Main Title

source : Parstoday
Jumanne

29 Agosti 2023

17:16:19
1389917

Russia: Wanachama wote wa BRICS wana hadhi sawa

Mikhail Ulyanov, mwakilishi wa kudumu wa Russia katika mashirika ya kimataifa, amelilinganisha kundi la BRICS na mashirika yaliyo mfano wake ya Magharibi na kusema: "Ndani ya BRICS hakuna kiongozi wa ndani au wa nje, na wanachama wote wa kundi hili wana hadhi sawa".

Ulyanov ameeleza katika ujumbe alioandika kwa muundo wa suali kwenye mtandao wa kijamii "X" (Twitter ya zamani): tofauti gani kuu iliyopo kati ya taasisi za Magharibi (Kundi la G7, NATO, Umoja wa Ulaya, n.k) kwa upande mmoja na BRICS kwa upande mwingine?


Akaongezea kwa kusema: "Wanachama wote wa BRICS wana hadhi sawa. Je, unaweza kusema vivyo hivyo kuhusu taasisi za Magharibi?"

Katika mlinganisho unaofanana na huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov naye pia amesema, tofauti kati ya BRICS na G7 au miungano mingine yenye mielekeo ya Magharibi ni kwamba wao wote wanaiangalia Marekani.

Mwanadiplomasia mkuu wa Russia ameongezea kwa kusema: Viongozi wa BRICS wanashughulikia masuala halisi, wakati wanasiasa wa Magharibi na waandishi wao wa habari wanapendezwa zaidi na kutikisa ndimi zao.

Akizungumzia wanasiasa wa nchi za Magharibi na waandishi wao wa habari walioizungumzia BRICS kwa dharau Lavrov amesema: "hii inaonesha kuwa wanatikisa ndimi zao tu, wakati sisi tunatumia akili zetu na kushughulikia masuala halisi."

BRICS ni jina la kundi la nchi zenye uchumi unaoichipukia na kukua. Jina hili linatokana na herufi za kwanza za majina ya Kiingereza ya nchi wanachama ambazo ni Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini.

Katika mkutano wa hivi majuzi, ambao uliandaliwa na Afrika Kusini na uliofanyika katika mazingira ya makabiliano makali kati ya Russia na China kwa upande mmoja mkabala na Marekani na Ulaya kwa upande mwingine, maombi ya uanachama wa nchi sita yalikubaliwa. Ifikapo 2024, nchi sita za Iran, Argentina, Ethiopia na nchi tatu za Kiarabu za Muungano wa Falme za Kiarabu, Saudi Arabia na Misri zitaongezwa kwenye kundi hilo.../

342/