali Bennett, na kutoa nyaraka na picha za kiongozi huyo, hatua inayoongeza wasiwasi kuhusu usalama wa mawasiliano ya viongozi wa Israel.
-
Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano la Kumuenzi Ayatollah Sayyid Mohammad Hadi Milani Wakutana na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu +Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Wajumbe wa kamati ya maandalizi ya kongamano la kumbukumbu kwa heshima ya Ayatollah Sayyid Mohammad Hadi Milani wamekutana na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, ambapo walijadili umuhimu wa kongamano hilo katika kuhifadhi na kuendeleza urithi wa kielimu, kidini na kijamii wa mwanazuoni huyo mashuhuri.
-
Marasimu ya Kumbukumbu ya Ayatullah Sayyid Muhammad Shahcheraghi huko Qom +Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Marasimu ya kumbukumbu ya Marehemu Ayatullah Sayyid Muhammad Shahcheraghi, aliyekuwa mwakilishi wa awali wa Wilayat al-Faqih na Imam wa Ijumaa wa zamani wa Semnan, ilifanyika Jumapili, 22 Desemba 2025 baada ya Sala ya Magharibi na Isha, katika Msikiti wa Imam Hasan Askari (A.S), kwa kuhudhuriwa na waalimu, viongozi mbalimbali wa kijamii, na makundi tofauti ya wananchi.
-
Kongamano la Kiislamu Kibaha Latoa Mafunzo ya Kina juu ya Uislamu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) +Picha
Kongamano hilo limeelezwa kuwa ni hatua muhimu ya kuimarisha uamsho wa kielimu na kiroho, huku Waandaji wakiahidi kuendelea kuratibu programu kama hizi ili kuendeleza malezi bora ya Kiislamu na kuimarisha umoja miongoni mwa Waumini.
-
Falah Islamic Development Yaendesha Kikao Maalumu cha Elimu ya Afya Kuhusu Hepatitis B na Umuhimu wa Chanjo
Kwa ujumla, kikao hicho kilikuwa cha kuelimisha, kuvutia na chenye athari chanya, kikiwapa washiriki maarifa sahihi ya kitabibu pamoja na hamasa ya kuchukua hatua za kinga kwa ajili ya kulinda afya zao, familia zao na jamii kwa ujumla. Falah Islamic Development ilipongezwa kwa mchango wake katika kuhamasisha elimu ya afya na ustawi wa jamii.
-
Malawi | Hafla ya Usomaji wa Qur’an Tukufu +Picha
Hafla hii ya kiroho imehudhuriwa na talaba / Wanafunzi pamoja na walimu wa Hawza na inalenga kukuza maadili ya Kiislamu, kuimarisha ibada, na kuongeza mapenzi na mshikamano kupitia kukaa pamoja chini ya kivuli cha Qur’ani Tukufu.
-
Taasisi ya Furqan Foundation yafungua Kisima cha Maji Namba 8 Katika Kijiji cha Mgomba, Ikwiriri, Rufiji +Picha
Taasisi ya Furqan Foundation imetoa shukrani za dhati kwa wafadhili waliowezesha mradi huu, na pia imetoa wito kwa wanakijiji kutunza na kusimamia kisima hiki, ili mradi huo uendelee kutoa manufaa ya muda mrefu na kuondoa adha ya ukosefu wa maji kama ilivyokuwa awali.