ABNA swahili
  • HABARI KAMILI
  • HABARI MUHIMU
  • Iran
  • ASIA
  • ULAYA
  • AMERIKA
  • AFRIKA
  • PICHA
  • MAKALA
العربية English فارسی Türkçe اردو Español bahasa Indonesia हिन्दी français 汉语 русский Deutsch Melayu Hausa বাংলা Азәрбајҹан Азәрбајҹан әлифбасы Kiswahili မြန်မာဘာသာ bosanski português سورانی 日本語 Kurmancî Pilipinas Тоҷик italiano 한국어
×
filterToday News
  • Nchini Burundi | Mimbari ya Imam Hussein(as) inamtambua Hussein(as) kama  ishara ya ujasiri, uadilifu, uhuru na upinzani dhidi ya Dhulma na Uistikbari

    Nchini Burundi | Mimbari ya Imam Hussein(as) inamtambua Hussein(as) kama ishara ya ujasiri, uadilifu, uhuru na upinzani dhidi ya Dhulma na Uistikbari

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majlisi (Vikao) mbalimbali vya Maombolezo ya Shahada ya Imam Hussein (as) vinaendelea nchini Burundi, ambapo Imam Hussein (as) anazungumziwa katika eneo hilo na duniani kote kwa ujumla kuwa: Yeye ni ishara ya ujasiri, uadilifu, uhuru na upinzani dhidi ya dhulma na uistikbari. Yeye ndiye kielelezo cha dhabihu na kujitolea kwa ajili ya maadili bora ya kibinadamu.

    2025-07-01 18:49
  • Muharram - 1447H, Arusha - Tanzania | Imam Hussein (as) hakuchagua Kifo bali alichagua Haki hata kama Haki hiyo itagharimu Maisha yake

    Muharram - 1447H, Arusha - Tanzania | Imam Hussein (as) hakuchagua Kifo bali alichagua Haki hata kama Haki hiyo itagharimu Maisha yake

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majlis mbalimbali zinaendelea katika Husseiniyya Jijini Arusha katika kuomboleza na kutoa masomo mbalimbali juu ya malengo ya harakati ya kimapinduzi ya Imam Hussein (as) aliyoifanya katika Ardhi ya Karbala, Mapinduzi ambayo hadi leo hii yanaendelea kutoa matunda yake mazuri kwa walimwengu wote, hususan kwa ulimwengu wa Kiislamu. Waumini mbalimbali wanajitokea katika Majalis hizi kwa ajili ya kujifunza masomo mbalimbali yaliyomo katika Mapinduzi ya Karbala yaliyoongozwa na Imam Hussein (as), Mjukuu Kipenzi wa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).

    2025-07-01 18:34
  • Mimbari ya Imam Hussein (as), Arusha- Tanzania | "Mapinduzi ya Haki ya Imam Hussein (as) dhidi ya Batili ya Muovu Yazid bin Muawiya"

    Mimbari ya Imam Hussein (as), Arusha- Tanzania | "Mapinduzi ya Haki ya Imam Hussein (as) dhidi ya Batili ya Muovu Yazid bin Muawiya"

    Shirika la Habari la Kimatifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majalis za Muharram zinaendelea katika mimbari mbalimbali za Imam Hussein (as) katika Jiji la Arusha. Waumini wengi wanajitokeza kutoka maeneo mbalimbali na kushiriki katika Vikao vya Kielimu kuhusiana na Mapinduzi ya Kiislamu ya Imam Hussein (as) katika Ardhi ya Karbala. Katika picha ni Majlisi ya Darsa kuhusiana na Mapinduzi ya Karbala, waumini wa Kiislamu wakiwa katika mkao wa kusikiliza historia ya Mapinduzi ya Haki ya Imam Hussein (as) dhidi ya Batili ya Yazid bin Muawiya(la), ikiwa ni mada iliyotolewa na Samahat Sheikh Bashir Bar'wan katika Husseiniyya ya Ahlul-Bayt (as) Jijini Arusha - Tanzania.

