Sergei Shoigu alitoa takwimu hizo jana Jumanne alipohutubia
hadhara ya makamanda wa kijeshi wa nchi hiyo na kutangaza kwamba jeshi
la Ukraine limepoteza wanajeshi 66,000 na silaha 7,600 tangu
lilipoanzisha operesheni za kujibu mapigo ya mashambulio ya Russia.
Shoigu ameendelea kueleza kwamba licha ya kupata hasara kubwa,
serikali ya Ukraine inajaribu kuendelea na operesheni zake za
kujibu mashambulio ya Russia.
Waziri wa Ulinzi wa Russia ameongeza kuwa, vikosi vya jeshi la nchi hiyo vimeteketeza makombora 159 aina ya Hymars, zaidi ya ndege elfu moja zisizo na rubani na makombora elfu kumi na tatu aina ya cruise katika operesheni za kijeshi ilizotekelezea ndani ya ardhi ya Ukraine katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
Siku ya Jumatatu, Wizara ya Ulinzi ya Russia ilitangaza kuwa katika
muda wa saa 24 zilizopita, jeshi la nchi hiyo limezima mashambulio 13
ya jeshi la Ukraine na wanajeshi 650 wa Ukraine wameuawa katika
makabiliano hayo.../
342/