Ndege ya kijeshi ya Jeshi la Marekani maalumu kabisa kwa kubeba wahanga wa jeshi lake imeonekana ikitoka nchini Iraq na kuelekea Ujerumani.
Taarifa picha za sattelite zinaashiria kwamba ndege hiyo aina ya BNDGE53 iliruka kutokea uwanja wa ndege wa Baghdad na kutua katika uwanja wa ndege mjini Ramstein Ujerumani.
Inaaminika kwamba eneo la Ramstein Kusini mwa Ujerumani kuna kambi kubwa ya Marekani ambayo inajitosheleza kwa kila aina ya matibabu, na hata wahanga na majeruhi wa mapambano yanayotokea Magharibi mwa Asia na hata Afrika hupelekwa huko kwa matibabu.