Main Title

source : Parstoday
Jumapili

13 Agosti 2023

17:38:09
1386795

Idadi ya waliofariki Hawaii kutokana na moto mkubwa wa karne kutokea Marekani wafikia 93

Idadi ya watu waliofariki kutokana na moto mkubwa wa msituni uliotokea Maui kisiwani Hawaii ilifikia 93 jana Jumamosi, kulingana na tovuti ya Kaunti ya Maui, na kuufanya kuwa moto mbaya zaidi kuwahi kutokea Marekani katika muda wa zaidi ya karne moja, huku kukiwa na uwezekano wa idadi ya vifo kuongezeka.

Kiwango cha uharibifu uliosababishwa na moto huo kilikuja kubainika zaidi siku nne baada ya kuusawazisha na kuufanya majivu mji huo wa kihistoria wa mapumziko, kuteketeza majengo na kuyeyusha magari. Kulingana na Shirika la Serikali Kuu ya Marekani la Usimamizi wa Masuala ya Dharura (FEMA) gharama za kuujenga upya mji wa Lahaina zinakadiriwa kufikia dola bilioni 5.5, huku zaidi ya majengo 2,200 yakiharibiwa au kuteketezwa na zaidi ya ekari 2,100 kuchomwa moto. Gavana wa Hawaii Josh Green ameeleza katika mkutano na waandishi wa habari kuwa idadi ya vifo itaendelea kuongezeka huku waathiriwa zaidi wakiendelea kupatikana.Idadi ya vifo vilivyotokana na moto huo uliozuka siku ya Jumanne iliyopita imelifanya tukio hilo kuwa janga baya zaidi la kimaumbile kukikumba kisiwa cha Hawaii, kuliko gharika ya tsunami iliyoua watu 61 mnamo 1960, mwaka mmoja baada ya kisiwa hicho kuwa jimbo la Marekani.

 Idadi mpya ya vifo iliyotolewa hadi sasa imeipita pia ya watu 85 walioafariki katika moto uliotokea mwaka 2018 katika mji wa Paradise, California, na kuwa idadi kubwa zaidi ya vifo vilivyosababishwa na moto wa nyika tangu ule wa mwaka 1918, wakati moto wa Cloquet huko Minnesota na Wisconsin uliposababisha vifo vya watu 453.../

342/