Sheikh Ibrahim Zakzaki amesema
hayo katika mahojiano maalumu aliyofanyiwa na shirika la habari la Iran
Press mjini Abuja na kuongeza kuhusu umuhimu wa ujumbe wa maadhimisho ya
Arubaini ya Imam Husain AS kwamba, kujitolea muhanga mtukufu huyo na
Ahlul Bait wa Mtume Mtukufu SAW na wafuasi wao watiifu katika jangwa la
Karbala mwaka 61 Hijria, ni muhimu sana kwa ajili ya kufikia ushindi wa
uadilifu na wa haki dhidi ya dhulma na ukandamizaji duniani na njia
pekee ya kuweza kuokoka mwanadamu ni kuendeleza muqawama kama wa Imam
Husain AS.
Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria vile vile ametoa mkono wa pole kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na kwa umma mzima wa Kiislamu kwa mnasaba wa kumbukumbu ya Arubaini ya Imam Husain AS.
Amesisisitiza kuwa, watu wa zama hizi wanahitajia mno kujitolea katika njia ya haki kama alivyojitolea Imam Husain AS na wafuasi wake katika jangwa la Karbala mwezi 10 Muharram mwaka 61 Hijria.
Athari za muqawama na mapambano ya Imam Husain AS zimebakia hai hadi leo na zitabakia milele hadi mwisho wa dunia. Imam Husain AS alimwaga damu yake katika njia ya ukombozi na kuwa kigezo bora kwa kila mpigania ukombozi duniani awe Muislamu na hata wasio Waislamu.
Sheikh Ibrahim Zakzaki ameongeza kuwa, kitu ambacho Imam Husain AS alikipigania na kuwaga damu yake kwa ajili yake kuna siku kitatimia tu na hicho si kitu kingine ghairi ya ushindi kamili wa uadilifu na haki dhidi ya dhulma.
342/