Main Title

source : Parstoday
Jumanne

26 Desemba 2023

17:10:28
1423948

Lukashenko: Russia yakamilisha zoezi la kuikabidhi Belarus shehena ya silaha za nyuklia za kitaktiki

Rais wa Belarus amesema kuwa Russia imekamilisha zoezi la kukabidhi Belarusia shehena ya silaha za nyuklia za kitaktiki ambazo zimetumwa nchini humo kwa lengo la kukabiliana na mashambulizi yoyote yanayoweza kutekelezwa na Mungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (Nato).

Rais Alexender Lukashenko wa Belarus alisema jana huko St. Petersburg katika hotuba yake katika Mkutano wa Jumuiya ya Kiuchumi inayoongozwa na Russia bila ya kutoa maelezo zaidi kuhusu idadi ya silaha hizo zilizotumwa au mahali zilipopelekwa kwamba: Russia ilikamilisha zoezi la kuikabidhi Belarus silaha za nyuklia za kitaktiki mnamo mwezi Oktoba mwaka huu. Alipoulizwa kwa nini shehena ya silaha hizo imekabidhiwa nchi yake, Rais Alexender Lukashenko pia amesema: Hatua hiyo imechukulikwa ili kuzuia uchokozi wa Poland ambayo ni mwanachama wa Muungano wa Nato. Russia ilisisitiza kabla ya kujiri zoezi la kuipatia Belarus silaha za nyuklia za kitaktiki kwamba nchi hiyo ndiyo itakayosimamia matumizi ya silaha hizo.  

342/