Main Title

source : Parstoday
Jumatatu

3 Julai 2023

20:21:09
1376911

Balozi wa Kenya Iran atembelea "Bustani ya Makumbusho ya Naderi" mjini Mashhad

Balozi wa Kenya nchini Iran ametembelea Jumba la Bustani ya Makumbusho ya Naderi lililoko mjini Mashhad, Mkoa wa Khorasan Razavi.


Ehsan Zohre Vandi, Mkurugenzi wa Turathi za Kiutamaduni katika Idara Kuu ya Turathi za Kiutamaduni, Utalii na Sanaa za Mikono ya Khrasan Razavi, amesema: Joshua Iguta Gatimu, balozi wa Jamhuri ya Kenya hapa nchini Iran, leo ametembelea eneo la Bustani ya Makumbusho ya Utamaduni na Historia ya Naderi mjini Mashhad.   Katika mahojiano na IRNA, Zohre Vandi ameongeza kuwa: katika ziara hiyo, na baada ya kupatiwa maelezo ya sehemu ya historia za enzi za Nader Shah Afshar na pia kujua sifa maalumu za kisanii za bustani hiyo ya makumbusho, balozi wa Kenya na ujumbe aliofuatana nao wamevutiwa na kusifia historia ya Naderi.   Kuhudhuria maonyesho ya sanaa za mikono ni sehemu nyingine ya programu ya ziara ya balozi wa Kenya na ujumbe wake kwenye jumba la kitamaduni na la kihistoria la Makumbusho ya Bagh-Nader, ambapo walipata fursa ya kuelewa zaidi aina mbalimbali za bidhaa na sanaa za jadi za Iran. Balozi wa Kenya nchini Iran Joshua Gatimu

Jumba la kumbukumbu la kiutamaduni na kihistoria la Bagh-Naderi Museum liko kwenye makutano ya barabara ya Mashahidi wa Mashhad umbali wa mita 500 kutoka mahali ilipo haram tukufu ya Imam Reza AS.
Kaburi la Nader liko katika sehemu kuu ya Ibn Bagh ya makumbusho hiyo na kando ya kaburi hilo, kuna kumbi kuu mbili.

Moja ya kumbi hizo ni Jumba la Makumbusho la Silaha za Kale, ambapo silaha za zama tofauti za historia ya Iran zinaonekana katika jumba hilo la makumbusho.
Halikadhalika, picha za uchoraji zilizopambwa kwa taswira za Nader Shah akiwa vitani na nyaraka za hati maridadi zilizoandikwa kwa mkono ikiwemo historia ya safari za dunia za Naderi ni turathi zingine adhimu za kihistoria zilizoko katika makumbusho hayo.

Ukumbi mwingine ni wa makumbusho ya athari, nyaraka na vifaa vya utawala wa Nader Shah.

Katika makumbusho hiyo kuna kaburi pia la Kanali Mohammad Taqi Khan Pesian, jemadari mzalendo wa Iran.../