Main Title

source : ParsToday
Jumapili

19 Januari 2020

10:20:24
1003615

Timu za Iran zajitoa kwenye mashindano ya soka ya mabingwa wa Asia kulalamikia uamuzi wa kisiasa wa AFC

Timu za Esteqhlal, Perspolis, Sepahan na Shahre-Khodroo zinazoiwakilisha Iran katika mashindano ya mabingwa wa soka wa Asia katika mwaka huu wa 2020 zimeamua kujitoa kwenye mashindano hayo kulalamikia uamuzi wa kisiasa uliochukuliwa na Shirikisho la Soka la Asia (AFC) wa kuzitaka timu hizo zicheze michezo yao yote katika nchi ngeni ya tatu.

(ABNA24.com) Timu hizo zimetangaza uamuzi huo leo na kusisitiza katika taarifa yao kwamba: Hazitatii uamuzi huo wa kiuonevu uliochanganyika na matashi ya kipropaganda dhidi ya hali ya usalama ya Iran.

Katika barua kwa Shirikisho la Soka la Iran, Shirikisho la Soka la Asia limetangaza kuwa, kamati ya utendaji ya shirikisho hilo inakusudia kuandaa mechi za timu za Iran na washindani wao katika nchi isiyoelemea upande wowote.

Kisingizio kilichotumiwa na Shirikisho la Soka la Asia kuchukua uamuzi huo wa kiafriti ni kutokuwepo amani na usalama nchini Iran.

..........
340