    2025-07-01 18:22
  • Majalis za Muharram na Maombolezo ya A'shura Zinaendelea kila Siku katika vituo vya Taasisi ya Kiislamu ya S.D.O Bukoba - Tanzania + Picha na Video

    Majalis za Muharram na Maombolezo ya A'shura Zinaendelea kila Siku katika vituo vya Taasisi ya Kiislamu ya S.D.O Bukoba - Tanzania + Picha na Video

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-Majalis za Muharram Zinaendelea kufanyika katika Mji wa Bukoba kwenye vituo vya Taasisi ya Kiislamu ya S.D.O ambavyo ni: Nshambya Center - Bukoba Mjini, Kemondo, Katobago, Muleba n.k). Majlisi hizi zinaendelea kwa muda wa Siku 12 za Mwezi wa Muharram katika kuhuisha Mapinduzi ya Imam Hussein (as) na kutoa mafunzo mbalimbali kwa Jamii ya Kiislamu yaliyomo ndani ya Harakati ya kihistoria ya Imam Hussein (as) iliyotengeneza Mapinduzi Makubwa yanayoendelea kutoa matunda yake hadi Leo hii.

    2025-06-29 23:58
  • Majlisi ya 2 Maombolezo ya Muharram | Katika Chuo cha Mabinti cha Hazrat Zainab (SA), Kigamboni - Dar-es-salaam+ Picha

    Majlisi ya 2 Maombolezo ya Muharram | Katika Chuo cha Mabinti cha Hazrat Zainab (SA), Kigamboni - Dar-es-salaam+ Picha

    Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majalis za Maombolezo na Kumbukumbu ya Shahada ya Ava Abdillah Al_Hussein (as), zinaendelea kila Siku katika Mwezi huu Mtukufu wa Muharram katika Madarasa ya Hazrat Zainab (sa) Kigamboni- Dar-es-salaam.

    2025-06-28 21:29
  • Majalis (Vikao) vya Kuadhimisha Shahada ya Imam Hussein (AS) katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa   - Dar-es-salaam - Tanzania + Picha

    Majalis (Vikao) vya Kuadhimisha Shahada ya Imam Hussein (AS) katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa - Dar-es-salaam - Tanzania + Picha

    Majalis / Vikao hivi vitaendelea kutoa fursa ya kutafakari kuhusu ujumbe wa A'shura kwa Wanafunzi na jamii ya kielimu bali Umma mzima wa Kiislamu wenye kiu kubwa ya kujua ukweli na uhakika, na kufuata Haki na Uadilifu.

    2025-06-28 21:07
  • Ripoti ya Picha | Mazishi ya Shahidi Kanali Mehdi Rezazadeh, mlinzi wa Taifa, huko Tabriz

    Ripoti ya Picha | Mazishi ya Shahidi Kanali Mehdi Rezazadeh, mlinzi wa Taifa, huko Tabriz

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as_ -ABNA- Hafla ya mazishi ya mlinzi aliyeuawa shahidi wa nchi hiyo, Kanali Mehdi Rezazadeh, shahidi wa kitengo maalum cha jeshi la polisi la mkoa wa Azerbaijan Mashariki aliyeuawa shahidi katika mashambulizi ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni huko Tabriz, ilifanyika kuanzia Msikiti wa Imam Khomeini hadi uwanja wa Saa wa Tabriz baada ya kuswaliwa swala ya kuuombea mwili wa shahidi huyo. Mazishi yalifanyika na watu wa Tabriz's Shahid Parvar.

    2025-06-28 18:15
  • Majlisi ya Kwanza ya Muharram - Husseiniyyah ya Imam Mahdi (as) + Picha

    Majlisi ya Kwanza ya Muharram - Husseiniyyah ya Imam Mahdi (as) + Picha

    Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) - Majlisi za Muharram katika kuomboleza Kifo cha Kishahidi cha Imam Hussein (as) zimeanza Leo Nchini Tanzania. Moja ya Husseiniyyah zilizohuisha Siku ya Kwanza ya Muharram ni Husseiniyyah ya Imam Mahdi (as) Tabora - Tanzania.

