Main Title

source : Parstoday
Ijumaa

22 Septemba 2023

15:57:49
1395019

Kiongozi wa Guinea: Mataifa ya Magharibi komeni kujifanya walimu wa demokrasia

Kiongozi wa kijeshi wa Guinea, Kanali Mamady Doumbouya, amesema mtindo wa Magharibi wa demokrasia haufanyi kazi barani Afrika na ametetea hatua ya kuingilia kijeshi.

Kiongozi huyo wa mpito wa Guinea ameliambia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York kwamba bara hilo lilikuwa likiteseka kutokana na "mfano wa utawala uliotwikwa juu yetu" na ambao "hauendani na hali halisi ya mambo".

"Wakati umewadia muache kutusomea na kutufanya kama watoto," aliongeza.

Kanali Doumbouya alichukua mamlaka katika mapinduzi mwaka wa 2021, na kumuondoa madarakani Rais Alpha Condé.

Alitetea hatua hiyo katika kikao cha Umoja wa Mataifa akisema ni "kuokoa nchi yetu kutokana na machafuko kamili".

Wakati huo, habari za mapinduzi zilipokelewa kwa furaha na umati wa watu katika mji mkuu, Conakry, kwani wengi walikuwa wamefarijika kwamba Rais Condé alikuwa ameondolewa.

Lakini nchi hiyo iliondolewa katika jumuiya ya kikanda, Ecowas, baada ya jeshi kuchukua hatamu, huku viongozi wa kikanda wakitaka kurejeshwa kwa utawala wa kiraia.

Rais wa zamani wa Guinea Alpha Conde aliyeondolewa madarakani katika mapinduzi ya kijeshi mwaka juzi baadaye aliachiliwa huru kutoka kifungo cha nyumbani baada ya ushikiliwa kwa takkribani wikii moja.

Guinea ni miongoni mwa nchi kadhaa za magharibi na kati mwa Afrika ambazo zimeshuhudia mapinduzi katika miaka ya hivi karibuni zikiwemo Mali, Burkina Faso, Niger na Gabon. Mapinduzi hayo yalilaaniwa vikali na Ecowas, Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa. 

342/