Kwa
mujibu wa ripoti ya Al-Ahad, mabuldoza ya utawala wa Kizayuni
yakkiungwa mkono na jeshi la utawala huo ghasibu, yamebomoa nyumba na
vituo vya viwanda vya Wapalestina mashariki mwa Baytul-Muqaddas
inayokaliwa kwa mabavu. Kitendo hicho kisicho cha kibinadamu, kinajiri
siku mbili tu baada ya utawala ghasibu wa Kizayuni kubomoa au kutaifisha
majengo 33 ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na
Quds inayokaliwa kwa mabavu kwa kisingizio cha kutokuwa na kibali cha
ujenzi.
Utawala wa Israel unabomoa nyumba za raia wa Kipalestina katika eneo hilo lengo likiwa ni kuwaweka chini ya mashinikizo na kuwafukuza raia hao katika eneo hilo.
Utawala haramu wa Israel umekuwa ukibomoa nyumba za raia wa Palestina na kujenga vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi mahali pake lengo kuu likiwa ni kubadili muundo wa kijiografia wa maeneo ya Palestina na kuyapa maeneo hayo sura ya Kiyahudi.
Hii ni licha ya kwamba, azimio nambari 2334 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linataja shughuli zote za ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi iliyoghusubiwa ya Palestina kuwa ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo utawala haramu wa Israel unaendeleza ubabe wake kwa kuharibu nyumba za Wapalestina na kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni mahali pale na kutokana na uungaji mkono wa madola ya Magharibi hususan Marekani na udhaifu wa Umoja wa Mataifa na baraza lake la usalama.
342/