    2025-06-27 00:01
  • Dua ya Kumail | Hawzat Hazrat Zainab (SA) _ Kigamboni - Dar-es-salaam

    Dua ya Kumail | Hawzat Hazrat Zainab (SA) _ Kigamboni - Dar-es-salaam

    Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) - Leo hii Dua adhimu ya Kumail Bin Ziyad imesemwa na Wanafunzi wa Madrasat ya Mabinti ya Hazrat Zainab (SA) - iliyopo Kigamboni Jijini Dar-es-salaam - Tanzania.

    2025-06-26 23:46
  • Israel yashuhudia nguvu kubwa ya Iran kwenye uwanja wa vita | Picha zinaonyesha jinsi ilivyogeuzwa kuwa ardhi ya magofu + Picha

    Israel yashuhudia nguvu kubwa ya Iran kwenye uwanja wa vita | Picha zinaonyesha jinsi ilivyogeuzwa kuwa ardhi ya magofu + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - Baada ya Iran kuachia wimbi la 20 la mashambulizi ya makombora kuelekea utawala ghasibu wa Israel, maeneo yote yoliyolengwa kwenye shabaha yageuzwa kuwa majivu.

    2025-06-22 16:05
  • Ripoti ya Picha | Sherehe ya Eid Ghadir na Kuvalisha Vilemba Wanafunzi wa Kishia Mjini Kabul

    Ripoti ya Picha | Sherehe ya Eid Ghadir na Kuvalisha Vilemba Wanafunzi wa Kishia Mjini Kabul

    Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul Bayt (A.S.) - ABNA - Sherehe ya Eid Ghadir imefanyika mbele ya maprofesa, wanafunzi na makundi mbalimbali ya watu katika Seminari ya Kielimu ya Maimamu Watukufu (Amani iwe juu yao) mjini Kabul. Pia, katika siku hii yenye baraka, idadi ya wanafunzi wa seminari hii walitawazwa kwa kuvishwa Vilemba vya Kielimu kupitia Mikono ya Maprofesa na Viongozi Wakubwa wa Seminari ya Kabul.

    2025-06-15 17:17
  • Mkusanyiko wa Wananchi wa Mji wa Isfahan - Iran katika kusapoti Operesheni ya Kijeshi ya Iran ya "Ahadi ya Kweli_3" + Picha

    Mkusanyiko wa Wananchi wa Mji wa Isfahan - Iran katika kusapoti Operesheni ya Kijeshi ya Iran ya "Ahadi ya Kweli_3" + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Wananchi wengi wa Isfahan kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa huu wamekusanyika katika uwanja wa Imam Hussein (as) uliopo katika Mji wa Isfahan kwa ajili ya kuonyesha sapoti yao na kushukuru Iran kwa sababu ya Operesheni yake ya kijeshi ya "Ahadi ya Kweli - 3" dhidi ya Utawala haram wa Kizayuni.

    2025-06-15 15:34
  • Ripoti ya Picha | Hafla ya Usiku wa Sikukuu ya Ghadir na Kulaani Jinai za Utawala Batili wa Kizayuni huko Rasht

    Ripoti ya Picha | Hafla ya Usiku wa Sikukuu ya Ghadir na Kulaani Jinai za Utawala Batili wa Kizayuni huko Rasht

    Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlulbayt (a.s) -ABNA- Hafla ya usiku wa Sikukuu ya Ghadir Khum pamoja na kulaani jinai za utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilifanyika katika Msikiti wa Imam Ridha (a.s) eneo la Golsar mjini Rasht.

    2025-06-14 23:18
  • Siku ya Pili ya Mitihani ya Mwisho wa Muhula wa Kwanza katika Shule ya Imam Zayn al-‘Abidin (A.S) – Burundi + Picha

    Siku ya Pili ya Mitihani ya Mwisho wa Muhula wa Kwanza katika Shule ya Imam Zayn al-‘Abidin (A.S) – Burundi + Picha

    Masomo waliyofanyia mitihani ni kama yafuatayo: 1_Vyanzo vya Sunna Tukufu. 2_Misingi ya Lugha ya Kiarabu (مبادئ العربية) – Sehemu ya 2 (Nahau).

