Catherine Colonna amesema katika mahojiano na gazeti la Le
Monde kwamba: "Vita vya Ukraine vitakapomalizika, itakuwa muhimu kwa
viongozi wa nchi za Magharibi kuanisha muundo wa usalama unaoheshimu
maslahi ya Russia."
Msimamo huu wa serikali ya Ufaransa unakwenda kinyume na ahadi ya serikali ya Paris ya kuiunga mkono Kiev kwa gharama yoyote ile.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ufaransa ameongeza kuwa: "Ukweli, historia na jiografia vyote vinaonyesha kwamba Russia iko katika bara la Ulaya. Hivyo tunahitaji kutafuta njia ya kuanzisha upya mfumo thabiti wa usalama unaozingatia maslahi na amani ya pande zote."
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, amesisitiza tangu mwaka jana kwamba Ulaya inapaswa kujadili "jinsi ya kutoa dhamana kwa Russia watakati itakaporejea kwenye meza ya mazungumzo".
342/