Gazeti la The Guardian, ambalo ni mojawapo ya vyombo vya habari vilivyobaguliwa na kuondolewa katika timu ya wanahabari ya Suella Braverman, limeandika katika ripoti yake kwamba, "gazeti hilo na mengine ya kiliberali, yamezuiwa kuwa katika safari hiyo iliyofadhiliwa kwa bajeti ya umma."
Ripoti hiyo inasema, kabla ya safari yake ya kwenda Rwanda siku ya Ijumaa, Suella Braverman alidai kwamba sera yake tata ya kuwafukuza wanaotafuta hifadhi nchini Uingereza na kuwapeleka Rwanda "itatumika kama kizuizi dhidi ya safari hatari na zisizo halali za wahamiaji."
342/