    2025-06-11 11:57
  • Waumini walivyoshiriki kwa wingi katika kisomo cha Dua ya Araf - Katika Chuo cha Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam + Picha

    Waumini walivyoshiriki kwa wingi katika kisomo cha Dua ya Araf - Katika Chuo cha Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Katika sehemu ya Dua hiyo iliyopokelewa kutoka kwa Imam Hussein (as) - tunasoma kipengele hiki ambapo Imam Hussein (as) alisema akielezea sehemu ya Neema za Mwenyezi Mungu kwa Waja wake: أَنْتَ الَّذِي مَنَنْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَنْعَمْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَحْسَنْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَجْمَلْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَفْضَلْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَكْمَلْتَ، أَنْتَ الَّذِي رَزَقْتَ، أَنْتَ الَّذِي وَفَّقْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَعْطَيْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَغْنَيْتَ، أَنْتَ الَّذِي أَقْنَيْتَ

    2025-06-09 22:58
  • Khutba ya Eid al-Adh'ha Singida | Shekh Fakhari Ally Sakilu: Umuhimu wa Malezi ya Vijana dhidi ya Mmomonyoko wa Maadili + Picha

    Khutba ya Eid al-Adh'ha Singida | Shekh Fakhari Ally Sakilu: Umuhimu wa Malezi ya Vijana dhidi ya Mmomonyoko wa Maadili + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Khutba ya Eidul Adh'ha ilisoliwa katika maeneo ya Uhamaka Singida Mjini. Khatibu wa Sala ya Eid: Shekh Fakhari Ally Sakilu Ambaye alizungumzia: Umuhimu wa Malezi ya vijana dhidi ya mmomonyoko wa maadili.

    2025-06-09 22:16
  • Mwanza , Wilayat ya Kwimba - Kituo kipya cha Kishiachini ya Taasisi ya Al-Hussein Foundation - Arusha kimefunguliwa 8 Juni, 2025 + Picha

    Mwanza , Wilayat ya Kwimba - Kituo kipya cha Kishiachini ya Taasisi ya Al-Hussein Foundation - Arusha kimefunguliwa 8 Juni, 2025 + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Kituo kipya cha Shia kimefunguliwa Jana katika Wilayat ya Kwimba Jijini Mwanza. Katika Picha pia anaonekana Ndugu Dhulfiqal Ally akikabidhi kalenda 25 mpya za Mwaka 1447 hijiria katika Hafla ya Ufunguzi wa Msikiti Ngudu. Kalenda hizo ni zawadi kwa Waumini kutoka katika taasisi ya The Desk and Chair foundation chini ya Alhaj Sibtain Meghjee.

    2025-06-09 21:04
  • Kiongozi Muadhamu Ayatollah Khamenei Aongoza Maadhimisho ya Miaka 36 ya Kifo cha Imam Khomeini (MA) + Picha

    Kiongozi Muadhamu Ayatollah Khamenei Aongoza Maadhimisho ya Miaka 36 ya Kifo cha Imam Khomeini (MA) + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei katika hafla ya kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 36 tangu kufariki kwa Imam Khomeini.

    2025-06-04 13:55
  • Habari Pichani | Haram ya Imam Ali (a.s) imefunikwa kwa rangi nyeusi kufuatia kumbukumbu ya Shahada ya Imam Baqir (a.s)

    Habari Pichani | Haram ya Imam Ali (a.s) imefunikwa kwa rangi nyeusi kufuatia kumbukumbu ya Shahada ya Imam Baqir (a.s)

    Kulingana na Ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul Bayt (a.s) -ABNA- Maeneo yote ya Haram Tukufu ya Imam Ali (as) yamefunikwa kwa rangi nyeusi kuadhimisha kumbukumbu ya Shahada ya Imam Muhammad Baqir (as) pamoja na Muslim bin Aqil (as). Hii ni ishara ya maombolezo na heshima kutoka kwa wafuasi wa Madhehebu ya Shi'a kwa Imam huyo Mtoharifu.

