Main Title

source : Parstoday
Jumatatu

4 Septemba 2023

18:41:07
1391159

Matamshi ya Papa Francis akisifu utamaduni wa Russia yamuweka pabaya

Matamshi yaliyotolewa hivi karibuni na Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, akisifu historia na utamaduni wa Russia, yameliweka jina lake katika orodha nyeusi ya maadui wa Ukraine.

Shirika la habari la IRNA limeripoti kuwa, tovuti ya Kiukreni ya Myrotvorets, ambayo huchapisha habari za kibinafsi za waandishi wa habari na watu mashuhuri kutoka nchi tofauti za ulimwengu ili eti kutambulisha maadui halisi wa nchi hiyo, imeorodhesha jina la kiongozi wa Wakatoliki duniani, Papa Francis katika orodha yake nyeusi kwa sababu ya matamshi yake yanayounga mkono historia na utamaduni wa Russia.

Ripoti hiyo imesema, tarehe 25 Agosti, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Vijana, Papa aliwaambia vijana waliokusanyika huko St. Petersburg, nchini Russia, kwamba: Msisahau utambulisho wenu. Ninyi ni warithi wa Urusi Kubwa, watakatifu wa Urusi Kubwa, wafalme wa Urusi Kubwa, Peter the Great na Catherine II.

Akihutubia vijana hao wa Russia, Papa aliongeza kusema kuwa: "Ninyi ni warithi wa Urusi, songeni mbele na mjivunie mtindo wenu wa maisha na Urusi wenu, na muwe na furaha."

Matamshi haya ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani yameibua mijadala mingi katika nchi za Magharibi zinazoiunga mkono Ukraine na kwa msingi huo wananchi wa Ukraine wameliweka jina la Papa Francis katika orodha ya maadui wa nchi yao. 

Miongoni mwa watu mashuhuri waliowekwa kwenye orodha nyeusi ya tovuti ya Kiukreni ya Myrotvorets ni pamoja na Henry Kissinger, waziri wa mambo ya nje wa zamani wa Marekani, na Silvio Berlusconi, aliyekuwahi kuwa waziri mkuu wa Italia.

342/