Hujjatul-Islam wal-Muslimin Kazem Sediqi amesema katika hotuba za Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran kwamba waziri mkuu mhalifu na mtenda jinai asiye na akili wa utawala wa Kizayuni hubomoa nyumba za watu kila mara, kwa hivyo kujihami kulikofanywa ni jambo la kimaumbile. Kwa mujibu wa ISNA, Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran ameongeza kuwa: Kwa muda wa miaka 70, nyumba za watu wa Gaza zimebomolewa, na wao wenyewe wameachwa bila makazi, wameuliwa na kuwekewa mzingiro. Hujjatul-Islam wal-Muslimin Seddiqi amebainisha kuwa: Wazayuni wana kila aina ya vifaa kama vile ukuta wa kizuizi, ambao wametumia mamilioni ya dola kuujenga na ambao hauna tofauti na ukuta wa Khaybar. Wameweka pia minara ya uangalizi, vitengo vya upelelezi, ndege zisizo na rubani za doria, wanapatiwa misaada ya kiintelijensia na kijasusi na Marekani na nchi kadhaa za Magharibi na wanapeleleza pia laini za simu za Wapalestina.Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran ameendelea kufafanua kwamba: Wazayuni hawakudhani kama maelfu ya wapiganaji wangeweza kuvivuka vizuizi hivyo kama umeme na kuziteketeza kambi za kijeshi na kuwaangamiza askari wa utawala unaoikalia Quds kwa mabavu na kurejea Gaza wakiwa na mateka chungu nzima.
342/