    2025-06-03 16:54
  • Majlisi ya Kumbukumbu ya Shahada ya Imam al-Jawad (A.S.) Yafanyika katika Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zainab (sa), Kigamboni - Dar es Salaam + Picha

    Majlisi ya Kumbukumbu ya Shahada ya Imam al-Jawad (A.S.) Yafanyika katika Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zainab (sa), Kigamboni - Dar es Salaam + Picha

    Katika kumbukumbu ya siku ya kuuawa Shahidi kwa Imam Muhammad al-Jawad (A.S.), Mkurugenzi wa Shule hii ya Mabanati, alitoa Hotuba Maridhawa, ambapo alizungumzia mambo yafuatayo: Alianza kwa kutaja siku ya kuzaliwa kwa Imam al-Jawad (A.S.) na sifa maalumu za Imam huyo wa tisa, namna alivyopata shahada, pamoja na hadithi mbalimbali na nzuri zilizopokelewa kutoka kwake.

    2025-05-27 18:32
  • Burundi | Maombolezo ya Kuuawa Shahidi kwa Imam Muhammad Al-Jawad (A.S) Yafanyika kwa Hisia Kubwa

    Burundi | Maombolezo ya Kuuawa Shahidi kwa Imam Muhammad Al-Jawad (A.S) Yafanyika kwa Hisia Kubwa

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (A.S) - ABNA- Limeripoti kufanyika kwa Majlisi ya Maombolezo ya Shahadat ya Imam Jawad (as) yenye hisia kubwa nchini Burundi.

    2025-05-27 17:53
  • Habari Pichani | Uwasili wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) Katika Mji Mkuu wa Niger

    Habari Pichani | Uwasili wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) Katika Mji Mkuu wa Niger

    Kwa mujibu ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul Bayt (a.s) –ABNA– Ayatollah "Ramezani" Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s), alisafiri kwenda nchi ya Niger, Magharibi mwa Bara la Afrika, kwa mwaliko wa Viongozi wa Dini wa nchi hiyo. Uwanja wa ndege wa Mji wa Niamey, viongozi wa Dini wa Niger walimkaribisha Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s).

    2025-05-27 17:06
  • Masomo ya Qur'an kupitia Khatamul Anbiyaa, Arusha - Tanzania | Qur'an: Sauti - Lahni - Hifdhi na Tafsiri ya Qur'an

    Masomo ya Qur'an kupitia Khatamul Anbiyaa, Arusha - Tanzania | Qur'an: Sauti - Lahni - Hifdhi na Tafsiri ya Qur'an

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - Soma Qur'an kupitia Chuo cha: Khatamul Anbiyaa, Arusha - Tanzania. Utapa masomo ya Qur'an yafuatayo: Qur'an - Hifdhi - Qiraat Sauti - lahni - mafahim - tadaburi- tafsiri. Mwalimu: Ustadhi M.Ridha Dosa.

    2025-05-27 10:28
  • Semina ya Kila Alkhamisi | Falah Islamic Foundation Zanzibar

    Semina ya Kila Alkhamisi | Falah Islamic Foundation Zanzibar

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Falah Islamic foundation Zanzibar - Tarehe 22/5/2025 - Katika Muendelezo wa semina za kila alkhamis kwa vijana juu ya Mada: Ushirikiano kati ya mwanamke na Mwanamme. Mtoa mada Sheikh Baqir.

    2025-05-27 09:35
  • Mazungumzo ya Iran na Pakistan | Yafanyika Jijini Tehran

    Mazungumzo ya Iran na Pakistan | Yafanyika Jijini Tehran

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, na Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, walikutana na kufanya mazungumzo mjini Tehran siku ya Jumatatu.

    2025-05-26 23:58
  • Kongamano Kubwa la Qur'an Lafanyika kwa Mafanikio Makubwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam + Picha

    Kongamano Kubwa la Qur'an Lafanyika kwa Mafanikio Makubwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam + Picha

    Tukio hili lilikuwa kiashiria cha wazi kuwa Qur’an ni kitovu cha mshikamano, upendo, na amani siyo tu miongoni mwa Waislamu, bali pia kwa jamii nzima ya kitaifa na kimataifa.

