Kwa mujibu wa Reuters, Naibu Waziri wa Nishati wa Russia Pavel
Sorokin ameeleza katika taarifa kwamba, marufuku hiyo ni ya muda
usiojulikana na hatua zaidi zitategemea kutoshelezeka kwa soko la ndani.
Sorokin ameongezea kwa kusema: kizuizi hicho cha muda kitajaza soko la ndani la mafuta na kupunguza bei yake kwa watumiaji.
Kulingana na ripoti hiyo, usafirishaji wa petroli na dizeli kwa nchi nne
za Belarus, Kazakhstan, Armenia na Kyrgyzstan haujumuishwi katika
marufuku hiyo iliyotangazwa na Moscow.
Katika miezi iliyopita, Russia imekabiliwa na uhaba wa mafuta ya petroli
na dizeli, ambao hatimaye umepelekea kuongezeka kwa bei ya nishati
hizo.
Hali hiyo ya ughali wa nishati imekuwa mbaya zaidi katika baadhi ya
sekta za kilimo kusini mwa nchi, ambazo ziko katika msimu wa mavuno.
Wadadisi wa mambo wanasema, matengenezo ya viwanda vya kusafisha mafuta
na kushuka kwa thamani ya ruble ya Russia ambayo huchochea usafirishaji
wa mafuta nje, ni miongoni mwa mambo ambayo yamesababisha mvutano katika
soko la ndani la mafuta la Russia.../
342/