Taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Russia imeongeza kuwa, kwa mujibu wa aina ya Omicron na virusi vya awali kabisa vilivyogunduliwa huko Wuhan China, Chuo Kikuu cha Boston cha nchini Marekani kimezalisha virusi vipya ambavyo husababisha ugonjwa wa corona.
Taarifa hiyo imeendelea kubainisha kuwa, virusi hivyo vilivyobadilishwa vimesababisha asilimia 80 ya vifo kwa sampuli za wanyama zilizofanyiwa majaribio na kusababisha dalili zisizo za kawaida katika neva na uharibifu mkubwa wa mapafu.
Taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Russia imebainisha kuwa: majaribio ya kinga ya mwili yaliyofanywa kwa wanyama hao yameonyesha kupungua mara 11 kwa uwezo wao wa mwili wa kukabiliana na vimelea vya maradhi na kutofanya kazi kwa chanjo zilizopo.
342/