Julia Black, ripota wa Shirika la Kimataifa la Uhajiri, ameeleza kuwa, tangu ilipoanza "Kampeni ya Wahajiri Waliotoweka" mnamo mwaka 2014 na licha ya kuongezeka idadi ya watu wanaofariki dunia katika hekaheka za uhajiri, serikali zimechukua hatua chache za kuchunguza na kushughulikia maafa ya kimataifa ya wahajiri wanaotoweka bila kujulikana hatima yao. Ripota huyo wa Shirika la Kimataifa la Uhajiri ameongeza kuwa: wakati maelfu ya vifo vinavyotokea katika njia zinazotumiwa na wahajiri vinasajiliwa kila mwaka, ni hatua chache sana zimechukuliwa kuchunguza madhara yanayosababishwa na majanga hayo, seuze kuyazuia!Kulingana na ripoti hiyo ya ripota wa ILO, utambulisho na utaifa wa zaidi ya wakimbizi 30,000 waliopoteza maisha haujaweza kufahamika.
342/