Main Title

source : Parstoday
Alhamisi

15 Juni 2023

15:59:41
1373307

Marekani yakiri; Vikwazo vimepunguza matumizi ya dola duniani

Waziri wa Hazina ya Taifa ya Marekani amekiri kuwa, vikwazo vya Washington vinaelekea kusambaratisha ukiritimba na matumizi ya safaru ya dola katika miamala ya kibiashara duniani.

Janet Yellen amesema hayo mbele ya Kamati ya Fedha ya Kongresi ya Marekani na kueleza kuwa, vikwazo vya Washington vimepelekea nafasi ya sarafu ya dola katika miamala na mabadilishano ya kibiashara kuporomoka kwa kuwa aghalabu ya nchi zinafadhilisha kutumia sarafu nyingine na njia mbadala.

Waziri wa Fedha wa Marekani ameiambia kamati hiyo ya Kongresi kuwa, "Haistaajabishi kuona nchi zinazohofia kuathiriwa na vikwazo vyetu zinatafuta mbadala wa dola."

Duru za kiuchumi zinaarifu kuwa, wafanyabiashara wa mafuta duniani hivi karibuni wameanzisha kampeni ya kutumia sarafu mbadala, na kuachana na dola ya Marekani katika miamala yao. 

342/