Main Title

source : ParsToday
Jumatano

5 Februari 2020

08:22:10
1008029

Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, adui ameondoa mezani chaguo la kufanya mazungumzo baada ya Marekani kumuua shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) sambamba na Iran kutoa jibu kali kwa ugaidi huo wa Washington.

(ABNA24.com) Brigedia Jenerali Amir Hatami amesema hayo Jumanne hapa jijini Tehran na kufafanua kuwa, adui huko nyuma alikuwa akizungumza kwa majivuno kuhusu machaguo yake yaliko mezani hususan chaguo la kijeshi lakini hii leo, amefyata mdomo.

Amesema Marekani ilitekeleza na kukiri wazi wazi kuwa imefanya ugaidi wa kumuua Jenerali Soleimani, na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilitoa majibu mawili kwa chokochoko hizo; mosi jibu laini ambapo wananchi wa Iran walijitokeza kwa mamilioni katika kuuaga na kuuenzi mwili wa Shujaa huyo, na pili kwa jeshi la SEPAH kupiga kwa makombora kambi za kijeshi za Marekani nchini Iraq.

Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, "taifa hili halina haja ya kusema litachukua hatua gani iwapo maadui watafanya kosa, wenyewe wanafahamu vyema."

Brigedia Jenerali Amir Hatami ameongeza kuwa, katika hali ambayo adui hivi sasa anazungumza kuhusu mashinikizo ya juu ili kupunguza nguvu za Iran, lakini taifa hili linaendelea kuimarika na kuwa na uwezo mkubwa siku baada ya siku.

Ameeleza bayana kuwa, Iran imepiga hatua katika nyuga za nishati ya nyuklia, mafuta na uundaji magari na ndiposa maadui hivi sasa wanazuia chakula na dawa kuingia nchini ili kutoa pigo kwa wananchi wa Iran.

...........
340