    2025-05-25 18:41
  • Maajabu | Kongamano kubwa la Qur'an Tukufu: Mji wa Tanga Wazizima

    Maajabu | Kongamano kubwa la Qur'an Tukufu: Mji wa Tanga Wazizima

    Kishindo... Kishindo ... Kongamano kubwa la usomaji wa Qur-ani kwa Tajweed latikisa Jijini la Tanga.

    2025-05-24 18:38
  • Watazamaji Katika Kongamano la Qur’an Tukufu Wafurika katika Uwanja wa Mkwakwani Tanga; Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mh. Balozi Dkt. Batilda Burian Apongeza

    Watazamaji Katika Kongamano la Qur’an Tukufu Wafurika katika Uwanja wa Mkwakwani Tanga; Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mh. Balozi Dkt. Batilda Burian Apongeza

    Kwa Mujibu wa Ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Jiji la Tanga, Tanzania – Uwanja wa Michezo wa Mkwakwani umefurika watu kutoka kila kona ya Mkoa wa Tanga na nje ya Tanga, ili kushiriki kwa kwa kuona kwa macho na kusikiliza kwa masikio yao Qur'an Tukufu ikisomwa kwa njia ya Tajweed katika Kongamano la Qur’an Tukufu lililofanyika leo hii katika Uwanja huo. Kongamano hili lilihudhuriwa na wasomaji bingwa wa Tajweed kutoka nchini Iran na ndani ya Tanzania, ambapo walitoa usomaji mzuri wa Qur’an Tukufu ulioleta msisimko mkubwa miongoni mwa hadhira.

    2025-05-24 18:36
  • Tanga Yawakutanisha Viongozi wa Kitaifa na Kimataifa Katika Kongamano la Qur'an Tukufu + Picha

    Tanga Yawakutanisha Viongozi wa Kitaifa na Kimataifa Katika Kongamano la Qur'an Tukufu + Picha

    Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian (aliyevaa Hijab na Mtandio Mweusi), akiwa katika picha ya pamoja na Mheshimiwa Balozi wa Iran Nchini Tanzania, Mwenyekiti wa Jumuia ya Maridhiano na Amani (JMAT-TAIFA), Sheikh Dkt. Al-Had Mussa Salum, Rais wa Chuo cha Kimataifa cha Al-Mustafa (s) - Tanzania, Hujjatul-Islam wal Muslimin, Dkt. Ali Taqavi, Mkurugenzi wa Kitengo cha Utamaduni wa Iran, Dkt. Maarifi, Sheikh Mkuu wa Jumuia ya Shia Ithna Ashari Tanzania, Maulana Sheikh Hemed Jalala, na viongozi mbalimbali waliohudhuria katika Kongamano la Qur'an Tukufu lililofanyika leo hii Jijini Tanga - Tanzania katika uwanja wa Michezo wa Mkwakwani ili kusikiliza Kisomo cha Qur'an Tukufu kikisomwa na wasomaji bingwa wa Tajweed kutoka nchini Iran na ndani ya Tanzania.

    2025-05-24 17:21
  • Habari Pichani: Makumbusho ya Nelson Mandela yaandaa Siku ya Kwanza ya Maadhimisho ya Siku ya Afrika kwa Heshima ya Palestina

    Habari Pichani: Makumbusho ya Nelson Mandela yaandaa Siku ya Kwanza ya Maadhimisho ya Siku ya Afrika kwa Heshima ya Palestina

    Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (ABNA): Makumbusho ya Nelson Mandela yamezindua siku ya kwanza ya Maadhimisho ya Siku ya Afrika kwa kutoa heshima ya kipekee kwa Palestina na kwa watu wote wanaodhulumiwa, chini ya kaulimbiu: “Mkutano wa Mshikamano na Palestina.”

    2025-05-24 15:37
  • Previous
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • Next
Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (a.s); Abna Sauti ya Mashia wasio na Vyombo vya Habari.
Desktop version Mobile version

Nukuu ya "Maudhui" inaruhusiwa bila kutaja chanzo

Nastooh Saba Newsroom