Kwa mujibu wa tovuti huru ya habari Al-Watan, maafisa hao wanane wa zamani wa Jeshi la Wanamaji la India waliajiriwa na kampuni binafsi nchini Qatar iitwayo Dahra Global Technology and Consulting Services, ambayo hutoa mafunzo na huduma zikiwemo za usaidizi na matengenezo ya vifaa kwa Jeshi la Wanamaji la Qatar. Tovuti ya Al-Watan imeripoti kuwa, mashtaka yanayohusishwa dhidi ya maafisa hao wa zamani wa jeshi la wanamaji la India bado hayajajulikana, lakini taarifa zilizofichuliwa zinaonyesha kuwa watu hao wamekuwa wakifanya ujasusi kwa manufaa ya utawala haramu wa Israel.Kulingana na ripoti hiyo, mnamo mwishoni mwa mwezi Septemba, serikali ya Doha iliwaruhusu maafisa hao wa zamani wa jeshi la wanamaji la India waliokamatwa kupiga simu kwa familia zao.
342/