Main Title

source : Parstoday
Jumatatu

17 Julai 2023

16:35:35
1380053

Russia yasitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya nafaka ya Bahari Nyekundu

Ikulu ya Kremlin imetangaza kuwa Russia imesitisha ushiriki wake katika makubaliano ya kuruhusu meli ya Ukraine iliyobeba nafaka kuvuka Bahari Nyeusi kuelekea maeneo ya dunia yanayokabiliwa na njaa kwa ajili ya kufikisha bidhaa hiyo, hatua ambayo ni pigo kwa usalama wa chakula duniani, kutokana na ongezeko la bei kufuatia uvamizi wa Moscow dhidi ya Kyiv.

Umoja wa Mataifa na Uturuki zilisimamia mapatano ya kihistoria kati ya Ukraine na Russia mnamo Julai mwaka jana, ambayo yalifuatana na makubaliano mengine tofauti ya kuwezesha usafirishaji wa chakula na mbolea ya Russia ambayo Moscow inasisitiza kuwa hayajatekelezwa.

Mkataba wa Bahari Nyeusi umerefushwa mara kadhaa lakini ulipangwa kumalizika leo Jumatatu jioni.

"Makubaliano ya Bahari Nyeusi yamekoma kuwa halali kisheria leo," msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov aliwaambia waandishi wa habari alasiri ya leo.

Peskov ameongezea kwa kusema: "kwa bahati mbaya, sehemu ya makubaliano haya ya Bahari Nyeusi kuhusiana na Russia haijatekelezwa hadi sasa, kwa hivyo utekelezwaji wake umehitimishwa".

Russia imeifahamisha Uturuki, Ukraine na Umoja wa Mataifa kwamba inapinga kurefusha mkataba huo. Hayo ni kwa mujibu wa Maria Zakharova, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Russia.

342/